Kumbe tunahesabu awamu za Serikali bila kuwa na sheria au utaratibu maalum unaotuongoza? Si muhimu sasa kuweka utaratibu rasmi?

Kumbe tunahesabu awamu za Serikali bila kuwa na sheria au utaratibu maalum unaotuongoza? Si muhimu sasa kuweka utaratibu rasmi?

No. Amechukuwa awamu ya Magufuli anamalizia japo ni rais kamili. Tulifanya ''uchaguzi'' wa kutafuta serikali ya awamu ya tano, na ndiyo iliyoko bado madarakani. Awamu nyingine inaanza 2025.
Awamu ni kipindi alichohudumu rais sio miaka kwahiyo awamu ya Magufuli iliisha pale alipofariki hivyo Rais Samia hamalizii awamu ya yeyote bali ni yake.
 
Mimi nafikiri hivi,
Rais na makamu wa Rais ni pacha, ndio maana wanagombea pamoja.
Katiba inampa mamlaka makubwa Pacha wa kwanza na mamlaka madogo pacha wa pili,
Mathalani akifa makamu wa Rais, makamu atakayemrith hawezi kuwa Makamu wa Awamu ya sita atakuwa chini ya Rais wa Awamu ya tano,
Sasa amekufa Rais wa awamu ya Tano maana yake Makamu wa awamu ya Tano ndio anakuwa Rais wa awamu hiyo, kumalizia muda uliobakia, Japo kwa namba anakuwa Rais wa Sita.
Hakuna cha kumalizia wala nini, Magufuli amefariki na awamu yake imeisha mnateseka bure kwa kulazimisha kitu ambacho hamuwezi kukibadilisha.
 
Akili ndogo bhana!Badala ya kujadili mambo madogo ya awamu tujadili jinsi ya kunusuru Taifa hili na ufisadi wa kutisha unaofanywa na serikali ya CCM ya Samia.
202112.jpg
 
Sisi hatujawah kuw na utaratbu na tukausimamia yote hutegemea na nan yupo mbele na anasema nn hatun mising ya kusimamia sheria zetu

Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app
 
Imeandikwa wapi tuna-refer Jima la Raisi? Na serikali za kikoloni mbona hatuzihesabu na ziiongoza hii nchi?Nadhani mpaka hapa utakuwa umeona umuhimu au logic ya hizi awamu kuwa defined tena baada ya nchi yetu kuwa huru vinginevyo hata awamu ya Nyerere sio awamu ya kwanza bali tutasema serikali ya kikoloni ndio awamu ya kwanza.
Kwanza hata hiyo kuita awamu siyo hitaji la kisheria wala kikatiba. Kisheria na kikatiba, neno linalotambulika ni muhula. Huu ni muhula wa kwanza wa Rais Samia.

Neno awamu kwa mara ya kwanza lilianza kutumika wakati wa Mwinyi ili kutofautisha uongozi wa Mwalimu Nyerere na Mwinyi.

Katika matumizi, awamu haiangalii idadi ya miaka au mihula. Mwalimu aliongoza kwa miaka 24, ni awamu moja. Waliofuatia miaka 10 kila mmoja, ni awamu kamili. Magufuli miaka 5 na kidogo, ndipo awamu yake ilipoishia.

Kwa nini tusihesabu viongozi kabla ya uhuru - kabla ya uhuru hakukuwa na nchi, lilikuwa koloni la Mwingereza, na mkuu wa makoloni yote ya Uingereza alikuwa malkia. Kabla ya ukoloni, hakukuwa na nchi bali chiefdoms.
 
Hakuna cha kumalizia wala nini, Magufuli amefariki na awamu yake imeisha mnateseka bure kwa kulazimisha kitu ambacho hamuwezi kukibadilisha.
MAGUFULI AMEFARIKI LAKINI AWAMU YA URAIS ILIKUWA HAIJAISHA NDIO MAANA MAKAMU WAKE AMEPOKEA BILA UCHAGUZI.
SUALA SIO KUANGAIKA ILA NI FACTS.
 
MAGUFULI AMEFARIKI LAKINI AWAMU YA URAIS ILIKUWA HAIJAISHA NDIO MAANA MAKAMU WAKE AMEPOKEA BILA UCHAGUZI.
SUALA SIO KUANGAIKA ILA NI FACTS.
Ni facts pia hilo neno "awamu" hata kwenye katiba na sheria halitajwi wala kutafsiriwa na matokeo ndio huu mkanganyiko.
 
Kwanza hata hiyo kuita awamu siyo hitaji la kisheria wala kikatiba. Kisheria na kikatiba, neno linalotambulika ni muhula. Huu ni muhula wa kwanza wa Rais Samia.

Neno awamu kwa mara ya kwanza lilianza kutumika wakati wa Mwinyi ili kutofautisha uongozi wa Mwalimu Nyerere na Mwinyi.

Katika matumizi, awamu haiangalii idadi ya miaka au mihula. Mwalimu aliongoza kwa miaka 24, ni awamu moja. Waliofuatia miaka 10 kila mmoja, ni awamu kamili. Magufuli miaka 5 na kidogo, ndipo awamu yake ilipoishia.

Kwa nini tusihesabu viongozi kabla ya uhuru - kabla ya uhuru hakukuwa na nchi, lilikuwa koloni la Mwingereza, na mkuu wa makoloni yote ya Uingereza alikuwa malkia. Kabla ya ukoloni, hakukuwa na nchi bali chiefdoms.
Nafikiri tatizo hasa linalowasumbua baadhi ya watu ni mapenzi yao binafsi kwa Magufuli hivyo ni kama wanaona sifa zake anaenda kupewa mtu mwingine maana wakikumbuka hata huyo mpendwa wao alifanya hivyo hivyo kwani miradi yote pamoja na ile aliyoikuta taratibu zote zimekamilika na pesa tayari imepatikana lakini utekelezaji wake umeanza Magufuli akiwa rais basi sifa zote alizibeba yeye.
 
Kwanza hata hiyo kuita awamu siyo hitaji la kisheria wala kikatiba. Kisheria na kikatiba, neno linalotambulika ni muhula. Huu ni muhula wa kwanza wa Rais Samia.

Neno awamu kwa mara ya kwanza lilianza kutumika wakati wa Mwinyi ili kutofautisha uongozi wa Mwalimu Nyerere na Mwinyi.

Katika matumizi, awamu haiangalii idadi ya miaka au mihula. Mwalimu aliongoza kwa miaka 24, ni awamu moja. Waliofuatia miaka 10 kila mmoja, ni awamu kamili. Magufuli miaka 5 na kidogo, ndipo awamu yake ilipoishia.

Kwa nini tusihesabu viongozi kabla ya uhuru - kabla ya uhuru hakukuwa na nchi, lilikuwa koloni la Mwingereza, na mkuu wa makoloni yote ya Uingereza alikuwa malkia. Kabla ya ukoloni, hakukuwa na nchi bali chiefdoms.
... at least it makes sense! Kama Mwalimu alihudumu kwa miaka 24 na ni awamu moja; basi hata Magufuli aliyehudumu kwa miaka 5+ ni awamu kamili hence hata Samia atakayehudumu kwa miaka 5- ni awamu iliyokamilika.

Vitu viwili najifunza kwenye hili suala la AWAMU; kwamba, vitu vya msingi kama hivi (kama ni vya msingi kwa wote anyway) viwekwe kwenye sheria ili viwe na tafsiri moja inayoeleweka kwa wote.

Pili, ideas za kisiasa associated with a certain political affiliation vibaki huko huko badala ya kurasimishwa informally kuwa vya nchi. Awamu linaonekana kuwa suala la ki-CCM zaidi, libaki huko huko badala ya kulifanya kana kwamba ni suala la kitaifa (la wote).
 
MAGUFULI AMEFARIKI LAKINI AWAMU YA URAIS ILIKUWA HAIJAISHA NDIO MAANA MAKAMU WAKE AMEPOKEA BILA UCHAGUZI.
SUALA SIO KUANGAIKA ILA NI FACTS.
Kwani awamu kwako tafsiri yake ni nini?
 
Rais anayepokea kijiti kama imebaki miaka zaidi ya mitatu anahesabiwa ni awamu yake.Ila kama amepokea chini ya miaka miwili anahesabiwa anakamilisha awamu ya mtangulizi wake,Ndiyo maana anaruhusiwa kugombea mara mbili
 
Yaani tunaacha kujadili mambo ya msingi kama taifa- mfano tufanye nini ili tujikwamue na huu umaskini wa kujitakia (wakati nchi ni tajiri kwa raslimali), umaskini ambao umesababishwa kwa sehemu kubwa na viongozi wabinafisi, wala rushwa wanaoingia mikataba ya hovyo ya kulididmiza taifa; tunapoteza muda kujadili awamu ya 5 au ya 6?
Je, tukisha jua kuwa ni ya 5 au ya 6 itasaidia kuziondoa hizi changamoto zinazotukabili? Itasaidia kuyaondoa haya majizi na wala rushwa yaliyojaa nchini yakiwa yamejivika makoti ya uongozi katika ngazi mbalimbali ?

Nimekasirika sana. 😬😬😬
Kama mkinitukana poa tu.
 
Samia ni Raisi wa Sita wa Tanzania anayetawala katika awamu ya tano ya utawala.wa hii nchi awamu kwa tafsiri ya kimantiki ni kipindi cha uongozi wa sarikali (naomba tusitumia tafsiri ya uchanguzi ama kuhesabu namba ya viongozi) kwani Kwa dhana ya uchaguzi Nyerere na Mwinyi hawakuchaguliwa na wananchi hivyo dhana idadi au namba haina mashiko
Hivyo Nyerere ni Raisi wa awamu ya kwanza ya uongozi wa nchi iliyodumu kwa miaka 21, mwinyi ni Raisi wa awamu ya pili ya uongozi iliyodumu kwa miaka 10 kama ilivyokuwa kwa awamu ya tatu na awamu ya nne Zilizongozwa na Mkapa na Kikwete mpaka kufikia kwa Raisi wa tano aliyeongoza awamu ya Tano ya serikali ya hii nchi

Na hapa ndipo likaja swala la Samia katiba iko wazi kuwa makamu wa Raisi huwa mgombea mwenza hii inamaanisha hushirikiana na mgombea wa nafasi ya uraisi kuunda serikali majukumu yake pamoja na mengine ni kushika nafasi ya raisi anapokuwa hawezi kufanya majukumu yake na hasa kuwa raisi pale raisi anapofariki ....

Naomba nigusie kidogo swala la serikali kuundwa kwa mujibu wa katiba yetu raisi huunda(huunda sio hubadili) baraza la.mawaziri kwa kuanza na waziri mkuu na hii hutokea baada ya uchaguzi mkuu na ikitokea Raisi akalivunja baraza la mawaziri italazimu kuitishwa kwa uchaguzi ......

So far kwa ubora wa uelewa wangu Samia ni Raisi wa Sita Wa Tanzania katika awamu ya Tano ya uongozi wa serikali ya JMT siku akichaguliwana wananchi au akivunja serikali au akifanya.mageuzi na kuunda serikali yake mpya atakuwa raisi wa sita wa Tanzania katika awamu ya sita
 
Hili ni jambo dogo sana lakini limedhihirisha Tanzania ni nchi isiyo na watu makini hata kidogo. Hata mimi niliposikia wanasema ni awamu ya sita nilibaki mdomo wazi. Itawaje awamu ya sita wakati yeye amekuwa rais wa muda mpaka uchaguzi utakapofanyika 2025?

No. Amechukuwa awamu ya Magufuli anamalizia japo ni rais kamili. Tulifanya ''uchaguzi'' wa kutafuta serikali ya awamu ya tano, na ndiyo iliyoko bado madarakani. Awamu nyingine inaanza 2025.

Akuna cha awamu ya 6 hapa, ungeitishwa uchaguzi alafu atangaze serazake tuzipimei tuchague.
Tatizo wote mmekalili na hasomi katiba mkaielewa.
 
... with due respect; fafanua maana ya neno AWAMU; neno muhimu sana kwenye mnakasha huu! Awamu ndio nini? Vigezo vya ku-determine AWAMU ndio vipi?
Katiba haijatafsiri neno AWAMU lakini imeelezea AWAMU za utawala wa raisi ziweje ambapo imeeleza raisi anaweza tawala kwa kipindi cha awamu mbili tu, kila moja ikiwa na miaka tano.

Ibara ya 40(2), pia soma Ibara ya 42(2) zote za Katiba
 
Ndani ya CCM kuna watu wana akili ila hawapendi kuzitumia kila wakati...

Huu mjadala lengo lake ni kuhakikisha Samia hagombei 2025, na kuna watu watautumia kumkaanga Samia na majeshi yake ya kukodi.

Nadhani Sukuma Gang na Tema Lowassa ndio walioko Jikoni
 
... tena kwa ilani tofauti; Cabinets tofauti, Bunge tofauti, etc. Shida iko kwenye neno moja tu la msingi - AWAMU! What is awamu? Vigezo vyake ndio vipi? Hapo ndio tunafeli!
AWAMU ni miaka tano ya utawala wa raisi baada ya uchaguzi Mkuu. Na kwa Tz raisi anaruhusiwa kutawala kwa awamu mbili tu. Ibara ya 40(2) na 42(2) za Katiba
 
Katiba haijatafsiri neno AWAMU lakini imeelezea AWAMU za utawala wa raisi ziweje ambapo imeeleza raisi anaweza tawala kwa kipindi cha awamu mbili tu, kila moja ikiwa na miaka tano.

Ibara ya 40(2), pia soma Ibara ya 42(2) zote za Katiba
... mkanganyiko zaidi! Kwamba Rais (mmoja) anaweza kutawala kwa awamu mbili? Basi tuna awamu nyingi sana aisee! Kuondoa utata, Samia ni Rais wa 6 wa JMT; upuuzi wa awamu tupa kuleee! Wahuni wa CCM wanautumia kumyumbisha Rais!
 
Naomba nigusie kidogo swala la serikali kuundwa kwa mujibu wa katiba yetu raisi huunda(huunda sio hubadili) baraza la.mawaziri kwa kuanza na waziri mkuu na hii hutokea baada ya uchaguzi mkuu na ikitokea Raisi akalivunja baraza la mawaziri italazimu kuitishwa kwa uchaguzi ......
Hayo uliyosema sio kweli, Rais anaweza kulivunja baraza la mawaziri wakati wowote na wala hailazimiki ufanyike uchaguzi upya ili rais kuunda upya, Rais anaweza kulivunja na kuliunda upya baraza la mawaziri wakati wowote akiona kuna haja kufanya hivyo.
 
Back
Top Bottom