Kumbukizi: Sokoine ndiye alibomoa uchumi wa nchi, na utawala wa sheria. Sioni chochote cha kumsifu, urathi wake uandikwe upya

Uchumi uliporomoshwa na vita vya Kagera. Tulioshiriki vita vile runajua mengi acha kabisa. Kutoka Kagera hadi mpaka wa Sudan kwa Mguu huku tukisafisha vichaka. lshia hapo hapo dogo.
Tulikuwa wazalendo wa kweli.
Mgekuwa wazalendo msingeruhusu katiba ya kijinga kama hii ambayo imeruhusu mfumo kujaa majangili tupu
 
Wengine ni watoto wa juzi hawajui chochote kuhusu sokoine.
 
We boya kweli aisee. Nyerere wakati wenzie wanajenga uchumi yeye ni kwenda kupiganisha mavita yasiyo na faida kwetu matokeo yake nchi ikamshinda akaamua kuachia ngazi unamlaumu sokoine?
 
Kama ulitupa sukari mtoni ulikuwa na uhakika ni mali ya wizi, utashindwa kujieleza uliitoa wapi. Yote ni mafisadi, uliyeandika huu uzi kwani nawe ni fisadi? Hakika mafisadi hawakumpenda. Unakumbuka walala hoi walivyotoa machozi juu ya kifo cha Sokoine?
 

Kama uchumi mzuri ni wetu kuiba mali za umma ,kama uchumi mzuri ni watawala kutumia watoto wao ,wake zao kutorosha madini ,kupendelea watoto wao na marafiki zao. Kuuza ardhi ya umma kama yule aliyeuza ardhi yote ya Mkonge kwa familia ya kina Mohamed wakati ina mashine ,mkonge ,maofisi na nyumba zaidi ya elfu mia tano kwa bei ya nyumba moja tu . Kama uchumi mzuri ni kuwapa wageni kila kitu kwa bei nafuu halafu wananchi wazawa wanapandishwa kodi kila siku .
Kama uchumi mzuri ni kufanya biashara za magendo na ujambazi kama wetu wa mikoa ya mipakani walivyokua wanafanya halafu wanakwepa kodi na kupitisha mageni . Kama hayo ndio uchumi mzuri basi Hili nchi ilipaswa itawaliwe kwa karne moja mbele maana ina watu wahuni na wasioweza kujiongoza zaidi ya kuishi kama wanayama wa porini ,mwenye nguvu ndiye anayekula.

Sokoine ni tunu tuliyopewa na Mungu kuleta mapinduzi makubwa ya kujenga uzalendo.

Hii nchi ina rasilimali nyingi sana lakini wezi wamefanikiwa kuweka watu wao madarakani tangu walipomuua Karume kule Zanzibar na Sokoine bara.
Mpaka sasa wezi wamefanikiwa kuua uzalendo kwenye nchi hii kwa ubinafsi wa watawala kuua moyo wa kizalendo na sasa watanzania wanakua omba omba kwa watawala wanaowaibia mali zote na kuwaridhisha watoto wao na marafiki zao .

Sokoine hakujimilikisha mali za umma wala Nyerere . Hakupendelea watoto wake na Wake zake kama wanavyofanya wengine .

Kuna watu wameshika kiti miaka mitatu tu ni latrionea wa kutupa na sasa wanafanya kila mbinu kubaki madarakani . Hawa ni jamii ya P Diddy na ndio wanaosifia majizi na kuwatukana watu wema kwa sababu tu ya rushwa ya pesa na uchawa
 
Akikuwa hataki longolongo

Ova
 
M

ata halali hamna shida mradi wanalipa kodi sawa sawa!
Tatizo ni wale matajiri wanaopiga Dili za kufa mtu hao ndio wanaoitwa mafisadi !!
Hakuna mtu anayeweza kumuita Bakhressa fisadi !
Na wapo wengine kama Bakhressa vile vile hawaitwi mafisadi !
Fisadi akiwekeza kwa "mcha Mungu", huyo mcha Mungu hawi fisadi!!??
 
Akikuwa hataki longolongo

Ova
1. Aliwakuta watu wanaficha bidhaa na wengine wanatupa baharini kukwepa ushahidi, akawaambia hapana msitupe hizo bidhaa ziuzeni wala msiogope akawaambia polisi waachieni wauze msiwashike

2. Unajua Basi dała dała ilianza vipi? UDA hazikutosha, kukawa na watu binafsi na vibasi na vigari vyao wanabeba watu na kukimbia polisi. Sokoine baada ya kutembelea Posta akawa anashangaa hivi vigari vinabeba watu na kukimbia vikawa vinahatarisha maisha ya watu. Sokoine aliwafuata na kuwaambia msiogope bebeni watu kwa mpangilio. Akawaelekesa polisi dała dała wasishikwe. Wakati huo dollar shs 5. Ndiyo dała dała ikaanza rasmi.

This man was innovative
 
Alimteuaga babu yangu ndy alikuwa custodian mali zote walizokamata zlikuwa chini yake
Anasisimamia...
Nilipokuwa naongea na mzee stori za sokoine ni zaidi ya kitabu

Ova
 
Waliokutwa na Mche wa Sabuni Kisura au mbuni walikamatwa
 
Uko sahihi 100%. Ndo MAANA nchi kama marekani Hawa viongozi wakubwa LAZMA wawe matajiri...kiongozi aliezaliwa na kutopea ktk umaskini lazima anakuwa na Roho mbaya na matajiri wafanyabiashara ambao kimsingi ndo walioshikilia uchumi
 
Sokoine hakupendwa na Mafisadi kipindi kile na hata mafisadi wa sasa hawawezi kumpenda Sokoine na wala hawawezi kumpenda JPM milele. ! 😳🙌

Au nasema uongo ndugu zanguni ???!!
Mkuu kila siku unaimba mafisadi, mafisadi ndio kina nani??? Si uwataje tuwajue???

Mahakama ya mafisadi ina miaka 5 sasa hakuna fisadi hata mmoja aliyehukumia!!!

Tofauti zako za chuki kwa walionacho tulia nazo, kama kuna fisadi unamfahamu na una ushahidi usio na shaka mpeleke kwenye mahakama ya mafisadi!!!
 
Sokoine alikuwa kichaa tu kama magufuli

Nchi hii tuna bahati mbaya ya kupata viongozi vijana wanaoact in negative direction badala ya positive direction
Nadhani tynayo katibabovu sana
Hii si bahati mbaya.

Nchi yetu ina mfumo wa ku promote chawa.

Hivyo, watu serious hawawezi kutoboa katika mfumo huo.

Ndivyo mfumo ulivyo, si bahati mbaya.
 
Nilivyomsikiliza WARIOBA Jana ...nakazi kubwa yakujua sababu zakumsifia ni nini ilikuwa au ,hizo Sheria alitaka zimkamate NYERERE au kawawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…