Kumbukizi: Sokoine ndiye alibomoa uchumi wa nchi, na utawala wa sheria. Sioni chochote cha kumsifu, urathi wake uandikwe upya

Kumbukizi: Sokoine ndiye alibomoa uchumi wa nchi, na utawala wa sheria. Sioni chochote cha kumsifu, urathi wake uandikwe upya

Kama uchumi mzuri ni wetu kuiba mali za umma ,kama uchumi mzuri ni watawala kutumia watoto wao ,wake zao kutorosha madini ,kupendelea watoto wao na marafiki zao. Kuuza ardhi ya umma kama yule aliyeuza ardhi yote ya Mkonge kwa familia ya kina Mohamed wakati ina mashine ,mkonge ,maofisi na nyumba zaidi ya elfu mia tano kwa bei ya nyumba moja tu . Kama uchumi mzuri ni kuwapa wageni kila kitu kwa bei nafuu halafu wananchi wazawa wanapandishwa kodi kila siku .
Kama uchumi mzuri ni kufanya biashara za magendo na ujambazi kama wetu wa mikoa ya mipakani walivyokua wanafanya halafu wanakwepa kodi na kupitisha mageni . Kama hayo ndio uchumi mzuri basi Hili nchi ilipaswa itawaliwe kwa karne moja mbele maana ina watu wahuni na wasioweza kujiongoza zaidi ya kuishi kama wanayama wa porini ,mwenye nguvu ndiye anayekula.

Sokoine ni tunu tuliyopewa na Mungu kuleta mapinduzi makubwa ya kujenga uzalendo.

Hii nchi ina rasilimali nyingi sana lakini wezi wamefanikiwa kuweka watu wao madarakani tangu walipomuua Karume kule Zanzibar na Sokoine bara.
Mpaka sasa wezi wamefanikiwa kuua uzalendo kwenye nchi hii kwa ubinafsi wa watawala kuua moyo wa kizalendo na sasa watanzania wanakua omba omba kwa watawala wanaowaibia mali zote na kuwaridhisha watoto wao na marafiki zao .

Sokoine hakujimilikisha mali za umma wala Nyerere . Hakupendelea watoto wake na Wake zake kama wanavyofanya wengine .

Kuna watu wameshika kiti miaka mitatu tu ni latrionea wa kutupa na sasa wanafanya kila mbinu kubaki madarakani . Hawa ni jamii ya P Diddy na ndio wanaosifia majizi na kuwatukana watu wema kwa sababu tu ya rushwa ya pesa na uchawa
Toka tumepata uhuru kuna kipi cha maana chini ya utawala upi tumekifanya? Wakoloni mfano walijenga shule kubwa na nzuri ambazo sisi kwa karne hii nyingine tumezigeuza vyuo vikuu wakati ni shule za sekondari.
 
Hhh mkuu unakatisha tamaa..Shule YouTube
Hapana mkuu, mim nasema ukweli tu. Japo ukiangalia juu juu unaweza ona ni jambo la maana lakini tumeua elimu yetu kwa mambo ya kisiasa. Weka shule chache zenye tija na walimu wa kueleweka. Shule ya kata walimu wa Voda fast( crushing program) kama wakumbuka
 
Uchumi uliporomoshwa na vita vya Kagera. Tulioshiriki vita vile runajua mengi acha kabisa. Kutoka Kagera hadi mpaka wa Sudan kwa Mguu huku tukisafisha vichaka. lshia hapo hapo dogo.
Tulikuwa wazalendo wa kweli.
Huyu ni kichaa mwenye simu ya android asamehewe.
 
Uwaziri Mkuu wa Sokoine ulikuwa wa hovyo kuliko mawaziri wakuu wote tangu nchi ipate uhuru mpaka sasa.

Ni yeye, kama alivyosema Mzee Warioba, aliasisi sheria za hovyo kabisa, hovyo kabisa ambazo zilikiuka haki za binadamu. Utesaji mkubwa ulifanyika na yeye akiwa anangalia.

Upande wa uchumi, mali za watu ziliporwa, watu wakafilisiwa, biashara zilikufa nchi nzima. Hakika yeye ndiye kiini cha uharibifubwa uchumi wa nchi, badala ya kuujenga. Imagine nchi inatoka vitani, halafu ikawa chini ya Sokoine. Yeye akiona duka, anamkamata mwenye duka na kutaifisha bidhaa. Watu wakamwaga sukari katika mito na bahari, watu wakatupa hela maporini. Ulikuwa uongozi wa hovyo kabisa kuwahi kushuhudiwa, mbali na ule wa JPM.

Sioni chochote cha kujivunia kutoka kwake. Urathi wake umeandikwa na Salva Rweyemamu, sikutarajia afanye critical analysis ya uongozi wake zaidi ya kupuliza maumivu waoiyopitia watanzania.

Hii project ya uongozi Institute ni kama iko structured na iko scripted. Tunasubiri urathi ambao utamjadili Sokoine kwa uhalisia wake.
Mkuu yawezekana wewe ni 'mtoto wa 2000' kwa namna ya uandishi wako na ulivyoelezea jambo hilo kinafiki.

Kifupi ni kwamba, baada ya 'vita vya Kagera' na Nyerere kutangaza waTz 'kujifunga mkanda miezi 18', wafanya biashara mafisadi walitumia slogan hiyo kuficha bidhaa muhimu ionekane ugumu wa maisha umebarikiwa na Serikali.

Hali hiyo ilivuruga kabisa uchumi na maisha ya raia.

Hali ilikuwa ngumu mno takribani kwa miaka mitano(1980-1984).
Maduka yalikuwa totally empty, nguo sukari, sabuni, C. Oil etc etc havikuwepo madukani vilifichwa.

Sokoine alikuja kuchukua hatua ya kuwabana mafisadi walioficha bidhaa, ninasema walikuwa wameficha kwa sababu walivyosikia kuna operesheni hiyo wakavitoa vitu kwenye maghala yao usiku na kwenda kuvitupa.

Bidhaa nyingi zilitupwa zikiwemo na magunia ya pesa wakihofia kutiwa nguvuni wakikwepa mkono wa sheria.

Maelezo ya kisa hiki ni marefu sana,
Itoshe kusema kwamba kumlaumu Sokoine bila kupongeza juhudi zake za kupigania maisha ya waTz ni kumtendea dhulma.

Aliwabana mafisadi kwa manufaa ya waTz na siyo kusema kwamba katika zoezi hilo alitia mkono kujinufaisha kama viongozi wa sasa wanavyofanya, hapana.

na kifo chake kilikuwa ni pigo kuu kwa Raia na kilitikisa nchi.

Tangia kifo chake 1984 hadi leo sijawahi kusikia ama kusoma popote mtu kaandika akimlaumu Sokoine kwa ubaya wowote alioifanyia nchi na raia wake, isipokuwa wewe tu!

Karudie tena kusoma historia yake, ukiendelea kuleta ubishi wa kijuaji na stori zako za uongo hapa tutaelewa kuwa unatumika, kuna watu wapo nyuma yako kuchafua legacy ya Sokoine Waziri mkuu aliyependwa sana kwa dhati kabisa na raia wa Tz kutokana na utumishi wake uliotukuka.
 
Mbwa nyie toka Sokoine afe ni miaka 40 sasa,hakuna mlichoweza kugeuza?

Iko siku kwa kushindwa kumzalisha mkeo utasema sababu ni Sokoine


Nchi ina kila kitu lakini haisongi,wewe unaisaidiaje nchi yako? zaidi ni kushinda mtandaoni kulaumu kina marehemu, Sokoine alienda na nchi kaburini?
Nchi Ina utajiri wa Mashujaa mitandaoni, kulalamika na kukosoa kazi rahisi Sana.
 
Siku tukiamua kuwa wa kweli na kujifunza kutokana na makosa itakuwa rahisi zaidi kusonga mbele.
VAN ARKADIE, BRIAN. “THE TANZANIAN SOCIALIST EXPERIMENT: SERIOUS OPTION OR ROMANTIC DREAM?” PERSPECTIVES ON POLITICS, PRODUCTION AND PUBLIC ADMINISTRATION IN AFRICA: ESSAYS IN HONOUR OF OLE THERKILDSEN, edited by Anne Mette Kjær et al., Danish Institute for International Studies, 2015, pp. 255–71. JSTOR, http://www.jstor.org/stable/resrep30721.20. Accessed 2 Oct. 2024.
 
Kipindi anafanya hayo yote,Mwalimu alichukua hatua gani? Kulinda uchumi wa nchi ?
Hii Ni kweli, kukawa na kipindi Cha mikingamo redio Tanzania. Ila Ni waziri mkuu aliyependwa kuliko wote. Warioba ndiye aliyekuwa waziri wa sheria na mwanasheria mkuu wa Serikali, alichukua jukumu gani kwa sheria zile? Angejiuzulu ningemwelewa
 
Uchumi uliporomoshwa na vita vya Kagera. Tulioshiriki vita vile tunajua mengi acha kabisa. Kutoka Kagera hadi mpaka wa Sudan kwa Mguu huku tukisafisha vichaka. lshia hapo hapo dogo.
Tulikuwa wazalendo wa kweli.
Nina Mzee Mtaani hapa ana sema yeye ndio walikua Front line, ktk vita, baada ya vita Nyerere aka waambia sina cha kuwalipa
 
Uchumi uliporomoshwa na vita vya Kagera. Tulioshiriki vita vile tunajua mengi acha kabisa. Kutoka Kagera hadi mpaka wa Sudan kwa Mguu huku tukisafisha vichaka. lshia hapo hapo dogo.
Tulikuwa wazalendo wa kweli.
Ni upuuzi tupu.

Kwani kulikuwa na ULAZIMA gani kwa Tanzania katika kupigana vita hiyo?? Nchi ilinufaika na Nini au ilipata faida gani kutokana na vita hiyo?

Aliyewahi kuwa Rais wa Marekani Bw.
 
Back
Top Bottom