Kumdhibiti mpenzi wako!!...ni woga au ndo mapenzi??

Kumdhibiti mpenzi wako!!...ni woga au ndo mapenzi??

SnowBall

JF-Expert Member
Joined
Sep 13, 2011
Posts
3,052
Reaction score
2,842
Wanabodi natumaini nyote hamjambo!

Kwa muda mrefu stori nyingi zinazohusu mapenzi zimegubikwa na migogoro mingi inayotokana na wapenzi husika kuhisiana kukosa uaminifu baina yao. Kwa kuhisi kuwa wanaweza kuibiwa, wapenzi wengi wamekuwa wanawekeana 'njia' nyingi za kudhibitiana. Tumesikia 'stori' za kuwekeana 'tego' baina ya wapendanao..ili kwamba kama mmoja atatoka 'nje' basi anasie. Lakini sio hivyo tu..tunashuhudia pia wapenzi/wanandoa 'wanakagua' simu na pochi za wenza wao kwa nia ya kuhakikisha 'haibiwi mtu'. Kuna cases za baadhi ya wenza kuwafuata wenzi wao kwenye sehemu zao za kazi kwa nia ya kuji'expose' ili wajulikane. Kuna wenzi ambao wamepeana hadi 'password' za accounts zao za kwenye mitandao ya kijamii. Alimradi kinafanyika kila kiwezekanacho kuhakikisha 'udhibiti' upo.

Binafsi naamini 'binadamu hachungwi' na kwamba ukishaanza kumdhibiti au kumchunga mwenzio ni wazi kuwa wewe ni muoga wa mapenzi. Kama anakupenda anakupenda tu na kama anakuzuga atajulikana tu...Kuku wako mwenyewe manati la nini??...Lakini kuna wanaosema 'abiria chunga mzigo' hawa wanasema binadamu ni kiumbe asiyetabirika ..hivyo kufuatilia nyendo zake inasaidia 'kumstua' na kumrudisha kwenye mstari.

Hivi jamani kweli kuchungana na kudhibitiana ndio kuonyesha kuwa una mapenzi ya dhati kwa mwenzio?? au ni woga tu na kutojiamini!!!

Wasalaam!
 
yaani hapo vyote .ni haki yako lakini vilevile kutokujiamini inakuja tena but ultimately KUNGURU HAFUGIKI
 
Nafikiri kuna zaidi ya kupendwa, kuna familia iliyoanzishwa (watoto n all), kuna uchumi mlioinvest, kuna maradhi ya maambukizo hivyo vyote vinakufanya:-
1. Uendelee kuishi na spouse wako hata kama mapenzi yamepungua
2. Umchunge au kumbana asitoke nje na kuathiri yote yale juu.
Ila kiukweli, kumchunguza na kumefbiai mwenzako ni kutafuta ushahidi wa usaliti. Swali ukishajua unasalitiwa unafanya nini? Mimi ningetafuta ushahidi pale ninapotaka kuachana na mtu na sio kabla ya hapo.
 
Okay.. mwekundu nimekusoma!
But kuna wakati najiuliza..nini kinatangulia...moyo wa kutojiamini?...au dalili za usaliti?
Vyovyote iwavyo lazima kuna 'motive' inakusukuma kwenye kufanya jambo lolote..

yaani hapo vyote .ni haki yako lakini vilevile kutokujiamini inakuja tena but ultimately KUNGURU HAFUGIKI
 
Last edited by a moderator:
Nimekusoma Kaunga
Labda nikushukuru kwa kuwa wazi..unaposema kuwa 'kumchunguza mwenzi wako inakuja pale unapobaini dalili za usaliti'.
Lakini kama ulivyojiuliza ndo na mimi najiuliza...haya umejua kuwa 'anakusaliti' are you ready to bear the consequences?
Wakati mwingine hata kabla mtu hajaonyesha dalili hizo tayari mitego kibao...hofu ya nini???


Nafikiri kuna zaidi ya kupendwa, kuna familia iliyoanzishwa (watoto n all), kuna uchumi mlioinvest, kuna maradhi ya maambukizo hivyo vyote vinakufanya:-
1. Uendelee kuishi na spouse wako hata kama mapenzi yamepungua
2. Umchunge au kumbana asitoke nje na kuathiri yote yale juu.
Ila kiukweli, kumchunguza na kumefbiai mwenzako ni kutafuta ushahidi wa usaliti. Swali ukishajua unasalitiwa unafanya nini? Mimi ningetafuta ushahidi pale ninapotaka kuachana na mtu na sio kabla ya hapo.
 
Last edited by a moderator:
nachokiona mimi hapa ni kuwa udhibiti wa kiasi katika mapenzi ni kiungo cha msinngi kwani udhibiti huonyesha hali ya kujaliana kuthaminianaa pia upendo na hasa kuleta zile hisia za faraja za kwamba mume/mke au mpenzi wako hataki kukupoteza na pia anaamini kuwa wewe ni wake peke yake,so udhibit wa kiasi katika mapezni si kukosa kujiamini ila ni jambo ambalo huja tu tena bila mtu kujitambua kama ana mdhibiti mtu wake,yaani huja automatically,so kwa mimi sio mbaya ila isiwe toooo much coz too much is harmful.
 
Nimekusoma Kaunga
Labda nikushukuru kwa kuwa wazi..unaposema kuwa 'kumchunguza mwenzi wako inakuja pale unapobaini dalili za usaliti'.
Lakini kama ulivyojiuliza ndo na mimi najiuliza...haya umejua kuwa 'anakusaliti' are you ready to bear the consequences?
Wakati mwingine hata kabla mtu hajaonyesha dalili hizo tayari mitego kibao...hofu ya nini???

hofu nafikiri yachangiwa na mambo mengi ambayo ni pamoja na tabia ya mwenzi wako lkn pia mitazamo ya jumla ya jamii. Mfano kauli kama:
1. Hakuna mwanaume aliye mwaminifu.
2. Mwanaume ni polygamist in nature
3. Wanawake siku hizi si waaminifu
4. Wanawake wafanyakazi wanamegwa sana.
Haya maneno yanarudiwa rudiwa sana kiasi kwamba yanakaa kwa ubongo na matokeo yake hofu ya kumegewa, ibiwa inakutanda. Na mara zote, ukilitafuta sana tatizo lazima ulipate, hivyo dalili za kusalitiwa utaziona hata kama hazipo.
 
Last edited by a moderator:
hata kama binadamu hachungwi ,kudhibiti ni muhimu sana ili hata kama akitenda madhambi basi ni iwe karibu na mission impossible................

monitoring ya 24/7 inahusika sana kwenye mahusiano ya kudumu.
 
Blue G kimsingi kila mwanadamu anapaswa kuwa na nidhamu aliojijengea kwenye maisha yake.
Nidhamu ile inaambatana na uhuru wa kutenda na kuamua pasi na kushurutishwa...kuanza kudhibitiana inaweza kuonyesha 'udikteta' na kulazimishana kutenda hata yale tusiyoyaamini..huoni hii inatupeleka kwenye penzi la unafiki?
Na ukishakubali kudhibitika unaeza kujikuta unaishi maisha feki....

nachokiona mimi hapa ni kuwa udhibiti wa kiasi katika mapenzi ni kiungo cha msinngi kwani udhibiti huonyesha hali ya kujaliana kuthaminianaa pia upendo na hasa kuleta zile hisia za faraja za kwamba mume/mke au mpenzi wako hataki kukupoteza na pia anaamini kuwa wewe ni wake peke yake,so udhibit wa kiasi katika mapezni si kukosa kujiamini ila ni jambo ambalo huja tu tena bila mtu kujitambua kama ana mdhibiti mtu wake,yaani huja automatically,so kwa mimi sio mbaya ila isiwe toooo much coz too much is harmful.
 
Last edited by a moderator:
Snowball tatizo hapa neno kudhibiti ni relative term. Unapo dhibiti where do you cross the line na wapi ni acceptable?

Kwenye mahusiano "kudhibiti" ni moja ya ingredients za muhimu; kikubwa ni isiwe misused for ina mipaka yake. Unaposema kudhibiti haimaanishi, kumkaaba saana, kumchunga saana, kufuatilia saana, kumpekua saana OR kufanya yale yote ambayo huwa kero kwa wapenzi.

Kuna umuhimu wa kumlinda mpenzi wako kama ilivyo muhimu kulinda penzi lako. Mfano; inapotokea una mpenzi wako, anakuja mtu mwingine kutaka kumzoea zoea na kutaka kuwa nae karibu bila sababu zozote za msingi (na ukute yupo single OR hata hayupo single but inajulikana wazi ni tanga tanga) – hapo wapaswa kabisa kuingilia kati. Maana saa ingine wapenzi huweza kukusaliti kwa mitego aliyowekewa na si kwa kwenda kutafuta makusudi. Unapo ona such mitego; kama mpenziwe una haki ya kudhibiti au kumdhibiti.

Nikija suala la kuanza kuwa na shauku kwa mtu wako, nadhani hili huanza tokana na sababu Fulani za msingi – kama vile kubadilika mienendo, kusikia maneno ya watu, kuto kujiamini n.k. Si wote ambao wapo katika mahusiano wana mashaka na wapenzi wao.
 
Kumdhibiti mtu? mzima wa afya? na akili zake timamu!
hii kazi sitaifanya, hata kwa wanangu.
mamangu alikuwa anatuambia sisi tumeshakuwa watu wenye akili timamu tangu tulipoanza sekondari, na kwa maana hiyo hatamfwatilia mtu nyendo zake nje ya nyumbani, hana huo muda na hataki kuwa kichaa. la maana alikuwa anatuambia madhara ya kuwa na matendo maovu..... kupata mimba zisizotarajiwa, kuambukizwa magonjwa, kushindwa kuendelea vizuri na masomo na vitu kama hivyo. kila mtu alipewa uhuru wa kuchagua analotaka kulifanya. na ukweli sikuwahi kufanya lolote ambalo nilijua mama hapendi, sababu sikutaka kuingia kwenye matatizo aliyoyasema....
hata sasa nilishasema sichungi mtu, namchungaje kwanza? simu? ofisini? bar? safarini? kwa nini haswa nimchunge?
 
Okay.. mwekundu nimekusoma!
But kuna wakati najiuliza..nini kinatangulia...moyo wa kutojiamini?...au dalili za usaliti?
Vyovyote iwavyo lazima kuna 'motive' inakusukuma kwenye kufanya jambo lolote..
hebu jaribu utofautishe WIVU(ambao tunaambiwa ukipenda lazima uwe nao) na KUTOJIAMINI whats the difference Snowball
 
hofu nafikiri yachangiwa na mambo mengi ambayo ni pamoja na tabia ya mwenzi wako lkn pia mitazamo ya jumla ya jamii. Mfano kauli kama:
1. Hakuna mwanaume aliye mwaminifu.
2. Mwanaume ni polygamist in nature
3. Wanawake siku hizi si waaminifu
4. Wanawake wafanyakazi wanamegwa sana.
Haya maneno yanarudiwa rudiwa sana kiasi kwamba yanakaa kwa ubongo na matokeo yake hofu ya kumegewa, ibiwa inakutanda. Na mara zote, ukilitafuta sana tatizo lazima ulipate, hivyo dalili za kusalitiwa utaziona hata kama hazipo.

Wakati mwingine wasiwasi wangu unakuwa kwa yule unayehangaika kumchunga na kuweka mitego ya kumdhibiti..
Je, anaweza kuona 'cencern' yako au ataona ni usumbufu na kwamba 'humuamini' katika nyendo zake?
Je, huoni hii inaweza kupelekea mhisiwa kuamua kuwa 'victim' moja kwa moja kwa sababu mazingira ubayojenga yanaonyesha haaminiki. Kama ni mwanamke anaweza kuamua 'kukupa penzi la unafiki'...kumbuka pia mwanadamu anao utashi ambao hauondoki hata kama kaolewa/kaoa...Kuna mtu yeye ni msemaji tu...kuanza kumwekea mipaka ya usemaji wake ni kama kumdictate..ultimately ataishi na wewe a fake life kwa sababu hafanyi kile kilichomo ndani yake....
 
How do you do that in 24/7??

hata kama binadamu hachungwi ,kudhibiti ni muhimu sana ili hata kama akitenda madhambi basi ni iwe karibu na mission impossible................

monitoring ya 24/7 inahusika sana kwenye mahusiano ya kudumu.
 
Kuna umuhimu wa kumlinda mpenzi wako kama ilivyo muhimu kulinda penzi lako. Mfano; inapotokea una mpenzi wako, anakuja mtu mwingine kutaka kumzoea zoea na kutaka kuwa nae karibu bila sababu zozote za msingi (na ukute yupo single OR hata hayupo single but inajulikana wazi ni tanga tanga) – hapo wapaswa kabisa kuingilia kati. Maana saa ingine wapenzi huweza kukusaliti kwa mitego aliyowekewa na si kwa kwenda kutafuta makusudi. Unapo ona such mitego; kama mpenziwe una haki ya kudhibiti au kumdhibiti.
mtu anatakiwa ajue mipaka yake yeye mwenyewe, utamdhibiti mara ngapi?
na akishazoea kudhibitiwa basi ikatokea mitego ambayo wewe hujaiona basi atanaswa, sababu hakuna wa kumdhibiti.
rafiki yangu jiulize hapo ulipo ni mara ngapi umekutana na mitego ambapo mpenzi wako hajui? uliingia au uliweza kujinasua? kama uliweza kujinasua bila yeye kujua huko ndo kunaitwa kujitambua, na binadamu anatakiwa awe hivyo, ajitambue, yeye mwenyewe.
mimi sikubaliani kabisa kusema kuwa mtu aliingia majaribuni, ina maana hakujijua wakati anaingia? ni kwamba huyu jamaa anaingia majaribuni kwa kila mtego? kama mingine anaweza kuidhibiti, kwa nini huu aingie?
 
nachokiona mimi hapa ni kuwa udhibiti wa kiasi katika mapenzi ni kiungo cha msinngi kwani udhibiti huonyesha hali ya kujaliana kuthaminianaa pia upendo na hasa kuleta zile hisia za faraja za kwamba mume/mke au mpenzi wako hataki kukupoteza na pia anaamini kuwa wewe ni wake peke yake,so udhibit wa kiasi katika mapezni si kukosa kujiamini ila ni jambo ambalo huja tu tena bila mtu kujitambua kama ana mdhibiti mtu wake,yaani huja automatically,so kwa mimi sio mbaya ila isiwe toooo much coz too much is harmful.
tumetofautiana aisee....
yaani mimi ukionyesha kunidhibiti kwa kiasi naona huniamini, na siwezi kuendelea kuwa na mtu asiyeniamini.
Nashukuru mume wangu kaniacha free mno, yaani kupita maelezo, ananiamini sana. na huwezi amini sijawahi kupoteza uaminifu wangu kwake (sijui wake kwangu.....?)
 
AshaDii nimekusoma vizuri sana dadaangu..Kwanza hujambo?...long tyme ujue?
Back to the topic ..mie concern yangu ni kuwa hata kama tuko kwenye mahusiano/mapenzi..lakini as individuals kila mtu anao uhuru na nidhamu yake ya kutenda. Na beforehand natambua mtakuwa mshafahamiana vya kutosha kuhusu individuals characters..na kama mnaoana obvious kila mtu anakuwa amekubaliana na mwenzie.

Sasa wasiwasi wangu ni kile unachokiita 'ingredient muhimu ya penzi' kudhibitiana/kuchungana/kupelelezana..Na kimsingi hii inatokana na hofu..na hofu hapa ni kuwa umeshindwa kukubali kuwa mwenzi wako 'atavishinda' vishawishi?..Kwa nini umjengee hiyo dhana??. Bahati mbaya mwengine anakuspy bila hata kujua na anaweza ku-connect dots hata zisizokonektika..Unapendwa kuchungwa dadaangu??

Snowball tatizo hapa neno kudhibiti ni relative term. Unapo dhibiti where do you cross the line na wapi ni acceptable?

Kwenye mahusiano "kudhibiti" ni moja ya ingredients za muhimu; kikubwa ni isiwe misused for ina mipaka yake. Unaposema kudhibiti haimaanishi, kumkaaba saana, kumchunga saana, kufuatilia saana, kumpekua saana OR kufanya yale yote ambayo huwa kero kwa wapenzi.

Kuna umuhimu wa kumlinda mpenzi wako kama ilivyo muhimu kulinda penzi lako. Mfano; inapotokea una mpenzi wako, anakuja mtu mwingine kutaka kumzoea zoea na kutaka kuwa nae karibu bila sababu zozote za msingi (na ukute yupo single OR hata hayupo single but inajulikana wazi ni tanga tanga) – hapo wapaswa kabisa kuingilia kati. Maana saa ingine wapenzi huweza kukusaliti kwa mitego aliyowekewa na si kwa kwenda kutafuta makusudi. Unapo ona such mitego; kama mpenziwe una haki ya kudhibiti au kumdhibiti.

Nikija suala la kuanza kuwa na shauku kwa mtu wako, nadhani hili huanza tokana na sababu Fulani za msingi – kama vile kubadilika mienendo, kusikia maneno ya watu, kuto kujiamini n.k. Si wote ambao wapo katika mahusiano wana mashaka na wapenzi wao.
 
Last edited by a moderator:
How do you do that in 24/7??

mkuu namaanisha unafuatilia mwenendo wa maisha yake muda wote kujua yupo wapi anafanya nini yupo na kina nani , madhumuni ya matendo yake n.k................. njia unayotumia inaweza ikwa physically au kidigitalia zaidi...........

mkuu kuwa na mazoea ya kumuuliza mpenzi wako sasa hivi upo wapi , au kumjengea mazoea ya kuwa mnaagana kila unapotoka sehemu moja kwenda nyingine ni hatua kubwa sana katika kujua ukweli............

maswali ya kawaida , mepesi kujibu huwa yanatoa majibu magumu sana kwenye mahusiano............
 
Fixed Point na mimi ndo ninachokisema..unamdhibitije mwenzio?
Nadhani kuna haja ya kuwekana sawa na kila mtu amjue mwenzie beforehand..lakini hii habari ya 'uspy'..lolz
Kwa sisi wanaume naona hili limezidi sana..lakini kwa nini tufike huko?
Mie naona ile tu mwenzio kujua 'humuamini' inapunguza hata kile kilichokuwepo..

Kumdhibiti mtu? mzima wa afya? na akili zake timamu!
hii kazi sitaifanya, hata kwa wanangu.
mamangu alikuwa anatuambia sisi tumeshakuwa watu wenye akili timamu tangu tulipoanza sekondari, na kwa maana hiyo hatamfwatilia mtu nyendo zake nje ya nyumbani, hana huo muda na hataki kuwa kichaa. la maana alikuwa anatuambia madhara ya kuwa na matendo maovu..... kupata mimba zisizotarajiwa, kuambukizwa magonjwa, kushindwa kuendelea vizuri na masomo na vitu kama hivyo. kila mtu alipewa uhuru wa kuchagua analotaka kulifanya. na ukweli sikuwahi kufanya lolote ambalo nilijua mama hapendi, sababu sikutaka kuingia kwenye matatizo aliyoyasema....
hata sasa nilishasema sichungi mtu, namchungaje kwanza? simu? ofisini? bar? safarini? kwa nini haswa nimchunge?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom