Kumdhibiti mpenzi wako!!...ni woga au ndo mapenzi??

Kumdhibiti mpenzi wako!!...ni woga au ndo mapenzi??

nakuelewa sana unachosema my dear friend, lakini kuna mambo mengi sana hapa tunatakiwa kuyazingatia....
sisi ni binadamu na kama binadamu kuna mambo mengi sana ambayo tunatakiwa kuyafanya kukamilisha maisha yetu.
wakati nakua niliwahi kuishi na kakangu kwenye nyumba ya kupanga. kuna mama alikuwa anaishi na mumewe, huyo mama alikuwa mama wa nyumbani mwenye watoto. alikuwa anaishi na wasichana wa kazi wamsaidie watoto. mimi ni shuhuda, wasichana wake walikuwa wanafanya kazi za watoto tu, lakini yule dada alikuwa anapata shida sana na wasichana wa kazi sababu mumewe alikuwa anatembea na kila msichana anayemleta.
sisi wamama au hata hao wababa, kuna kipindi wanalazimika kuwa nje ya nyumbani kikazi au masomo, tuwe tunaambatana na wenzetu?


Kuna mipaka ya vitu. Siwezi mjudge huyo mama sababu sina all the details, ila mwisho wa siku alikua ni mdhaifu mno kwa mumewe. Mwanaume afanye makosa kama hayo mara moja, usamehe na isitokee tena! Anapofanya kwa kurudia tena kwa makusudi kabisa ndani mwako mwenyewe, anakutafuta ubaya... Believe me you.

Sasa hapo kwa huyo mama FP huoni kuwa kulikuwa ni muhimu kufanya udhibiti? So in this case unaona ni sawa tu mwanamke kumwachia mumewe kufanya maamuzi na hali anajua tabia yake fika?

Pengine alikua hadhibiti, ndio maana mume alikua na uwezo wa kulala na binti zake wa kazi. Ingawa naona ni disclaim kuwa kudhibiti haimaanishi hatafanikiwa lengo, ila unalipunguza makali.

Likija suala la kua mbali na mwenza, huwezi kwenda nae FP. Ila unapo ondoka unaenda kwenye kisomo unajua kabisa unakaa mwaka, huna haja ya kuacha mdogo wako wa kike au house gal ndani ya nyumba else by the time unarudi atakua tayari ni mke mwenzako. So hapo unadhibiti pale nyumbani, akitoka nje huko you can't help it, yale yaliyo ndani ya uwezo do it.
 
Dadaangu AshaDii sio kama nachukulia for granted..nooo!
Binafsi naamini ili mpaka uanze udhibiti lazima kuwe na 'hofu' moyoni mwako.
Tatizo mwanadamu huyu huyu akishajua anachungwa huwa anajenga kitu kama 'moral rebellion'
Anaanza kuweka hisia moyoni mwake kuwa haaminiki..na hii inapunguza upendo pia
Kwa mfano..kila wakati nikikupigia simu niwe nakuomba unipe niongee na watoto?..then?
Au unakagua kms za gari zilizotembea..na unalinganisha na umbali wa nyumbani kwenda ofsn?
Nasema haya kwa sababu nimeyaona...
Precaution ni nzuri but you need to be very smart..lakini kama hujapata sababu why giving yourself a headeache?




Mie mzima kabisa SnowBall na nafurahi kukuona hapa.

Naomba niseme kuna kitu nadhani unachukulia for granted. Kana kwamba wanadamu wote tunaweza behave the same way. Sio kweli. Ingekua hivyo it would have been so simple.

Mahusiano ya mapenzi ni sawa tu na mahusiano hata ya kikazi. Unaweza kuwa una kampuni yako, una mfanyakazi mchapa kazi sana na utendaji wake ni mzuri, anakufurahisha na kukuridhisha kwa kila namna kiasi kwamba hata wateja na wafanya kazi wenzake wanamkubali. BUT unatambua ana madhaifu, na dhaifu moja kubwa kuliko zote ni yeye kupenda pesa na saa ingine kufanya maamuzi damaging sababu tu anapenda pesa - Utamwachia tu sababu anapenda pesa ambayo inamfanya awe na maamuzi mabovu? Nadhani to most itakua hapana.

Utajitahidi kumdhibiti kwa kuhakikisha unaweka mazingira ya yeye kuwa na pesa consistent, aidha kwa kumpa mshahara mkubwa anao deserve, kumpa marupu rupu, na once in a while kumpa hata lecture ya matatizo ya kuweka pesa mbele. 🙂 Else unaweza jikuta unamfukuza kazi, unaishia kupata mfanyakazi mwingine ambae kichwa gongana na kukuaribia kabisa biashara.
 
Last edited by a moderator:
Kaunga, nimezungumzia housegal because ni rahisi. Kama mzazi au dada inauma sana kusikia mume katembea na mwanao or mdogo wako.

Hilo sasa ndio mfano mzuri saana. Kudhibiti ni muhimu saana, call me old fashioned or not, mdogo wangu wa kike, rafiki yangu wa kike azoeane but kwa heshima sana na mpenzi wangu. Siruhusu usasa wa watu kuwa karibu, wengine hadi kukumbatiana na kuhagiana wakijifanya ni utani wa mke mdogo...

Siruhusu mtoto wangu wa kike kakua na kavunja ungo kuwa karibu na babake kila saa pamoja ya kukumbatiana or uzungu zungu wa kwenda kuogelea pamoja na vitu vyote ambavyo vinawanya wawe private katika mazingira yanayo hamasisha ngono. Si kwamba naona kua babake anaweza kufanya hivyo na ni malaya - ila kwa sababu najua babake mwisho wa siku ni mwanaume ambaye anaweza kufanya hivyo.

Mimi kuto endekeza baadhi ya hayo nilotaja above ni moja ya namna ya kudhibiti. Na kwa mtazamo wangu naona kuwa ni muhimu kudhibiti. Narudia iwe within reason, isiwe udhibiti wa kero.

Anyway ni mtazamo tofauti. Ila ninachokiona kwako unamprotect mumeo kuliko wengine, kwanini nasema hivyo. Umetolea mfano wa mdogo wako na shoga zako ni wadada wamekuwa na hofu yako wanaweza mseduce mumeo (mwanaume as you said). Bado umezungumzia bintiyo, AKISHAVUNJA UNGO,.maana yake amekuwa msichana ana hisia na hivyo uwezo wa kumseduce baba yake (mwanaume) again baba hapa ni victim. Lakini umesahau hao wanaume wanabaka vitoto vidogo ambao hawajavunja ungo. So kwa ushauri wangu, katika kumthibiti mthibiti yeye mumeo maana 70% ya tatizo laanzia kwake, swala ni jinsi gani utamthibiti, unajua wewe zaidi yangu.
 
nimekulewa dadaangu na kama ulivyosema watu tunatofautiana wapo wanaopenda kudhibitwa na wasiopenda kudhibitiwa ila sasa dada Fixed Point we mume hata ukirudi saa nne labda kwa siku hiyo hata hakuulizi?au laba siku hiyo umeongea na work mate wako wa kiume hata nusu saa ye haaaa?
tumetofautiana aisee....
yaani mimi ukionyesha kunidhibiti kwa kiasi naona huniamini, na siwezi kuendelea kuwa na mtu asiyeniamini.
Nashukuru mume wangu kaniacha free mno, yaani kupita maelezo, ananiamini sana. na huwezi amini sijawahi kupoteza uaminifu wangu kwake (sijui wake kwangu.....?)
 
Last edited by a moderator:
Umeona eeh, lengo la kuchunguza lilikuwa nini? Ujue, eh ukishajua? Umbadilishe? How? Can you real change him? Au umuache? Can you? Vipi kuhusu watoto, miradi?

bado nipo mpaka leo hii, na wazo la kumuacha halikuwepo, ila nilitaka kujua ili nilitibue tu halafu yeye aamue iweje, unaona hapo? sio mie niamue, ni yeye aamue, nilipania kuliharibu siku hiyo sasa ningefanikiwa sijui kama angewezana na hiyo aibu niliyokuwa nimepania kuifanya, ningefanikiwa kuifanya ningesikilizia maamuzi yake baada ya kumtia aibu, kwanini nilikuwa nataka kufanya vurugu/kumtia aibu? sijui mana nilichoshwa kabisaaa na nimeshamjua huyo mwanamke anaezurura nae kila mabaa mjini, nina kila michongo/mitoko yao, mpaka hotel waliyokuwa wanaenda kulala, mwisho wa siku sasa hivi sitaki mtu wa kuja kuniambia ohh msukuma hivi na vile oohh yupo sijui na Kaunga, sijui nani, ntakutimua, sitaki ile presha/maumivu na nahisi sasa ndoa imetulia so sitaki kuliamsha, afanye yake, nitulie na yangu, mana hata ukija kuniambia kwasasa, kuondoka sitaondoka sana sana utanitubua tu.
 
Wakati mwingine hapa huwa ndo panaleta hatari zaidi..
Unaweza kufikiri unajenga kumbe unabomoa..
Fikiria mkeo kakuambia niko nyumbani...mara hebu mpe mwanangu simu niongee naye!
Tayari vitu kama hvi vinaanza kumuonyesha kuwa humuamini..
Na akishajua kuwa humuamini anakosa 'confidence'..

kwa baadhi ya watu inawezekana ikawa hivyo ila kwahiyo unataka kusema ukiomba kuongea na mtoto wako (mimi nasema wenu) kwanini asiichukulie kimtazamo chanya kuliko kuchukulia unamchunga...........

halafu kwanini akose confidence na asichukulie kama changamoto kuwa unamlinda kwa manufaa ya ndoa yenu.........

mkuu kumbuka uhuru unamipaka yake , na ukicheza na nyani utavuna mabua,,,,,,,,,,,,,, huwezi kumuacha tu mpenzi wako kama vile free object tu isiyokuwa na ulinzi wowote , Risk ni kubwa kuliko faida.
 
mie nilijaribu hilo but madhara yake ni maumivu matupu, nilichunga/chunguza mpaka nikafumania, nikaumia sana, nimeacha kuchucga/chunguza kajituliza mwenyewe, sujui kwanini nilichungaga nikajiumiza vile.

Umeona eeh, lengo la kuchunguza lilikuwa nini? Ujue, eh ukishajua? Umbadilishe? How? Can you real change him? Au umuache? Can you? Vipi kuhusu watoto, miradi?

Nilitoa tahadhari katika moja ya Post. Kua tatizo neno kudhibiti linachukuliwa ama kutumika vibaya. Ya kudhibitiana hadi kutaka kufuatiliana simu, kila mara kujua mwenzio yuko wapi, na the like; unaishia kwenye maumivu.

Kudhibiti kwapaswa mtu ajue wapi mpaka wake. Suala la kukagua kagua simu kila mara ni kujitafutia tu matatizo.
 
nimekulewa dadaangu na kama ulivyosema watu tunatofautiana wapo wanaopenda kudhibitwa na wasiopenda kudhibitiwa ila sasa dada Fixed Point we mume hata ukirudi saa nne labda kwa siku hiyo hata hakuulizi?au laba siku hiyo umeongea na work mate wako wa kiume hata nusu saa ye haaaa?
mimi ni mke, na ninajua kuwa ni mke wa mtu....
hata nilipokuwa kwa wazazi sikuwahi kurudi saa 8 usiku bila kuwaambia wazazi wangu kuwa naenda wapi na nitachelewa kurudi. nyumbani kwangu napenda (mimi pia nafanya hivyo) ninapoona nitachelewa kurudi nyumbani hata kama kwa nusu saa, huwa natoa taarifa kuwa nitachelewa kurudi. huwa nafanya hivi hata kwa msichana wa kazi. ikitokea mume kasafiri na nitachelewa kurudi huwa nampigia dada wa kazi kumwambia kuwa nitachelewa kurudi nyumbani.
huwa napenda kutoa taarifa siyo sababu nisifikiriwe vibaya, ila sababu mtu asiwe na wasiwasi kuwa nipo salama au la. mimi ni binadamu, chochote kinaweza nipata. mtu ajue kuwa nipo salama ila nimechelewa tu kurudi.
mdogo wangu, asilimia kubwa sana ya rafiki zangu ni wakaka, nje na ofisini. kwa hiyo huwa anajua kabisa nawasiliana/kutoka zaidi na wakaka kuliko wadada, na yupo sawa tu kwa hilo.
 
kumchunga siyo kumsidia mtu, ni kumlazimisha.
kumsaidia ni kuongea naye kuhusu mema na mabaya bila kutafuta kuwa anafanya au la

mimi naamini kumuweka mtu mbali na hivyo vishawishi ni kumsaidia kuvishinda na kumlinda dhidi ya hivyo vishawishi..........

hata mtoto mdogo haitoshi kumuambia huu ni umeme unaumiza halafu ukaachia hapo bila kuchukua hatua zaidi ya kumuweka mbali na huo umeme...........

vishawishi vipo na hata viliwashinda baadhi ya mitume wakasaliti ,sembuse sisi wanadamu wa kizazi hiki..........?

ni mara ngapi mtu anafanya jambo halafu anajutia?.......... kwanini majuto?

kwahiyo tusisubiri mtu akafanya jambo la majuto ,bali tumlinde na kujaribu kumzuia yasitokee hayo...........
 
Nilitoa tahadhari katika moja ya Post. Kua tatizo neno kudhibiti linachukuliwa ama kutumika vibaya. Ya kudhibitiana hadi kutaka kufuatiliana simu, kila mara kujua mwenzio yuko wapi, na the like; unaishia kwenye maumivu.

Kudhibiti kwapaswa mtu ajue wapi mpaka wake. Suala la kukagua kagua simu kila mara ni kujitafutia tu matatizo.

Nafikiri mleta mada alidefine kuthibiti ikiwa ni pamoja na kuchunguza simu na kuweka tego iwe fumanizi au kunasana.
 
ha haaaa, pole sana my dear.
rafiki yangu Kaunga kasema vizuri sana, unachunga ili iweje? kama unauhakika ukifumania utamuacha then endelea kuchunga, otherwise hakuna sababu ya kufanya hivyo.....
habari huwa zinakuja, hata kama huchungi. kama mtu wako anafanya mambo ya ovyo, hata baada ya miaka kadhaa, utapata taarifa, hakuna haja ya kujipotezea muda kumchunga mtu mzima mpaka unajisababishia maumivu

ni juzi kati tu hapa mke wa rafiki yake msukuma amenitafuta kuniuliza nimemfanyaje mbona siku hizi msukuma katulia kwake ndio kumekucha sasa, nimsaidie, nikamwambia sina hata nililomfanya, yeye akinywa bia kule mie nakunywa ballantin huku, najiwahia nyumbani natulia na wanangu, sina habari nae na sitakuwa tena na habari nae, ajiheshimu/ajitunze!
 
.Nilitolea mfano..kwa sababu huwa inatokea wenzi wanakuwa tayari wako kwenye udhibiti..
Hujawahi kusikia kwamba..'kama uko sehemu flani basi nipe flani niongee naye'?
Na nimeongelea udhibiti wa wazi ambapo mlengwa anajua kabisa anachungwa..
Sikatai kuwa na 'doubts' na mwenzio..lakini je umejiridhisha vya kutosha?
Na kama umejiridhisha uko tayari kwa maamuzi magumu in case...

kwa baadhi ya watu inawezekana ikawa hivyo ila kwahiyo unataka kusema ukiomba kuongea na mtoto wako (mimi nasema wenu) kwanini asiichukulie kimtazamo chanya kuliko kuchukulia unamchunga...........

halafu kwanini akose confidence na asichukulie kama changamoto kuwa unamlinda kwa manufaa ya ndoa yenu.........

mkuu kumbuka uhuru unamipaka yake , na ukicheza na nyani utavuna mabua,,,,,,,,,,,,,, huwezi kumuacha tu mpenzi wako kama vile free object tu isiyokuwa na ulinzi wowote , Risk ni kubwa kuliko faida.
 
Kuna mipaka ya vitu. Siwezi mjudge huyo mama sababu sina all the details, ila mwisho wa siku alikua ni mdhaifu mno kwa mumewe. Mwanaume afanye makosa kama hayo mara moja, usamehe na isitokee tena! Anapofanya kwa kurudia tena kwa makusudi kabisa ndani mwako mwenyewe, anakutafuta ubaya... Believe me you.

Sasa hapo kwa huyo mama FP huoni kuwa kulikuwa ni muhimu kufanya udhibiti? So in this case unaona ni sawa tu mwanamke kumwachia mumewe kufanya maamuzi na hali anajua tabia yake fika?

Pengine alikua hadhibiti, ndio maana mume alikua na uwezo wa kulala na binti zake wa kazi. Ingawa naona ni disclaim kuwa kudhibiti haimaanishi hatafanikiwa lengo, ila unalipunguza makali.

Likija suala la kua mbali na mwenza, huwezi kwenda nae FP. Ila unapo ondoka unaenda kwenye kisomo unajua kabisa unakaa mwaka, huna haja ya kuacha mdogo wako wa kike au house gal ndani ya nyumba else by the time unarudi atakua tayari ni mke mwenzako. So hapo unadhibiti pale nyumbani, akitoka nje huko you can't help it, yale yaliyo ndani ya uwezo do it.
haya mambo ni magumu sana my dear....
huyo mama alikuwa anamdhibiti mumewe kwa kufanya kazi zote zinazomuhusu mumuwe bila kumwachia hg, afanye nini tena zaidi ya hapo?
bahati mbaya sana kuna wababa huwezi watenganisha na watoto wao, mmoja wapo ni mume wangu. yaani fanya ufanyalo atataka kuwa na watoto wake muda wote. sasa inapotokea naenda shule lazima niache watoto na baba yao.... nawaachaje bila msichana wa kazi?
 
Anyway ni mtazamo tofauti. Ila ninachokiona kwako unamprotect mumeo kuliko wengine, kwanini nasema hivyo. Umetolea mfano wa mdogo wako na shoga zako ni wadada wamekuwa na hofu yako wanaweza mseduce mumeo (mwanaume as you said). Bado umezungumzia bintiyo, AKISHAVUNJA UNGO,.maana yake amekuwa msichana ana hisia na hivyo uwezo wa kumseduce baba yake (mwanaume) again baba hapa ni victim. Lakini umesahau hao wanaume wanabaka vitoto vidogo ambao hawajavunja ungo. So kwa ushauri wangu, katika kumthibiti mthibiti yeye mumeo maana 70% ya tatizo laanzia kwake, swala ni jinsi gani utamthibiti, unajua wewe zaidi yangu.

Kaunga, naona umeelewa ila umenielewa vibaya. bahati mbaya ama nzuri ni kua hapa tunazungumzia mtu wako. Ila the way I respond to mahusiano kati ya mume na wadogo na wanangu its the same way kwa Kaka yangu na wadogo ama mtoto wangu. Mwanaume kwa ku seduce yupo imara saana, mtoto wa kike yoyote at a young age yupo vulnerable. So inapotokea binti mdogo kalalwa, nachukulia kwa kiasi kikubwa mwanaume ndiye sababu kubwa.

In general, mdogo wangu wa kike or mtoto wangu, nawasihi sana kuepuka kuendekeza ukaribu na mazoea ya kupitiliza mno na mwanaume wa aina yoyote iwe baba, kaka, mjomba or whoever. Else yupo interested and she entertains the idea urafiki kuweza enda beyond na ulipo.

Niongezee hili; I don't believe katika kumchunga mtu hasa mwanaume. Ni pressure za buree... BUT hata siku moja mie sitamwekea mazingira ya yeye kufanya kitu kwa wepesi. (Refer to baadhi ya mifano nimetoa)
 
Wakati mwingine hapa huwa ndo panaleta hatari zaidi..
Unaweza kufikiri unajenga kumbe unabomoa..
Fikiria mkeo kakuambia niko nyumbani...mara hebu mpe mwanangu simu niongee naye!
Tayari vitu kama hvi vinaanza kumuonyesha kuwa humuamini..
Na akishajua kuwa humuamini anakosa 'confidence'..
hapo nilipobold SnowBall ndipo wengi wanapoharibu hiyo tunaita ni kutomwamini yule uliyenaye na ni udhibiti uliopita kiasi ambao haufai na unaweza kumpelekea mtu kufanya kweli,lakini udhibiti ninaouunga mono hapa ni ule aliojaribu kuudadavua vizuri sana pale dada AshaDii,wanadamu hatujakamilika na kwa hiyo huenda kuna wakati unaweza anza lega lega na hivyo kuhitaji kikumbusho na hapo ndipo ule udhibiti wa kiasi unapokuwa unahitajika.
 
Last edited by a moderator:
….kaka,

Mpaka pale Roho itapojiridhisha kwamba pana imani, amani na utulivu wa roho, ndipo
wengi wetu tunapojiona tunapendwa. Kinyume na hapo, ni mwendo wa Woga, Mashaka na maswali
tele ufanye nini mwenzio aamini Unampenda na yeye anakupenda.

Mapenzi ni kujithaminisha, kujikinaisha na kujiaminisha.
Utapoyamudu haya matatu, hisia za kuibiwa hazitakusumbua saaana.




Wanabodi natumaini nyote hamjambo!

Kwa muda mrefu stori nyingi zinazohusu mapenzi zimegubikwa na migogoro mingi inayotokana na wapenzi husika kuhisiana kukosa uaminifu baina yao. Kwa kuhisi kuwa wanaweza kuibiwa, wapenzi wengi wamekuwa wanawekeana 'njia' nyingi za kudhibitiana. Tumesikia 'stori' za kuwekeana 'tego' baina ya wapendanao..ili kwamba kama mmoja atatoka 'nje' basi anasie. Lakini sio hivyo tu..tunashuhudia pia wapenzi/wanandoa 'wanakagua' simu na pochi za wenza wao kwa nia ya kuhakikisha 'haibiwi mtu'. Kuna cases za baadhi ya wenza kuwafuata wenzi wao kwenye sehemu zao za kazi kwa nia ya kuji'expose' ili wajulikane. Kuna wenzi ambao wamepeana hadi 'password' za accounts zao za kwenye mitandao ya kijamii. Alimradi kinafanyika kila kiwezekanacho kuhakikisha 'udhibiti' upo.

Binafsi naamini 'binadamu hachungwi' na kwamba ukishaanza kumdhibiti au kumchunga mwenzio ni wazi kuwa wewe ni muoga wa mapenzi. Kama anakupenda anakupenda tu na kama anakuzuga atajulikana tu...Kuku wako mwenyewe manati la nini??...Lakini kuna wanaosema 'abiria chunga mzigo' hawa wanasema binadamu ni kiumbe asiyetabirika ..hivyo kufuatilia nyendo zake inasaidia 'kumstua' na kumrudisha kwenye mstari.

Hivi jamani kweli kuchungana na kudhibitiana ndio kuonyesha kuwa una mapenzi ya dhati kwa mwenzio?? au ni woga tu na kutojiamini!!!

Wasalaam!
 
Nilitoa tahadhari katika moja ya Post. Kua tatizo neno kudhibiti linachukuliwa ama kutumika vibaya. Ya kudhibitiana hadi kutaka kufuatiliana simu, kila mara kujua mwenzio yuko wapi, na the like; unaishia kwenye maumivu.

Kudhibiti kwapaswa mtu ajue wapi mpaka wake. Suala la kukagua kagua simu kila mara ni kujitafutia tu matatizo.

lakini ilinipa fundisho/ujasiri/kujiamini sana, sasa hivi mpaka mwenyewe anashangaa kwanza ndio ana wasiwasi na mie balaa,ameshangaa yule mcharuko wake amekuwaje siku hizi, anahisi yasiyopo na matisho juu.
 
mimi naamini kumuweka mtu mbali na hivyo vishawishi ni kumsaidia kuvishinda na kumlinda dhidi ya hivyo vishawishi..........

hata mtoto mdogo haitoshi kumuambia huu ni umeme unaumiza halafu ukaachia hapo bila kuchukua hatua zaidi ya kumuweka mbali na huo umeme...........

vishawishi vipo na hata viliwashinda baadhi ya mitume wakasaliti ,sembuse sisi wanadamu wa kizazi hiki..........?

ni mara ngapi mtu anafanya jambo halafu anajutia?.......... kwanini majuto?

kwahiyo tusisubiri mtu akafanya jambo la majuto ,bali tumlinde na kujaribu kumzuia yasitokee hayo...........
kweli kabisa unaamini ukiwa unapekua simu ya mpenzio ataacha kukusaliti? kweli kabisa?
umeshawahi kuwasikia watoto wakikatazana kufanya kitu fulani sababu mama kakataza?
mara nyingi napendaga sana kufanyia kazi zangu nyumbani, huwa najifungia chumbani kwangu kiasi kwamba watoto hawajui kama nipo ndani. utasikia tu huko nje wanaonyana "wewe usishike hapo mama anasema utanaswa", natabasamu tu kuona somo limeingia
 
Okay..kwa hiyo unachosema ni 'scale' ya udhibiti kupishana..ryte?
Lakini tukatae tukubali kwenye aina yeyote ya udhibiti woga na kutojiamini kunakuwa kukubwa kuliko hata mapenzi yenyewe..hivi kama najitambua mkewangu anashindwaje kuniamini hata ninapokuwa na wadogo zake?
Ni kwa vipi nisiamini tu kuwa mkewangu yupo jf kwa nia njema
Kwa nini nihangaike na mi'passwords'?...lazima kuna sehemu lipo tatizo
Aidha ni woga ulonijaa/wivu ulopevuka au mwenzangu ni kicheche..

hapo nilipobold SnowBall ndipo wengi wanapoharibu hiyo tunaita ni kutomwamini yule uliyenaye na ni udhibiti uliopita kiasi ambao haufai na unaweza kumpelekea mtu kufanya kweli,lakini udhibiti ninaouunga mono hapa ni ule aliojaribu kuudadavua vizuri sana pale dada AshaDii,wanadamu hatujakamilika na kwa hiyo huenda kuna wakati unaweza anza lega lega na hivyo kuhitaji kikumbusho na hapo ndipo ule udhibiti wa kiasi unapokuwa unahitajika.
 
Back
Top Bottom