Kumekucha DSTV, Mkurugenzi wa vipindi Maisha Magic Bongo na msaidizi wake wasimamishwa kwa rushwa!

Kumekucha DSTV, Mkurugenzi wa vipindi Maisha Magic Bongo na msaidizi wake wasimamishwa kwa rushwa!

Mpali ilikuwa ya moto pale mwanzoni bwana.

Alipozidi kuongeza wanawake hadi wazungu ikapoteza ladha.
Bora hata hao wameongeza wanawake,mi huba ndo sielewi mwelekeo wake kila siku watu wanaanzisha mapenzi hovyohovyo sijui maudhui yake ni yapi yaani hata direction haieleweki kila siku watu wanapendana

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
 
Watu hawajui tu, hayo maigizo yamewashika watu sana.

Mimi nilikuwa nayadharau hadi nilipochangamana na watu ndio nikajua.
Watu wanachukulia poa..
Mm mwenyewe nilipoanza kufatilia nikatekwa.
Yaani heri mtu asile nyama ila aweke kifurushi 🤣🤣
Mabeki tatu ndo wadau namba Moja 🙌

Zile za kikorea na zingine zilizotafsiriwa sitaki kabisa kufatilia maana zimewashika watu balaa.

Zangu bongo movies tu,, so far tumepiga hatua watz.
 
This is exclusive!

Mkurugenzi wa vipindi wa kitengo cha tamthilia za kiswahili zinazoruka kupitia kisimbuzi cha DSTV mwanamama Mtanzania Barbara Kambogi sambamba na msaidizi wake bwana Onesmus Ndarite yeye akiwa ni Mkenya wamesimamishwa kazi kwa tuhuma nzito za rushwa.

Mwanamama huyo na msaidizi wake walijijengea mfumo wao mahususi wa kuwezesha kuruka kwa sinema hizo za Kiswahili ndani ya kitengo hicho.

Mfumo huo ukiwa ni upigaji kwa pande zote, kwa madairekta kutakiwa kutoa hongo tamthilia zao zipate nafasi ndani ya DSTV, na huku haohao madairekta watakachopokea kutoka DSTV walitakiwa kugawana fungu na Mkurugenzi huyo na msaidizi wake.

Hali hiyo ilidumu kwa kipindi kirefu, ikapelekea hadi wakawa sehemu ndani ya tamthilia za Jua Kali pamoja na Huba.
Ndio maana tamthilia hizo zinaikaribia Isidingo kwa ukaribu kwa mlolongo wa vipindi vyake visivyoisha!

Wazalishaji wa tamthilia hizo maarufu wanaofahamika ni mwanamama aliyejizolea sifa kubwa Leah Mwendamseke (Lamata) na Aziz Mohamed, ila nyuma ya pazia walikuwepo Mkurugenzi na msaidizi wake.

Ubadhirifu huo wa madaraka katika kitengo hicho uliingia sura mpya baada ya ingizo jipya la tamthilia ya Chanda.
Mkurugenzi kama ilivyo ada alitaka fungu liwekwe kama ulivyo utaratibu, mtayarishaji wa tamthilia hiyo bwana Isike Samweli alikataa kutoa ‘ushirikiano’
Ndipo balaa lilipozuka!

Mtayarishaji huyo (Isike Samweli) hapo awali alitayarisha tamthilia ya Pazia, na alitoa ushirikiano hadi alipokataa kwenye tamthilia yake mpya ya Chanda.
Alipokataa akaundiwa zengwe la kukatishwa kwa tamthilia yake hiyo ambayo bado ilikuwa inaendelea…

Bwana Isike hakukubalina na hilo, na kwa kuwa walikuwa na ‘ushirikiano’ hapo awali kwenye tamthilia ya Pazia alitunza ushahidi wote wa ushirikiano aliowahi kuwapa Mkurugenzi huyo na msaidizi wake.

Bwana Isike alienda mbali zaidi kwa kumwaga ugali baada ya Mkurugenzi kutishia kumwaga mboga yake.
Alituma email kwenda makao makuu Afrika ya Kusini akiambatanisha na ushahidi wote wa miamala ya ‘ushirikiano’ aliowahi kuutoa.

Baada ya tuhuma hizo nzito zenye ushahidi kufika makao makuu, ndipo Mkurugenzi huyo na msaidizi wake waliposimamishwa kazi kwa haraka kupisha utaratibu mwingine kufanyika wa kushuhulikia hilo.

Pichani ni mwanamama Barbara Kambogi, na mtayarishaji aliyeundiwa zengwe bwana Isike Samweli.

Nikiripoti kutokea hapa JF kupitia chanzo changu makini,

Nifah.

View attachment 2825510View attachment 2825511
Tz taifa la hongo!

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
 
Nimeshapoa.

Huo ubuyu wa moto ni next weekend, wala usijali kabati langu halikaukiwi ubuyu.

Tutakuwa na holidays nzuri, tuombe uzima na kukiombea chanzo changu pia.
Mtafanya na sisi Wazee tuhamie mitaa ya Watu maarufu(Celebrates forum) ili kuja kusoma huo Ubuyu.

Fanya hivyo ili kumuenzi mdau pamoja na kulipa uhai Jukwaa la Macelebrates maana tangu atutoke Warumi Jukwaa bado halijapata mrithi wake japo baadhi wanajaribu lakini inaonekana viatu vyake vimekosa mtu sahihi.
 
Wizi ni tabia za kiume?. Mbona siku hizi kuna wamama wezi wengi tu.
Nimemshangaa sana huyo member kwa kuihusishanisha tabia ya wizi na uanaume, huyo inaonekana ni mtu aliyelelewa kwa kuaminishwa kwamba wanawake siku zote ni innocent na waaminifu na hawana kabisa kasumba za udokozi wala ujambazi, na ndio maana ameonesha kushangazwa na hii habari.

Yaani jamaa ameshindwa kabisa hata kuangalia mifano ya akina Tibaijuka,Hawa Gasia,Angelina na mama Fulani nimemsahau jina alikuwa mkurugenzi wa MSD enzi za awamu ya nne hili aondokane na hiyo Imani aliyonayo na kutambua kwamba hata wanawake pia ni majizi vile vile na Tena ni majizi haswa wakiamua.
 
Kupiga pesa mimi huwa napiga in situations ambapo naempiga anakuwa hafahamu chochote.

Ila ile kutengeneza mazingira kwamba mpigwaji ajue kabisa kwamba nampiga ishu za hivyo huwa sifanyi. Zile style kama za kiafande kwamba niungie tukamilishe jambo hizo huwa sifanyagi.

Ila unataka mzigo flani na najua unapopatikana hapo lazma nikuongezee sifuri mbele kisha ukituma hela najilipa juu kwa juu.[/color=red] Au kwenye supplies ya bidhaa huwa tunafanya sana michezo sisi watu wa sales.

Hapo kwa maafande Huwa pananiumiza sana, hivi kwanini askari wabongo kutimiza wajibu wake mpaka umfurahishe kwa kumpa hongo kidogo? Kiukweli hakuna askari aliyewahi kunisaidia pasipo kumrefushia mkono!

Sasa huko kunaitwa kujiongeza na Wala sio upigaji huo maana mtoaji wa hela kaitoa bila manung'uniko ya aina yoyote[/red]
Kupiga pesa isivyo halali kwa namna yeyote ile ni kubaya.
Mbongo anakwambia pesa ni pesa haijalishi umeipata vipi maana hakuna sehemu utakayoenda kuitumia wataikataa kisa umeipata kwa njia isiyokuwa ya halali.
 
Bora hata hao wameongeza wanawake,mi huba ndo sielewi mwelekeo wake kila siku watu wanaanzisha mapenzi hovyohovyo sijui maudhui yake ni yapi yaani hata direction haieleweki kila siku watu wanapendana

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
Nafikiri sababu umeijua leo sasa, huenda baada ya hili sakata hizo tamthilia zitaisha.
 
Mtafanya na sisi Wazee tuhamie mitaa ya Watu maarufu(Celebrates forum) ili kuja kusoma huo Ubuyu.

Fanya hivyo ili kumuenzi mdau pamoja na kulipa uhai Jukwaa la Macelebrates maana tangu atutoke Warumi Jukwaa bado halijapata mrithi wake japo baadhi wanajaribu lakini inaonekana viatu vyake vimekosa mtu sahihi.
Shaka ondoa, pele limepata mkunaji.

Tuombe uzima tu, tutakuwa na wakati mzuri.
 
Back
Top Bottom