Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Uvaaji wa suruali yake tu unatia mashakaThis is exclusive!
Mkurugenzi wa vipindi wa kitengo cha tamthilia za kiswahili zinazoruka kupitia kisimbuzi cha DSTV mwanamama Mtanzania Barbara Kambogi sambamba na msaidizi wake bwana Onesmus Ndarite yeye akiwa ni Mkenya wamesimamishwa kazi kwa tuhuma nzito za rushwa.
Mwanamama huyo na msaidizi wake walijijengea mfumo wao mahususi wa kuwezesha kuruka kwa sinema hizo za Kiswahili ndani ya kitengo hicho.
Mfumo huo ukiwa ni upigaji kwa pande zote, kwa madairekta kutakiwa kutoa hongo tamthilia zao zipate nafasi ndani ya DSTV, na huku haohao madairekta watakachopokea kutoka DSTV walitakiwa kugawana fungu na Mkurugenzi huyo na msaidizi wake.
Hali hiyo ilidumu kwa kipindi kirefu, ikapelekea hadi wakawa sehemu ndani ya tamthilia za Jua Kali pamoja na Huba.
Ndio maana tamthilia hizo zinaikaribia Isidingo kwa ukaribu kwa mlolongo wa vipindi vyake visivyoisha!
Wazalishaji wa tamthilia hizo maarufu wanaofahamika ni mwanamama aliyejizolea sifa kubwa Leah Mwendamseke (Lamata) na Aziz Mohamed, ila nyuma ya pazia walikuwepo Mkurugenzi na msaidizi wake.
Ubadhirifu huo wa madaraka katika kitengo hicho uliingia sura mpya baada ya ingizo jipya la tamthilia ya Chanda.
Mkurugenzi kama ilivyo ada alitaka fungu liwekwe kama ulivyo utaratibu, mtayarishaji wa tamthilia hiyo bwana Isike Samweli alikataa kutoa ‘ushirikiano’
Ndipo balaa lilipozuka!
Mtayarishaji huyo (Isike Samweli) hapo awali alitayarisha tamthilia ya Pazia, na alitoa ushirikiano hadi alipokataa kwenye tamthilia yake mpya ya Chanda.
Alipokataa akaundiwa zengwe la kukatishwa kwa tamthilia yake hiyo ambayo bado ilikuwa inaendelea…
Bwana Isike hakukubalina na hilo, na kwakuwa walikuwa na ‘ushirikiano’ hapo kabla kwenye tamthilia ya Pazia alitunza ushahidi wote wa ushirikiano aliowapa Mkurugenzi huyo na msaidizi wake.
Bwana Isike alienda mbali zaidi kwa kumwaga ugali baada ya Mkurugenzi kutishia kumwaga mboga yake.
Alituma email kwenda makao makuu Afrika ya Kusini akiambatanisha na ushahidi wote wa miamala ya ‘ushirikiano’ aliowahi kuutoa.
Baada ya tuhuma hizo nzito zenye ushahidi kufika makao makuu, ndipo Mkurugenzi huyo na msaidizi wake waliposimamishwa kazi kwa haraka kupisha utaratibu mwingine kufanyika wa kushuhulikia hilo.
Pichani ni mwanamama Barbara Kambogi, na mtayarishaji aliyeundiwa zengwe bwana Isike Samweli.
Nikiripoti kutokea hapa JF kupitia chanzo changu makini,
Nifah.
View attachment 2825510View attachment 2825511
Unanikumbusha kigogo mmoja ikifika saa ya HUBA kurushwa usimpigie simu, hadi ratiba ya Huba niliikariri kwa ajili yake😂😂Kumbe kuna watu wanaangaliaga hivyo
Vipindi
Ova
Akawa mbishi kama mjomba wake Kiyungi.Isike aligoma kuendeleza ushirikiano wa jumuia 🤣🤣
Kadri mshahara unavyokuwa mkubwa, ndio kadri ambavyo dau lake la rushwa linavyokuwa kubwa.Unazungumzia wa mkurugenzi wa DSTVmkuu?huyo ana nini hadi uone hawezi kula rushwa?
Zungumzia wa waziri fulani serikalini huku mshahara ukiambatana na allowance chungu mbovu lakini bado huwa wanakunja noti,ukiona mikataba mibovu tunayoingizwa na hao viongozi usidhani ule ni utashi wao kuna kitu behind.
Na ndipo unapaswa kutumia akili na maarifa ili usiharibu vyote.Hii mbona ipo kila mahali ?, Hata ngazi a Nchi hizi ni zile zinaitwa 10%, Unadhani Msemo wa Mkono Mtupu Haulambwi walimaanisha nini ?
Akili na maarifa ni kwamba mtu hachukui mlungula moja kwa moja anamtumia mdau wa mdau wa mdau wa mdau..., kuja kufanya connection kunakuwa na plausible deniabilityNa ndipo unapaswa kutumia akili na maarifa ili usiharibu vyote.
Kwahiyo ndio tuhalalishe rushwa kila mahali?Unazungumzia wa mkurugenzi wa DSTVmkuu?huyo ana nini hadi uone hawezi kula rushwa?
Zungumzia wa waziri fulani serikalini huku mshahara ukiambatana na allowance chungu mbovu lakini bado huwa wanakunja noti,ukiona mikataba mibovu tunayoingizwa na hao viongozi usidhani ule ni utashi wao kuna kitu behind.