Kumekucha DSTV, Mkurugenzi wa vipindi Maisha Magic Bongo na msaidizi wake wasimamishwa kwa rushwa!

Kumekucha DSTV, Mkurugenzi wa vipindi Maisha Magic Bongo na msaidizi wake wasimamishwa kwa rushwa!

Ila Nchi za Afrika na Rushwa ni kama Pete na Kidole

Kama hadi Yuda Eskariote alikula rushwa ya vipande 30 ili kumsaliti Masihi ndiyo iwe kwa huyo Bibie?

Ila nimependa ulivyomaliza habari yako
"Nikiripoti kutokea hapa JF kupitia chanzo changu makini"........

Utasema warumi 🫡
Usinikumbushe binamu yangu, R.I.P

Ipo siku nitaweka thread ya ubuyu kumuenzi!
 
Bora juakali ilianza kwa setting nzuri na mastar wengi sana kiasi ilikuwa huwezi kuimiss.
Ila hii huba niliikuta watu wanaangalia na sikuelewa wanaangalia nini maana story line sikuielewa na hata uigizaji wenyewe

Labda Nicole joeberry anawahamasisha maana ana fans wa kutosha
Huba ilikuwa na kick kubwa sababu ya Wema kuwepo msimu wa kwanza kama sikosei.
 
Shem, kitu wizi ndio nimeshindwa maishani!

Nimelelewa vyema, udokozi ulinipitia kando utotoni hadi hivi sasa.

Uaminifu kazini ni kila kitu, napenda amani hivyo siwezi kuipoteza kwa tamaa.

Halafu hao wanaoiba sijui hela wanapelekaga wapi masikini! Sijigambi ila nina maisha bora kuwazidi!
Nafikiri ni vile Mungu anabariki kidogo changu cha halali.
Tunatofautiana.

Binafsi cha mtu siibi ila kwenye makampuni nabeba ilimradi nakuwa smart
 
Shem, kitu wizi ndio nimeshindwa maishani!

Nimelelewa vyema, udokozi ulinipitia kando utotoni hadi hivi sasa.

Uaminifu kazini ni kila kitu, napenda amani hivyo siwezi kuipoteza kwa tamaa.

Halafu hao wanaoiba sijui hela wanapelekaga wapi masikini! Sijigambi ila nina maisha bora kuwazidi!
Nafikiri ni vile Mungu anabariki kidogo changu cha halali.
Tunatofautiana.

Binafsi cha mtu siibi.
 
This is exclusive!

Mkurugenzi wa vipindi wa kitengo cha tamthilia za kiswahili zinazoruka kupitia kisimbuzi cha DSTV mwanamama Mtanzania Barbara Kambogi sambamba na msaidizi wake bwana Onesmus Ndarite yeye akiwa ni Mkenya wamesimamishwa kazi kwa tuhuma nzito za rushwa.

Mwanamama huyo na msaidizi wake walijijengea mfumo wao mahususi wa kuwezesha kuruka kwa sinema hizo za Kiswahili ndani ya kitengo hicho.

Mfumo huo ukiwa ni upigaji kwa pande zote, kwa madairekta kutakiwa kutoa hongo tamthilia zao zipate nafasi ndani ya DSTV, na huku haohao madairekta watakachopokea kutoka DSTV walitakiwa kugawana fungu na Mkurugenzi huyo na msaidizi wake.

Hali hiyo ilidumu kwa kipindi kirefu, ikapelekea hadi wakawa sehemu ndani ya tamthilia za Jua Kali pamoja na Huba.
Ndio maana tamthilia hizo zinaikaribia Isidingo kwa ukaribu kwa mlolongo wa vipindi vyake visivyoisha!

Wazalishaji wa tamthilia hizo maarufu wanaofahamika ni mwanamama aliyejizolea sifa kubwa Leah Mwendamseke (Lamata) na Aziz Mohamed, ila nyuma ya pazia walikuwepo Mkurugenzi na msaidizi wake.

Ubadhirifu huo wa madaraka katika kitengo hicho uliingia sura mpya baada ya ingizo jipya la tamthilia ya Chanda.
Mkurugenzi kama ilivyo ada alitaka fungu liwekwe kama ulivyo utaratibu, mtayarishaji wa tamthilia hiyo bwana Isike Samweli alikataa kutoa ‘ushirikiano’
Ndipo balaa lilipozuka!

Mtayarishaji huyo (Isike Samweli) hapo awali alitayarisha tamthilia ya Pazia, na alitoa ushirikiano hadi alipokataa kwenye tamthilia yake mpya ya Chanda.
Alipokataa akaundiwa zengwe la kukatishwa kwa tamthilia yake hiyo ambayo bado ilikuwa inaendelea…

Bwana Isike hakukubalina na hilo, na kwakuwa walikuwa na ‘ushirikiano’ hapo kabla kwenye tamthilia ya Pazia alitunza ushahidi wote wa ushirikiano aliowapa Mkurugenzi huyo na msaidizi wake.

Bwana Isike alienda mbali zaidi kwa kumwaga ugali baada ya Mkurugenzi kutishia kumwaga mboga yake.
Alituma email kwenda makao makuu Afrika ya Kusini akiambatanisha na ushahidi wote wa miamala ya ‘ushirikiano’ aliowahi kuutoa.

Baada ya tuhuma hizo nzito zenye ushahidi kufika makao makuu, ndipo Mkurugenzi huyo na msaidizi wake waliposimamishwa kazi kwa haraka kupisha utaratibu mwingine kufanyika wa kushuhulikia hilo.

Pichani ni mwanamama Barbara Kambogi, na mtayarishaji aliyeundiwa zengwe bwana Isike Samweli.

Nikiripoti kutokea hapa JF kupitia chanzo changu makini,

Nifah.

View attachment 2825510View attachment 2825511
Tamthilia haziishi miezi nenda,rudi

Azam Tv angalau kuna fairness
 
Back
Top Bottom