Hismastersvoice
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 21,741
- 26,735
Siri ya mtindi kuwa mzito, kwanza anza wewe kuyachunguza kwa kuyaacha yalale siku tatu, utakuta yamegawanyika maratatu chini kitu kama maziwa hiki hufanya yawe mazito, kinafuatia maji na juu kabisa maziwa ya mtindi, yanakuwa juu kwa sababu ni mepesi.Mtindi wao huwa ni mzito kweli kweli,nambari wani.
Umeweka Picha ya Punda? Ili kutishia wasio kuwa na uelewa?Kumekuwa na wimbi kubwa la vijana kuuza maziwa fresh na mtindi mitaani, Je maziwa hayo huwa ni salama kwa afya za watumiaji?
Niliwahi fanya tafiti kidogo kwa kumuuliza kijana mmoja muuzaji wa maziwa haya, aliniambia wanayanunua ubungo na hivyo wao huyauza tena mitaani kwa faida kidogo.
Je, ni maziwa ya ngombe?
Mtindi umechanganywa na unga wa ngano umeingia kingi...kweli Dar akili kijijini nguvu!Mtindi wao huwa ni mzito kweli kweli,nambari wani.
Huwa wanatia na unga wa ngano,kukoleza radhaMtindi wao huwa ni mzito kweli kweli,nambari wani.
Ina maana unga wa ngano ni bei rahisi, mpaka mnachanganya na maziwa kisha kupata faidaSiri ya mtindi kuwa mzito, kwanza anza wewe kuyachunguza kwa kuyaacha yalale siku tatu, utakuta yamegawanyika maratatu chini kitu kama maziwa hiki hufanya yawe mazito, kinafuatia maji na juu kabisa maziwa ya mtindi, yanakuwa juu kwa sababu ni mepesi.
Hiki sasa ndicho hufanyika kuyaboresha, unga wa ngano hukorogwa kwenye maji kisha huchemshwa na kuacha uji huo mwepesi upowe, ukishapoa huchanganywa na mtindi na kukorogwa muda wote, mnunuzi anaponunua huuona mtindi mzito.
Kwanini hukorogwa muda wote, jibu lipo juu.
Kwa watu wa Dsm jinsi walivyochanganyikiwa na maisha, unaweza ukauziwa hata maziwa yaliyokamuliwa kutoka katika matiti ya binadamu. Uaminifu kwa sasa umekufa kabisa.Kijana angalia usije kunyweshwa utomvu wa mapapai, Dar ni jiji kubwa hivyo usiamini kila kinachouzwa na usiowajua.
Wanaweka kiasi kidogo sana kutengeneza uji mwepesi, mbona wengine wanatengenezea gundi ya kutengeneza mifuko ya karatasi.Ina maana unga wa ngano ni bei rahisi, mpaka mnachanganya na maziwa kisha kupata faida
Hao CHAWAKIM na TREASURE nilishawahi kununua maziwa kwao kipindi nipo Dar... Top class maziwa, huwa sinunui tofauti na hapo.. mtaani " i got trust issues"Hayo ni maziwa halali ya ng'ombe pamoja na mtindi.
Hao wachuuzi wanajumua kutoka viwanda vya maziwa CHAWAKIMU na Kingine TREASURE vilichopo Kiluvya madukani vinachoendeshwa na wafugaji wa Kisarawe, Kibaha, Dar es salaam na Baadhi ya Bagamoyo.
Kama kuna uchakachuaji basi waamue kuongeza maji kidogo ili kupata faida zaidi ila hiyo kwa watu wenye tamaa.
Na mteja kama amewahi kuonja maziwa hayo yakiwa hayajachakachuliwa akionja yenye uchakacjuaji atajua tu na wateja atawapoteza.