Kumfanyisha Interview Medical Doctor aliyethibitishwa na Baraza la Madaktari (MCT) ni dharau kubwa sana

Africans value more politicians than professional,hivi huna aibu kusema kuwa madaktari ni WA kawaida kweli watu wanaoweza fanya operation mkeo akazaa salama na mtt akawa hai,
Wewe subiria ipo siku utajua value yao na hela zako hizo kiburi kitaisha
Izo operation Ata waganga wa jadi wanafanya bana sio jambo kubwa ilo
 
Kuna soft skills nyingi ambazo madaktari wana gap. For example, communication skills, team work, solving ethical dilemma, etc. Ukiwa na knowledge peke yake, with poor attitude and skills, you are an incomplete clinician!
 
Ila wa hapa bongo wanalipwa kidogo sana.
 
So fani yenu tu ndiyo inayopitia msoto ama...?
 
Interview imekuendea mlamaa leo
 
Kwaio daktari inatakiwa awe amefaulu tu ila ata kama ana tabia mbovu fresh au hana customer care, ubinadamu nk. Yeye apewe tu kazi au sio
Hivyo vyote sijui tabia, client care, humanity na vingine deep sana mpaka psychology ashavisoma na kafanya mitihani huko chuoni ya oral na written tena migumu ilioshiba, it doesn't make sense kwenda kumpima tena upya
 
Mwisho wa siku watu hawatasoma hiyo course na kufanya kitu kingine
 
Hivyo vyote sijui tabia, client care, humanity na vingine deep sana mpaka psychology ashavisoma na kafanya mitihani huko chuoni ya oral na written tena migumu ilioshiba, it doesn't make sense kwenda kumpima tena upya
Kapimwe akili
 
Nilipofika hapo kwenye "prectical" nimeelewa kwann unachukia interview
 
Interview ni muhimu kupata watu wazuri. Tunatofautiana kwenye kila laaluma.

Kwani taluuma gani hawasomi sana?Au unadhani umuhimu wako unatokana na miaka mingi kukaa Muhimbili?

Kila taaluma ina umuhimu wake, na kuwa daktari ni uamuzi wako, ungesoma Bcom au BAF pia ni maamuzi yako binafsi, hivyo usijione unamaana kuliko yeyote.

Kama wewe hutaki au huoni umuhimu wa interview, basi ikiondolewa kwa daktari iondolewe na kwa mfagizi wa ofisi.
Ni utaratibu ufuatwe na kila mtu.
 
Wanafanyiwa interview mabingwa huko Ulaya na Marekani udaktari ulipoanzia na wana maboard yanayofanya kazi sawasawa nyie vijana wa kisasa mnataka free lunch bonglendi! Kweli ujamaa ni uchafu umetuharibia sana kizazi hadi uje ufutike vichwani labda kizazi cha tano kule
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…