Kumfanyisha Interview Medical Doctor aliyethibitishwa na Baraza la Madaktari (MCT) ni dharau kubwa sana

Kumfanyisha Interview Medical Doctor aliyethibitishwa na Baraza la Madaktari (MCT) ni dharau kubwa sana

hakuna cha usenge wala nini ndiyo kawaida ufanyiwe interview ili kieleweke kama wewe uko vizuri kuliko yule mwenzako aliyeachwa.

Sasa kama muko 1000 na nafasi zilizoko ni 30 unadani mchujo utapita vipi hapo bila interview?
Mtu akishapata leseni ya udaktari tayari yuko vizuri.
 
Kaka in real world muda uliosoma si moja ya qualification, ww hata usome miaka 100, kama cheti ni kimoja ndio hiko hiko, ndio utakuwa judged nacho.

Huku mtaani time uliyosoma doesnt matter, is what ume acquire after that. No offence siwadharau but you guys are not the only one
Katika udaktari muda uliosoma ni moja ya qualification, Marekani madaktari wanasoma miaka nane ya chuo ndio maana madaktari wa Africa wakifika huko inabidi warudi tena shule pamoja na kufanyishwa mitihani mingi ili waweze kuajirika.
 
Vijana hawataki usaili wanataka kitonga.Juzi tu kuna mwalimu aliweka uzi wa kulalamika kufanyiwa usaili. Sasa nasema hivi mpende msipende mtafanyiwa usaili tu. Iwe dharau isiwe dharau mtafanyiwa usaili.pumbavu mnataka kupewa kazi bure wakati wengine wanafanyiwa usaili.
umepiga kwenye mshono😂😂😂😂
 
Kuna watu hawachuji kwa kuangalia vyeti na historia ya umwpitia wapi, wanachuja kwa kuangakia attitude ya mtu.

Usiwanyime haki yao ya kuchuja wanavyotaka.
Kama ni hivyo wangekuwa wanafanyiwa psychology tests tu, pia hii ingewafaa zaidi viongozi, wabunge, polisi, Rais n.k. Interviews kwa madaktari ni janjajanja ya kupunguza watu kwa sababu ya ufinyu wa ajira.
 
Etiii nimepataa A mara division one WTF ajira za serikali ni haki ya kila mtu regardless ufaulu wako wa huko mashulenii nendenii mkapambanee nafasii ni chachee mno😂😂 nyie ndo mnakosea kufanyia watu operation baada ya goti mnafanya kichwa kisa umepata division one four……. Nenda kwenye interview kaonyeshee kwamba wewe unauwezo kuliko wengnee sio kutupigia kelele hapaa
Kuna wajomba wana A kibao kwenye cheti ukimhoji ndio unajiuliza alitoa wapi hizi A
 
Hii mitihani ni kwa ajili ya kuweka fair ili kuepusha maneno kwamba kuna watu wanapata kazi kwa kupendelewa, Nafasi zingekua nyingi kusingekua na haja ya interview sasa watu ni wengi kuliko nafasi mfano nafisi zipo 50 halafu waombaji wapo 1000 hapo wewe utafanyaje ili iwe fair.
Wewe uko sahihi, hizo interviews kwa madaktari hazipimi chochote cha maana, ni njia ya kupunguza watu tu.
 
Daktari wa binadamu hahitaji interview ya kazi, leseni yake ya udaktari inatosha.
Uchache wa kazi ndio unasababisha interviews kuwepo, pia Daktari aliyefaulu kwa kiwango cha juu darasani kwa A nyingi ndiye Daktari bora hata kama atafeli usahili wa kupiga/kuuza maneno.
Unaongea wewe,mimi ndio mwenye hospitali,unataka nifate utakacho wewe?

Kwahiyo A ndio amri ya kutuamrisha wenye taasisi kwa lazima tukuajiri?

Una A lakini jambazi na evil,nikuajiri kwenye taasisi yangu kivipi yaani?

Mali yangu,unataka uje kuniletea ulazima eti ulipata A?

Fungua taasisi yako utafanya utakalo,who cares!
 
Sasa hivi fani nyingi zina mabaraza ya kuwathibitisha na kuwasajili.
Sasa kwa namna hiyo tuziondoe interview zote au ?
Wahasibu, Wahandisi , Wagavi, wagani n.k wana mabodi yao .
Acheni ujinga
Wahasibu, wagavi na Wagani ni kazi za social sciences/ngwini ambazo zinahusisha siasa, majungu, fitna na janjajanja za hapa na pale tofauti na kazi za pure science kama Wahandisi, madaktari, nk.
 
One may be good at answering selected number of questions, ila iki fika ku relate katika fani husika ni majanga mazito.

So acha wawa chuje, huenda Waka pata watu makini.
SI una elewa Kuna watu ni mabingwa wa kununua vyeti??.
Sio kwenye udaktari, mtu yeyote mwenye leseni ya udaktari hawezi kuwa majanga hata kidogo, anachoweza kukosa na experience kubwa tu, lakini akipata nafasi atazidi kuwa bora zaidi kadri muda unavyokwenda.
 
Kama ni hivyo wangekuwa wanafanyiwa psychology tests tu, pia hii ingewafaa zaidi viongozi, wabunge, polisi, Rais n.k. Interviews kwa madaktari ni janjajanja ya kupunguza watu kwa sababu ya ufinyu wa ajira.
Wenye kutoa kazi ndio wanaoweka vigezo.

Na wewe unaweza kuanzisha ajira zako na kuweka vigezo vyako.
 
Kuna jamaa angu anafundisha feza hata hajafanyiwa interview alichukuliwa moja kwa moja alipomaliza chuo tu maana wanakuwa na taasisi zao za kuwasimamia graduates vyuoni

Na kila ajira zikitoka huwa anaomba ili aingie serikalini. Kwahiyo sio kweli kuwa shule za kata zina vilaza na hizo feza zina magenius hapana ni utofauti wa kimazingira tu na usimamizi
Tutajie hizo taasisi za Feza zinazochukua walimu bila interview ?
 
Just imagine kijana kapata division one ya 7 au 10 form four kaenda high school kupiga PCB. Kapambana sana kachakaa kajitesa kajinyima kapata division one form six ya point tatu au tano.

Kaaply Muhimbili University kapitia mchujo katoboa akaanza masomo ya udaktari.

Kasoma miaka mitano bila kudisco tena kwa mateso makubwa bila kula bata mpaka kamaliza chuo.

Kabla hajaingia intern kafanyishwa mtihani wa MEDICAL COUNCIL OF TANGANYIKA katoboa kaanza interniship.

Kapiga intern kwa mwaka mmoja kisha kamaliza kisha kapigishwa pepa lingine la MCT katoboa.

Kasajiliwa na kutambulika kama MEDICAL DOCTOR na MCT.

Kijana huyu wa kitanzania aliyesoma kwa kujinyima na kujitesa tangu kidato cha kwanza leo hii anafanyishwa interview tena written interview sio prectical interview ili iweje?

Huyu kijana akikosa nafasi mnajua stress atakazopata mtaani na jamii inayomzunguka?

Hiyo michujo yote alopitia akipata ajira mnamlipa milioni moja na laki mbili ukitoa makato anabeba laki tisa bado mnampigisha interview ya nini sasa?

Hamuoni kama mnakatisha tamaa vijana waliopo shuleni na vyuoni?

Wadau
Hivi unaweza kuajiriwa popote bila interview? Nchi hii tuna shida sana na uwezo wa watu kufikiri.
 
Wenye kutoa kazi ndio wanaoweka vigezo.

Na wewe unaweza kuanzisha ajira zako na kuweka vigezo vyako.
Sijapinga wenye kutoa kazi ndio wanaoweka hivyo vigezo, ninachosema hivyo vigezo kwa fani ya udaktari havina mashiko,
 
Kwenye udaktari muhimu ni ufaulu na experience, mambo ya ukarimu na personality ni kazi za siasa na fani nyingine za ngwini. Kwenye science jambo muhimu ni ufaulu, wanasayansi wakubwa zaidi duniani mfano washindi wa Nobel na vumbuzi mbalimbali ni watu fulani wasio na ukarimu au personality nzuri.
Mkuu a Doctor is a Healer kuna jinsi ya kumwambia mgonjwa ili a feel good huwezi kuja unamwambia mgonjwa ana ukimwi au cancer au ana siku tatu za kuishi huku unavuta fegi na kuchekelea au unatangazia watu bar kwamba fulani ana gono....

Ngoja nikupe Qoute from Person of Interest huenda ikakuonyesha what I mean....

Sameen Shaw: I watch the others. I watch the fear creep into them. I watch them make mistakes, and you think these feelings that I'm lacking make them better? You'd really rather have one of them working on you instead of me?
QMI Manager: Yes. Because if If the only thing motivating you is technical mastery, when one of your patients needs you the most, then this job just might start to bore you. That's the difference between fixing and healing. You have a brilliant mind, Sameen. And you're very gifted. But you'll never be a doctor.
 
Sijapinga wenye kutoa kazi ndio wanaoweka hivyo vigezo, ninachosema hivyo vigezo kwa fani ya udaktari havina mashiko,
Vina mashiko kwa sababu wao ndo wanajua wanahitaj daktari wa aina gani
 
Chief, sipingi usaili ila naomba nikuswalike swali

Hivi lengo la usaili ni kuchuja idadi au ubora?

Kama ni idadi vipi mtihani wakifaulu wote watatumia kigezo gani kingine kupata hao 20 out of 200
Lengo la interviews za udaktari ni kuchuja idadi tu sio ubora, kama ni ubora wangeangalia ufaulu wa darasani, hilo ndilo jambo muhimu zaidi kwa daktari.
 
Back
Top Bottom