Kumwacha jela kifungo cha mwaka kutasaidia kutoa sumu ya ulevi wa pombe?

Kumwacha jela kifungo cha mwaka kutasaidia kutoa sumu ya ulevi wa pombe?

Ngome, Ndichi, kama unampenda ndugu yako na unaweza kumtoa usiruhusu akakkae jela sio kuzuri kabisa
 
Mkuu hakuna chenye utafanya wewe kimzuie huyo nduguyo kunywa pombe.

Siku zote mabadiliko ya aina yoyote huanzia ndani ya nafsi ya mtu mwenyewe. Bila yeye kuamua hakika nakuambia hataacha.

Unachoweza kumsaidia ni kumtafutia mtaalamu wa counseling ili azungumze nae. Wao wana mbinu nyingi za kuweza kuongea na mtu na kumshawishi aone maisha katika angle ya toauti.

Counsel ya mtaalam inaweza kuwa ndio chanzo cha inner drive ya yeye kujitafakari na kufikiri kuhusu kuacha pombe.

Kumwacha aende gerezani haitakuwa suluhu zaidi itakuwa ndio umeongeza tatizo. Gerezani sio sehemu nzuri.
 
Jela kila kitu kinapatikana mzee akiwa na sabuni za kutosha anafanya biashara ya kubadilishana tu hata ganja atanyonga ila kama hana kitu na anapenda pombe akikubali tu kuwa mke wa mtu hata ugali maharage atauskia kwa wenzake ye atakua anakula rosti tu na kazi ngumu hafanyi
Sasa kuwa makin asije kurudi akiwa bwabwa.
[emoji134][emoji134][emoji134][emoji134],Jela hakufai.
 
Utakuta pombe anazotumia ikizidi sana bei yake 2000 ambiance’s,shumwaa na balimi.

Mwambie hatumie Jack daniel !

Sijawahi kuona walevi wa pombe kuanzia 70 wanamambo ya kijinga
 
Mkuu hakuna chenye utafanya wewe kimzuie huyo nduguyo kunywa pombe.

Siku zote mabadiliko ya aina yoyote huanzia ndani ya nafsi ya mtu mwenyewe. Bila yeye kuamua hakika nakuambia hataacha.

Unachoweza kumsaidia ni kumtafutia mtaalamu wa counseling ili azungumze nae. Wao wana mbinu nyingi za kuweza kuongea na mtu na kumshawishi aone maisha katika angle ya toauti.

Counsel ya mtaalam inaweza kuwa ndio chanzo cha inner drive ya yeye kujitafakari na kufikiri kuhusu kuacha pombe.

Kumwacha aende gerezani haitakuwa suluhu zaidi itakuwa ndio umeongeza tatizo. Gerezani sio sehemu nzuri.
Kuna kijana alipokea mshahara akanywea wote pombe. Asubuhi alipoamka akasema sinywi tena pombe, ilikuwa 2018 hadi leo hajagusa pombe.

Uamuzi wa kuacha pombe, punyeto, bangi, umalaya n.k inabidi utoke ndani ya mtu mwenyewe.
 
Pia utofautishe mlevi na muhalifu. Ndugu yako ni muhalifu ndio maana kila siku anakamatwa.
 
Mwache akapumzike akirudi atakuwa kanyooka.. Mitaa ninayoishi kuna mmoja alikuwa hivyohivyo..kaswekwa mahabusu wiki tatu tuu karudi kanyooka kama rula nyumbani anaingia saa 12
Kuingia nyumbani saa 12 nalo ni tatizo kubwa zaidi
 
UPDATE: Nimepewa wazo na Mshana Jr na Daudi Mchambuzi kumuacha Polisi au mahabusu muda mrefu, Bado naendelea kupokea maoni

Kuna ndugu yangu ni mlevi sana, Mara kwa mara nimelazimika kumtoa kituo cha polisi kwa kuwapa pesa za kubrashia viatu ma afande ambao tunajuana, Matatizo hayo yanatokea kwasababu ya ulevi wake wa pombe.

Kazi anafanya za ujenzi wa nyumba, kuchoma na kuuza matofali, kufyatua matofali , n.k n.k, Ni kijana mchapa mwenye mwili wenye misuli iliyojaa na mchapa kazi ila pombe inamharibu

Sasa nimeona labda aende tu huko gerezani maana kosa lake ni la mwaka 1 na nuu hivi gerezani endapo nisipomtoa.

Kesi yake nimeshaifatilia huwa inasikilizwa haraka mahakamani na hukumu hutokewa papo hapo,

Sasa nimeona huenda akienda huko jela hio sumu ya uraibu itamtoka.

Je, nichukue huu uamuzi?
Jela za kitanzania ndugu hapana, najua inachosha sana kubeba matatizo yake lkn nakuomba usimwache aende jela.
 
UPDATE: Nimepewa wazo na Mshana Jr na Daudi Mchambuzi kumuacha Polisi au mahabusu muda mrefu, Bado naendelea kupokea maoni

Kuna ndugu yangu ni mlevi sana, Mara kwa mara nimelazimika kumtoa kituo cha polisi kwa kuwapa pesa za kubrashia viatu ma afande ambao tunajuana, Matatizo hayo yanatokea kwasababu ya ulevi wake wa pombe.

Kazi anafanya za ujenzi wa nyumba, kuchoma na kuuza matofali, kufyatua matofali , n.k n.k, Ni kijana mchapa mwenye mwili wenye misuli iliyojaa na mchapa kazi ila pombe inamharibu

Sasa nimeona labda aende tu huko gerezani maana kosa lake ni la mwaka 1 na nuu hivi gerezani endapo nisipomtoa.

Kesi yake nimeshaifatilia huwa inasikilizwa haraka mahakamani na hukumu hutokewa papo hapo,

Sasa nimeona huenda akienda huko jela hio sumu ya uraibu itamtoka.

Je, nichukue huu uamuzi?
Huyo ni kumchanganyia madawa kwenye pombe tu atapike mpaka akili inayomtuma aende bar!
 
Pombe kama ni mlevi haswa , hata akae miaka mingapi akitoka ataendelea. Labda awe willing kuacha.

Nina ushuhuda na ndugu yangu mmoja yeye alikaa miezi sita akarudi akaendeleza vyombo kama kawaida
 
Usimwache apelekwe huko mambo yatazidi kuwa mabaya zaidi
 
Talking from experience!.

Nina mdogo wangu 34 years. Nimehangaika naye sana. Ni chapombe kupitiliza.

Alikuwa mfanyakazi mzuri sana, pombe zikamlemea. Akaachishwa kazi. Akaanza kufanya biashara, jioni ikifika hela ya mauzo anaenda kunywea.

Ana mke na watoto wawili, hela anazo biashara inafanyika lakini mahitaji hawapati.

Mbaya zaidi, akilewa wala halegei. Anakuwa na nguvu balaa.

Nimehangaika naye sana. Kuna dawa nilipewa, akaacha kabisa kunywa kwa wiki tatu. Akarudia tena kwa nguvu zaidi.

Nimeamua kumpeleka Gereza la Karanga kwa miezi mitatu. Ndo kwanza ana mwezi, ila ninaumia sana yeye kuwepo huko.

Ngoja tuone akitoka hali itakuaje. Nitaleta mrejesho..
 
Huyu kashawekewa mara 2 dawa za kuacha pombe na dada yake lakini wapi? Pombe ni uraibu ambao hausikii dawa
Mjomba wangu ana hiyo dawa. Kwa ndugu huwa anawapa bure. Hakuna aliyenyweshwa hiyo dawa akaendelea kunywa pombe.
 
Back
Top Bottom