Kuna baadhi ya koo / makabila ni ngumu kupata maendeleo kwa sababu ya hizi tabia

Kuna baadhi ya koo / makabila ni ngumu kupata maendeleo kwa sababu ya hizi tabia

round kick

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2025
Posts
345
Reaction score
1,145
Mtu katoboa kwenye familia, watu wanarundikana kumuomba pesa tena kwajili ya matumizi badala ya mitaji, kukodi mashamba, n.k. Ndio hawa virusi wanafika miaka 40 bado wanaomba pesa, ukiwanyima unatangazwa ukoo mzima unaanza kushambuliwa huwapi pesa ndugu zako, yani wanachojua ni matumizi tu na wapo entitled vibaya mno, wengine wanaenda mpaka kwenye vyombo vya habari kaka yetu kaacha kututumia pesa, khaaa!!

Watu wenye nguvu na afya kujazana kwa ndugu, Eboo! Mnaenda kujazana kwa ndugu yenu bila shughuli za kimaendeleo kufanya nini wakati hali zenu kiuchumi bado hazijakaa sawa ? ohh tunaenda kwa dada yetu kaolewa, ohh naenda kwa kaka yangu kapata kazi mjini, huko wakifika watakaa hapo bila kufanya shughuli za kimaendeleo ? Yani mnamtegea mume wa kaka atoe pesa au kaka atoe pesa, hao watu wameridhika kabisa hawataki kujituma, unamtafutia mtu kazi anaanza kulalamika huko kwenu "ananinyanyasa kanitafutia kikazi cha laki 2 wakati yeye ana pesa nyingi" jamii zinazojitambua haya mambo ya kusalimiana ni wiki 2 top au ukikaa sana basi uwe kwenye shughuli zako kama masomo.

Uwajibikaji mdogo kwenye vitega uchumi kwasababu ya kuwa familia au koo moja, umeamua kupunguza kelele unawaleta ndugu zako kwenye biashara lakini wanaanza kukuharibia, pesa inachukuliwa bila taarifa, garu ya ofisi inatumiwa matumizi binafsi, kuingia ofisini saa nne, kunyanyasa wafanyakazi wengine, n.k. hii yote ni kwasababu "biashara ni ya kaka", entitlement inayoweza kuua kabisa biashara iliyopata jina kubwa kwa jasho la miaka mingi.

Watu kupoteza muda kwenye majungu na umbea – Kuna baadhi ya sehemu vijana kwa wazee wakiamka kutwa nzima ni kushinda vibarazani, vijiweni wakicheza bao, kula kashata na story nyingi sana za kuzungumzia watu badala ya kujadili mawazo ya maendeleo, watu wanapoteza muda wakijadili maisha ya wengine. Majungu hayasaidii maendeleo ya familia wala ya mtu binafsi.

Kujenga uhasama kwa anayefanikiwa – Badala ya kumtia moyo na kujifunza kutoka kwake, wengi wanamchukia na hata kumuharibia jina kwa chuki zisizo na msingi. Watu wanaenda kwa waganga kuroga ndugu zao
 
Hata Kwa hao waliopata mafanikio Kuna majungu pia Tena haswaa watu weusi tumeumbiwa roho za kwanini
 
Aliyeshiba humsahau mwenye njaa...
Kuna muda hayo ni maneno ya anaeomba pesa kila wiki / mwezi, anachojua ni kula tu, kuwekeza hataki, msaada ukikata huanza kutamka hayo maneno
 
Jitahidi uongeze kipato kwanza malalamiko Kama haya hutolewa na watu masikini wa akili na fedha.
Billgates na kina Elon Musk huwezi kuta ndugu zao wamejazana nyumbani kwao, ndugu zao wanajishughulisha, hawarogani, hakuna majungu, n.k. wewe mmatumbi endelea kupiga majungu
 
Kuna muda hayo ni maneno ya anaeomba pesa kila wiki / mwezi, anachojua ni kula tu, kuwekeza hataki, msaada ukikata huanza kutamka hayo maneno
Mpe mtaji na umwambie kuwa akisimama akurejeshee ... Unajua Mungu kaumba levels ? Maskin na matajiri kwasababu Gani?
 
Waafrika wengi tunafanana kwa tabia na maisha yetu. Mmoja kati yetu(mwana ukoo) akifanikiwa, tunaona vyake ni vyetu, na asipotupa tunaona katunyima halali yetu. Hii inatokana undugu tulionao huwezi kukwepa.
 
Waafrika wengi tunafanana kwa tabia na maisha yetu. Mmoja kati yetu(mwana ukoo) akifanikiwa, tunaona vyake ni vyetu, na asipotupa tunaona katunyima halali yetu. Hii inatokana undugu tulionao huwezi kukwepa.
Mwafrika amelaaniwa

Tazama waarabu , wahindi , wasomali wanavyosapotiana kiuchumi na kimaisha
 
Watu weusi wana roho mbaya sana, hata tabia za kuomba omba ni matokeo ya hizo hizo roho mbaya. Unajitahidi unalipia ndugu mpaka mamilion ya ada ili siku moja hizi kero zikuondokee lakini wapiii. Na unakuta mtu ana wazazi wake wote wawili. Kitu mtu mweusi hukifanya kwa ufanisi bila tija ni umalaya, uchawi, majungu na ufitini. Wachache sana hizi tabia zimewaepuka. Halafu hata uwakute nchi za watu wengi wao hawajielewi zero social skills. Huku uswahilini mtu Unajitahidi ku mind your own business napo utaundiwa zengwe na na kuekewa vigenge. Unakuta jitu zima linataka ulipe zawadi kisa eti ni mwaka mpya.
 
Back
Top Bottom