Kuna bia za kike na za kiume?

mchagua bia si mlevi gentleman 🐒
Kwa Nini mkuu, mfano bia Zina harufu mbaya..

Ukimuongelesha mtu kwa ukaribu pia jasho mkipishana unaona kabisa huyu ni mlevi..

Kuna wanao kunywa spirit tuu, wine TU, imported beer tuu na wale wa local beer bila kusahau banana,ulanzi, GONGO, chimpumu, niagieni e.t.c 😊😊
 
Bia ya kiume ni Safari lager
 
Mnanywea Uswahilini bila shaka, Nakumbuka nilipokuwa sekondari ya Azania, Sisi watoto wa Tandika tulikuwa tunawacheka watoto wa kishua waliokuwa wanakula kiepe yai, huku tukijisifia kula mihogo na chachandu.

Lakini ukweli ni kwamba sisi wa uswahilini hatukuwa na hela ya kumudu bei ya chipsi, ilikuwa wivu tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…