Kuna chuki naanza kuiona inachomoza Tanzania

cumbamalema

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2024
Posts
366
Reaction score
820
Kuna chuki naanza kuiona inapandikizwa ndani ya Tanzania, kitu ambacho siyo kizuri kwa mstakabali wa nchi yetu, kilichotokea Mbeya ni mfano mdogo tu wa kundi la watu wengi wanaoamuliwa cha kufanya au kufuata na kikundi cha watu wachache, huwezi kumlazimisha binadamu apende asichokitaka, hata ukipita Mitaani ukajaribu kuongea na watu utaiona hiyo chuki ya waziwazi kabisa.

Na hii yote imesababishwa na kupotea kwa watu na Serikali kushindwa kuwapa wananchi majibu ya kujitosheleza wamekuwa na hasira sana na kujiona wao kama ni kundi la watu wa kupuuzwa

Tumuombe Mungu tusifike huko kwani tunakoelekea ni kubaya
 

Naomba tufike huko maana tumechelewa sana
 
Haukufafanua mkuu. Ila kwa kinachoendelea kuna hatari ya kuongeza chuki naogopa kusiwe na visasi siku za usoni.
 
Umeishia darasa la tatu?
 
M Mbaya sana hii
 
Haukufafanua mkuu. Ila kwa kinachoendelea kuna hatari ya kuongeza chuki naogopa kusiwe na visasi siku za usoni.
Yaani tunakokwenda siyo kuzuri kabisa,nashukhuru Magufuri aliweza kucheza na akili za watu wanyonge ambalo ndiyo kundi kubwa kabisa akaweza kufanya chochote kama Rais
Lakini kwa kipindi hiki kuna gape kubwa sana kati ya selikali na wanyonge,au sijui tumetoka kwa Magu tunajihisi kama bado hatuthaminiwi, lakini napenda kusema kuna moshi unafuka kila mtu anataka kusema au kuonyesha kitu fulani wakati haya yote ilibidi yafanywe na Rais kama Jemedar wa inchi,ukiambatanisha na matukio ya huko nyuma ambayo mpaka leo hayana majibu kamili inatisha, tunaombeni mlioko kalibu na Rais na wanaoitakia mema Tanzania wamwambie ukweli Rais,watu wanataka majibu, Siasa za kistarabu na akomeshe haya mambo ya utekaji,siyo maendeleo peke yake hayaweze kuwaridhisha wananchi ni pamoja na Amani pia
 
Katika kuhubiri Amani hakuitaji umeishia darasa la ngapi? Kumbuka hao wenye elimu ndiyo wanaoharibu amani ya inchi
Jibu swali, maana inawezekana tatizo lako ikawa ni ukosefu wa maarifa na akili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…