Kuna haja mamlaka husika kudhibiti wasafirisha mayai kwa baiskeli

Kuna haja mamlaka husika kudhibiti wasafirisha mayai kwa baiskeli

Unataka wasafirishe kwa punda au ndege?

Wameokoa polution, msongamano barabarani, wahatumii mafuta mnayogombnia, wewe unawatakia nini hawa watu? Walale njaa wewe utawapa watoto wao chakula au kuwasomesha? Sijasoma ulichoandika nimesoma heading tu ikani touch. Ningekuwa mod ningefuta hii mada.
soma pia alicho andika though kusema wazuiliwe kazingua ila ana ujumbe sensitive sana ndan yake
 
Huna point ya msingi waacheni watu waishi kwa Uhuru wewe unaendesha IST gar ya mil 2 lkn unaleta dharau kwa Mtu anayesafirisha Mayai ya mil 10 shame
kweny baiskeli gan , hayo mayai yanasafirishwa?
 
Ni usafiri hatarishi, hata kuwa rahisi mtu kupoteza mtaji wake in a second!! Kuwa positive kuwashauri watu ili kuboresha maisha yao, Mimi Naona wangekodi canter wakakutana na mayai Yao kunako Wateja Kwa kuchangia gharama ( group)
atleast umeongea point mkuu
 
soma pia alicho andika though kusema wazuiliwe kazingua ila ana ujumbe sensitive sana ndan yake
Ujumbe anao hatukatai ila kumbuka ujenzi wa barabara zetu siyo rafiki. Nchi nyingi zikijenga barabara, huwa zinaweka waendesha baiskeli halafu na watembea kwa miguu. Sisi pamoja na kusemba mita 20 ziwe za barabara, utakuta ni mita labda 10 tu zinatumika mita 10 au tusema 6 zipo idle ndo mwanzo wa machinga kupata mahali pa kufanya biashara zao. Kosa letu tusiwalaumu waendesha baiskeli.
 
sasa unaingia kanda maarum ya mayayi be wochifulu poti...hii ni rorya ya piri mura
 
Mleta mada ameongelea issue ya usalama Barabarani wala hajataka hao wabeba mayai kwa Baiskeli waondolewe,ni kama wale tu ambao hua wanalalamikia uendeshaji wa hatari kwa wale Bodaboda,

Tuwe tunasoma thd na kuzielewa kabla ya kumshambulia mtu,watu wana stress sana aisee,anatafuta tu mtu wakum malizia stress zake bila sababu ya maana.
 
Mamlaka za usalama wa barabarani wanapaswa kuwaangalia kwa usalama wao na watumiaji wengine wa barabara na ikiwezekana kushurtishwa kwa faini pale wanapokosea kama watumiaji wa vyombo vya moto, labda hii italeta nidhamu kwao.

Mbali na kushurutishwa wanapokosea, unashauri namna gani iliyo salama zaidi wao waitumie huku wakiwa wakiendelea kupambana kutafuta ugali wao?
 
Kwa wanotumia Pugu/Nyerere Road kutokea Gongo la mboto kupitia Airport watakuwa mashuhuda wa utitiri wa wasafirisha mayai maarafu kama Wakurya wanao ongozana wakiwa na shehena za mayai kwenye baiskeli.

Tatizo linakuja kwa namna ya wanavyoongozana katika barabara kubwa na kuchomekea wenye magari. Na ikitokea kwa bahati mbaya ukamgusa mmoja wao basi wanakuzingira na kukufanyia fujo. Uendeshaji wao wa baiskeli ni wa hatari mno, kama haupo makini ni rahisi sana kuwagonga. Kitendo chao cha kutokutaka kuendesha pembezoni mwa barabara kunaleta hatari zaidi za kuweza kuwavaa na kuwagonga.

Mamlaka za usalama wa barabarani wanapaswa kuwaangalia kwa usalama wao na watumiaji wengine wa barabara na ikiwezekana kushurtishwa kwa faini pale wanapokosea kama watumiaji wa vyombo vya moto, labda hii italeta nidhamu kwao.
Sasa kuna siku palitokea ugomvi mkubwa sana kati ya wauza mayai na wachimba mchanga... likuwa vita haswaa...!!! Walipigana machepe, nyundo mawe... Baiskeli za wakurya zilikusanywa kwenye serela
 
Mbali na kushurutishwa wanapokosea, unashauri namna gani iliyo salama zaidi wao waitumie huku wakiwa wakiendelea kupambana kutafuta ugali wao?
Kutojimithilisha na magari na kutambua athari kubwa zaidi itapatikana kwao pale wanapomchomekea mwenye gari kupelekea kugongwa. Mayai yatavunjika pengine na mwili kuumia.
 
Kiujumla sheria za usalama barabaran hapa bongo hazifwatwi
Miundombinu duni
Ndio jumuishi wa matatizo yetu
Barabaran kuna
Mbuzi
Baiskeli
Boda
Guta
Gari
Haya yote at the same lane kweli?
 
Back
Top Bottom