Kuna haja ya Rais Samia kufundishwa jinsi ya kudhibiti hisia zake anapoongea/anapohutubia

Kwenye Hard Talk si atamkata mwandishi vibao huyu?!
 
Tatizo Rais wetu anataka kumfurahisha Kila mtu kitu ambacho ni kigunu.
 
Hapo mama alimjibu vizuri sana Kikeke. Huyo jamaa si ndiye alikuwa anasema watanzania tutakufa na maiti zetu zitakuwa zinaokotwa mitaani kama nzige wakati wa corona? Mnataka ajibiwe kwa kubembelezwa ili iweje, kuwafurahisha mabeberu?
Kwa taarifa yake, huko kwao ndiko wamekufa kwa corona kama nzige, wakajibana kwa lockdowns mpaka wakaachia; sisi huku kwetu tunadunda tu, wao bado wanavaa barakoa, sisi tulishasahu hata rangi zake zikoje.
Mbona hajawauliza chadema kwa nini wakati wa uchaguzi wana sera ya "sumu haionjwi kwa ulimi"?
Asante sana mama kwa jibu ulilompa, nakupa hi five!
 
Una umri gani? Ukimtoa Mwinyi na Nyerere, style hiyo ya majibu ilishatumiwa na Mkapa, Kikwete na Magufuli. Yaani sio style mpya.
 
Na tushukuru ni mwarabu angekuwa mmatumbi wa huko kwa profesa angetamka hata yale maneno magumu
 
Aliyemtangulia alikuwa hovyo sana kuliko yeye. Somo lingeanzia kwake kwanza.
 
Inabidi tuwe wapole tu, huyu ndio rais mpaka 2025 ikiwezekana ni mpaka 2030. Wakati hayati JPM anampa umakamu wa rais labda hakujua mipango ya Mungu ni ipi ifikapo March 2021, tuwe wapole tu.
 
Akitoka madarakani akajiangalia hizo Interview zake ndio atajiona kuwa alikuwa hajui

Kuna protocol inakuwa haiendi sawa,,, Rais huwa anaandaliwa maswali na majibu pia. kuepusha kuvurunda
Hayati JPM hata hizi interviews hakuwa akizifanya, alijijua udhaifu wake upo wapi.
 
Ila kwa nafasi aliyonayo anapaswa ajifunze kujizuia.

Maana anajibu kishari kama huyo Kikeke ndio kadai katiba.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] upo sahihi nimeangalia iyo clip apo mama anaonekana kuwa jazba....!!!! Nikionacho mama sio mzuri wakujibu waswali naisi anaulizwa maswali ambayo yeye hana majibu sasa anaishia kuwa mkali!!!! Kwasbabu hapo anaongea kwa ukali maybe alikuwa anamtisha kikeke kwa ukali ule ili asiendelee kumuhoji
 
Una umri gani? Ukimtoa Mwinyi na Nyerere, style hiyo ya majibu ilishatumiwa na Mkapa, Kikwete na Magufuli. Yaani sio style mpya.
Umri wangu hauna mantiki katika hili swala. Kuhusiana na hao uliowataja, walijibu hoja ya msingi hata kama walitumia ukali.
Rejea tena hiyo clip halafu uone kama swali lilijibiwa ndugu. Tujaribu kutofautisha mahaba na ufuasi. Wengi wanaohalalisha ujibuji wa mama ni wale wafuasi ambao lolote likisemwa kinyume na kusifia basi wanachukulia kuwa mpendwa wao kapingwa ama kadharaulika.
 
Kuna aina Tatu ya kujibu maswali.
1. Swali kwa Jibu
2. Swali kwa swali
3. Swali kwa maelezo
HIVYO BASI:
Mama alikua anatumia aina ya pili ambayo ni SWALI KWA SWALI.
 
Udikteta ndio mfumo wa kimungu kwa wale wenye kuamini dini .Mfumo bora kabisa
Sasa waliosoma politics wenyewe ndo wanaongoza kwa kutojua kitu. Wanahisi udictator ndo mfumo mzuri wa uongozi. Kama Bashiru alivyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…