Kuna hasara gani endapo mtu atasoma form 5&6 (A level) kwa shule za private,?

Kiwalo

New Member
Joined
Feb 26, 2024
Posts
3
Reaction score
3
Naomba mnipe majibu jamani,

Kuna hasara gani endapo mtu atasoma form 5&6 (A level) kwa shule za private,?​

 
Atatumia hela nyingi za wazazi wake kwa kitu kilekile ambacho angekipata bure kwa shule za umma. Pili kukosa uwezo wa kupambana katika mazingira halisi ya kitanzania kuliko kuandaliwa kila kitu bure na kukalilishwa.
 
Kuna hasara gani endapo mtu atasoma Form 5&6 katika shule za private?

Msaada jamani
 
Mkopo anapata labda kama kuna mwongozo mpya
 
Usipoteze mda kwenda 5 na 6 , Haina professional yoyote , tafuta cheti chenye professional, kwa Tz ya kipindi hiki 5 na 6 ni kupoteza mda. Haina thamani tena. Mwanzako anasoma miaka mitatu diploma anauwezo wa kuomba kazi yoyote na akaajilika , lakini six labda ukalime JkT .
 
Hasara atakayopata ni kupoteza muda wake huku akiwa na uwezekano wa kutopata marks zinazoweza kumpeleka akasome degree chuo. Mwisho wa siku anaweza kurudi na kuanza kusoma tena diploma kitu ambacho alipaswa akisome muda huu
 
Ni kupoteza muda kama atafeli, ila kama akifaulu ni best route to university.
 
Atatumia hela nyingi za wazazi wake kwa kitu kilekile ambacho angekipata bure kwa shule za umma. Pili kukosa uwezo wa kupambana katika mazingira halisi ya kitanzania kuliko kuandaliwa kila kitu bure na kukalilishwa.
Una mawazo ya kimasikini sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…