Kuna hatua ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike. Mnauza mali zote kulipia matibabu, ndugu anakufa kisha familia inabaki na umasikini wa kutupwa

Kwenye kupambania uhai wa mtuwako wa karibu aisee,achana na mali hata figo mtu unaweza toa.
 
Yani ingekuwa kuna option hio utajiri ungekuwa sio nyumba wala asset bali ni uwezo wa kuzuia ndugu asife kila mtu ndio ingekuwa lengo lake namba 1!

Kwamba familia yako na ukoo wasife.
 
Licha ya udogo wako Soja unaandikaga mada za maana sana. Kudos Soja wangu.

Kuna kisa kimoja cha shangazi yangu mwalimu mstaafu nitakuja kukiandika hapa ngoja kidogo kwa maana nipo safarini.

Mkuu andika sasa maana huna mkataba na Mungu........Haya mambo ya kusema nitaandika siku flani sio.

Ndio kisa Cha DJ JD na Late DJ OMMY............DJ OMMY aliomba msaada kwa JD na JD akampromise kumpa around January(Ahadi alitoa December) ,ilivyofika Jan Late DJ OMMY akampigia DJ JD ,JD akaiona Missed call yake ila akajisahau Kumpigia baada ya siku mbili akasikia DJ OMMY kavuta! Ilimuuma sana na kujiona kwamba inaonekana DJ OMMY alikuwa anahitaji msaada wa fedha kwa ajili ya matibabu na kwa kukosa fedha ikapelekea kufariki.
 
Jamaa anaongea, akizaa watoto na mke anae ataona jinsi ambavyo hata taxi bubu yake anaweza kuuza hata kwa bei ya hasara ili asimkose mwanae

Kabisa sijaona mbadala wa uhai ,kama kuna possibility ya kuokoa uhai kwa kuuza nyumba ni bora iuzwe!! Watu wanakufa kwa malaria tu hivyo hata figo/kansa kuna possibility ya kupona vile vile,
 
Kabisa sijaona mbadala wa uhai ,kama kuna possibility ya kuokoa uhai kwa kuuza nyumba ni bora iuzwe!! Watu wanakufa kwa malaria tu hivyo hata figo/kansa kuna possibility ya kupona vile vile,
Familia masikini/fukara kuuza nyumba yao ya pekee ni pigo kubwa sana kwa watoto wadogo.
 
Kabisa sijaona mbadala wa uhai ,kama kuna possibility ya kuokoa uhai kwa kuuza nyumba ni bora iuzwe!! Watu wanakufa kwa malaria tu hivyo hata figo/kansa kuna possibility ya kupona vile vile,
Eeh mkuu, yani mambo haya ni mitihani ya kimaisha. Uwe na asset halafu maza anaumwa ile mbaya na anatibika eti useme siwezi kuuza tv nikamtibu bi. mkubwa. Halipo hilo!
 
Ina maana baba kazaa akiwa na miaka 50+ au?
Soma hapa. Wewe pia ulikuwa unaunga mkono wanaozaa uzeeni.


Pia kumbuka terminal illness inawakuta sana vijana siku hizi ambao wapo below 45. Kumbuka Sajuki wa bingi movie
 
Yah i remember Sajuki
 
Kuna kuitumikia mali na mali kututumikia sisi...

Kama sherehe tunatumia mamillions ya pesa,hvyohvyo tunajibana tuchange tusherehekee tule bata....

Bado wale wanaoonga majumba,simu,gari n.k

Sasa wewe unashangaa mtu kuuza vitu kwa ajili ya matibabu....jiandae kushangaa wale wanaotoa michango sku ya msiba kuliko siku za kuugua mgonjwa.
 
Eeh mkuu, yani mambo haya ni mitihani ya kimaisha. Uwe na asset halafu maza anaumwa ile mbaya na anatibika eti useme siwezi kuuza tv nikamtibu bi. mkubwa. Halipo hilo!
Mbona Ulaya kama mgonjwa ni mahututi na mnajua hawezi kupona anapewa option ya Anaesthesia (kipimo kinazidishwa) mpaka unafariki ili kupunguza maumivu, gharama za kulaza/Matunzo, na sijui kuuza mali ili apone.

Nadhani ni uelewa tu wa jamii na kukubaliana na ukweli kwamba huyu atakufa tu hta tufanye nini. So ku minimize risks ni muhimu zaidi ya kuwa emotional.

Btw sheria imepitishwa nchi za EU huko kwamba hyo dozi anaweza pewa mpaka mtoto mchanga. Mfano mtoto anazaliwa leo ila tayari mapafu cjui yametoboka instead of kuishi maisha yake yote na mipira kifuani mnaona arudi tu kwa muumba wake kuliko ateseke kwa miaka 60 hapa duniani.
 
You said it right bro.
 
Insults reported. WELCOME TO MY IGNORE LIST. GOOD BYE.
who cares! mimi mwenyewe nimejiweka kwenye IGNORE LIST yangu unadhani nashughulishwa sana na wewe kuniweka kwenye list yako!? acha kua NAIVE.
 
Kuna kuitumikia mali na mali kututumikia sisi...

Kama sherehe tunatumia mamillions ya pesa,hvyohvyo tunajibana tuchange tusherehekee tule bata....

Bado wale wanaoonga majumba,simu,gari n.k
Hii ipo sana Afrika mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…