Kuna Homa za Mafua Makali zinasambaa kwa Kasi Mitaani, Mamlaka mbona hazitoi taarifa kuhusu hili?

Kuna Homa za Mafua Makali zinasambaa kwa Kasi Mitaani, Mamlaka mbona hazitoi taarifa kuhusu hili?

Mtoa Taarifa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2024
Posts
213
Reaction score
671
Kumekuwa na ongezeko la homa kali za mafua zinazowakumba wananchi wengi katika maeneo mbalimbali ya Tanzania. Wananchi wanaonekana kuwa na wasiwasi juu ya kasi ya kusambaa kwa ugonjwa huu, lakini wanahoji ukimya wa mamlaka husika kuhusu hatua zinazochukuliwa kukabiliana na hali hii.

Je, mamlaka zinafanya jitihada zozote za kudhibiti homa hizi, kutoa elimu kwa umma, au kuhakikisha kuna upatikanaji wa taarifa sahihi na ushauri wa kiafya kwa umma?

Kwa nini mamlaka hazitoi taarifa kwa umma ili kuwajulisha kuhusu hali halisi na namna bora za kujikinga? Utoaji wa taarifa sahihi na kwa wakati ni muhimu ili kuzuia taharuki na kuwapa wananchi mwongozo wa hatua stahiki zinazopaswa kuchukuliwa ili kujikinga na kusambaa zaidi kwa homa hizi.
 
Mkuu wewe chukua tahadhari mwenyewe na familia yako. Itafute walimu ya ugonjwa husika jifunze usisubiri serekali maana ina mambo mengi ikiwemo Ku fake data za uchaguzi
 
Mimi familia yangu wameugua watu wawili kikubwa ni kwenda hospital na kunywa maji mengi. Ni kama korona fulani hivi amazing
 
Wachawi wako kazini! Wewe unafikiri ulogwe ukaokote makopo tu au uwe zezeta? Wanakupiga tukio ili hela yako ya maendeleo iende kwenye matibabu! Wanakupiga tukio ili usiende kazini au utendaji wako upungue uangukie kwenye umasikini au ufukuzwe kazi! Wachawi nao wanaenda na wakati kaa ukijua! Kalaghabao!
 
Kumekuwa na ongezeko la homa kali za mafua zinazowakumba wananchi wengi katika maeneo mbalimbali ya Tanzania. Wananchi wanaonekana kuwa na wasiwasi juu ya kasi ya kusambaa kwa ugonjwa huu, lakini wanahoji ukimya wa mamlaka husika kuhusu hatua zinazochukuliwa kukabiliana na hali hii.

Je, mamlaka zinafanya jitihada zozote za kudhibiti homa hizi, kutoa elimu kwa umma, au kuhakikisha kuna upatikanaji wa taarifa sahihi na ushauri wa kiafya kwa umma?

Kwa nini mamlaka hazitoi taarifa kwa umma ili kuwajulisha kuhusu hali halisi na namna bora za kujikinga? Utoaji wa taarifa sahihi na kwa wakati ni muhimu ili kuzuia taharuki na kuwapa wananchi mwongozo wa hatua stahiki zinazopaswa kuchukuliwa ili kujikinga na kusambaa zaidi kwa homa hizi.
Hili ni kweli 78%
 
Back
Top Bottom