Pre GE2025 Kuna kila dalili uchaguzi mkuu 2025 Upinzani ukikazana unachukua, je Mwenyekiti Mbowe ataruhusu hili?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Nehemia Kilave

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2022
Posts
1,414
Reaction score
3,118
2025 , kuna dalili nyingi sana ambazo zinaonesha kuna uwezekano wa Upinzani kuchukua dola .

Kuna dalili 2025 kuna wana CCM kindaki ndaki wataihujumu CCM

Kuna dalili 2025 vyombo vya dola vikawa upande wa wananchi

Kuna dalili Asilimia kubwa ya wapiga kura wakawa vijana

Lakini sio siri CHADEMA ndiyo chama kikuu cha Upinzani na kuna kila dalili Mwenyekiti anatembea na maelekezo kutoka upande mwingine juu ya Uchaguzi wa 2025 .

Je kina lissu na wengine wataweza ?
 
Tangu Tundu Lissu aseme kuwa kuna Kiongozi Mwandamizi wa CHADEMA alienda na Abdul sebuleni kwake ili apewe Rushwa, na kuoneshwa orodha ya Viongozi wengine waliochukua "Mpunga" sina imani na Upinzani kama wanaweza kuchukua Dola.

Kinachoonekana ni kuwa kuna Viongozi Mamluki ndani ya Upinzani ambao wamechukua "Mpunga" na kuendelea kubaki kama Wapinzani huku wakiwa ni wavurugaji..
 
Uchukue upeleke wapi?
 
Labda upinzani against mbowe wa chakademus
 
Hili liko wazi
 
Vyombo vya ulinzi na usalama, vyombo vya dola ndio wanafiki namba 1 Tanzania, ndio chanzo HALISI cha Matatizo yote katika nchi hii. Wao wanatumika kuwabeba CCM kwenye uchaguzi hasa kuiba kura na kulinda watu wanaoharibu uchaguzi.
Wao ndio wanasababisha tuwe chini ya utawala wa watesi wetu CCM. Hali ngumu ya kiuchumi, vijana hawana ajira. Hivi hao maaskari hawana maisha magumu? je watoto wa maaskari wote wana ajira? Je ninyi maaskari hamna ndugu,jamaa na marafiki wenye hali ngumu? Je ninyi maaskari hamna watoto wa ndugu zenu, marafiki zenu ambao ni wasomi wazuri tu ambao hawana ajira mpaka leo?

Najua viongozi wengi wa vyombo vya dola mnatumia JF anzeni kujihoji juu ya halizenu, juu ya hatma ya watoto mliowasomesha kwa gharama kubwa na hawana ajira.

Muda umefika ninyi maaskari mkatae kutumika na ccm kuiba kura na kutesa watanzania wenzenu ambao lengo lao ni kututoa kwenye mateso makali ya ccm. Ninyi maaskari mmeapa kuilinda Tanzania, sio kuilinda CCM, mmeapa kuwalinda watanzania, sio kuwalinda mafisadi CCM. Muda umefika mmbadilike, mkatae kutumika na CCM.


Kama vyombo vya ulinzi na usalama vikiamua kukataa kuiba kura, CCM hawashindi uchaguzi labda washinde njaa.



Ova
 
Na Mungu akayabariki matazamio yako.
 
Mimi nilidhani ndio ungejua kuwa upinzani uko vizuri.....kiasi cha kugawiwa fedha ili waachie ngazi maana yake wanayo hadhi.

Na ukiona issue imevuja basi huo ndio ukomavu wa chama.

Kwanini wanahangaika kuwahonga? What is wrong? Je mbeleko ya ccm inafika mwisho?
 
πŸ˜†πŸ˜†πŸ˜†πŸ˜†
 
Umeandika deep sana.

Aking'ang'ania kugombea, kitu inaenda upinzani. Na mgombea wa upinzani atatoka tena CCM!!

Kugombea Kisha usishinde ni sawa tu na " KUTOGOMBEA".

Mbowe Si boya, aaminiwe!!
 
Umeandika deep sana.

Aking'ang'ania kugombea, kitu inaenda upinzani. Na mgombea wa upinzani atatoka tena CCM!!

Kugombea Kisha usishinde ni sawa tu na " KUTOGOMBEA".

Mbowe Si boya, aaminiwe!!
Yeye si boya hilo liko wazi na ndiye anatukwamisha .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…