Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Umeambiwa ya kaisari mwachie yeye na ya mungu mwachie mungu! Maana yake ya duniani waachie wanadamu walio hai na ya mbinguni mwachie Marehemu! Nani alikufa akarudi duniani kutusimlia? Kuzikwa na Padre ni muhimu na akikataa inaacha simanzi kwa wanaobaki hai.
Siku hizi wamejanjaruka hawakatai kuzika hata kama ulikua huhudhurii. Wanachofanya ni kwamba mkienda kuomba huduma ya ibada ya mazishi na kama marehemu alikua sio mchangiaji, basi mnapigiwa mahesabu ya michango yote ambayo alitakiwa kulipa. Kuna jamaa tulilipa laki 6 ndio padri akakubali kuja. Ukiona padri hajaja kabisa ujue ndugu wameshindwa kulipa "deni" la michango!
 
Leo ni Jumapili ya matawi Yesu anaingia Jerusalem, lakini nikitafakari imani yangu ya ufuasi wa kristu napata mashaka makubwa sana.

To declare interest mimi nimezaliwa nimejikuta tu ni mkatoliki kwahiyo nipo hivyo mpaka leo, mahusiano yangu na Mungu naamini ni mazuri kiroho lakini mahudhurio yangu kanisani kwa miaka ya karibuni si mazuri huwa nakwenda na kuacha kwenda.

Basi mambo yasiwe mengi last Sunday nikatimba church kwenye parokia yetu mambo niliyokutana nayo huko ni ya kusikitisha na nathubutu kuita kile alichokikemea mwokozi wetu Yesu kristu kwamba wasigeuze nyumba ya baba yake kuwa pango la walanguzi, kwa hakika hicho ndicho kinachoendelea parokiani kwetu si kanisa tena bali ni pango la walanguzi.

Sisi Wakatoliki huko nyuma tulikuwa tukiwacheka Lutheran kwa utaratibu wa sadaka nyingi na bahasha nyingi kumbe sasa utaratibu huo umeingia kwa speed kubwa kwenye kanisa katoliki ibada ya misa moja sadaka mnatowa mara saba, sina hakika na parokia zingine hali ikoje.

Sasa kila mwanaparokia unapewa kadi ya kuchanga pesa ya kuwa mkatoliki mume na mke 10,000)= kwa mwezi na watoto buku mbilimbili kila mwezi hii ni nje ya sadaka harambee na michango mingine, tunakwenda wapi?

Najuwa wapo watetezi waliolewa mvinyo wa dini watatetea uharamia huu kwa utetezi ni lazima tuchangie ujenzi wa kanisa, hakuna anayekataa hilo na tumekuwa tukijitolea miaka yote kwa kiasi, lakini naamini mtu ambaye yuko free minded hawezi kutetea uharamia huu kugeuza kanisa kuwa pango la walanguzi, na wasiokuwa na pesa za kuamka kwenye mabenchi mara saba kutowa hizo sadaka hawatojisikia vizuri na wataacha kuja kanisani kwa kuteswa kihisa kila watu wakiinuliwa kwenye mabenchi wao hawana kitu.

Hiyo sasa tisa kumi ni hawa jamaa zetu born again, nipo hapa nyumbani namsikiliza mtumishi wa Mungu akitangaza viwango vya sadaka ya kugombowa uzao wa kwanza ni laki mbili, uzao wa pili laki na na nusu, uzao wa tatu laki.

Kutokana na uharamia huu na unyang'anyi unaoendelea kupitia mwamvuli wa dini serikali haiwezi kusaidia lolote katika hili kwa sababu ni partners muhimu in crime.

Kwakuwa waislamu wanajitambuwa sana katika hili ni wakati sasa kwa wakristu wote kuamka na kupinga dhulma hii ambayo cha kusikitisha sasa imeingia radmi kanisa katoliki na hakuna hata mkatoliki mmoja aliwahi kuhoji miradi yote ya kanisa hadi mkombozi bank ipo kwa faida ya nani na inalisaidia vipi kanisa?

Tumsifu Yesu kristu.
Dini ni scam tu,njia ya kucontrol watu,ndo mana watoto wangu sitaki wawe chini ya mnyororo wa dini wawe huru.
 
Siku hizi wamejanjaruka hawakatai kuzika hata kama ulikua huhudhurii. Wanachofanya ni kwamba mkienda kuomba huduma ya ibada ya mazishi na kama marehemu alikua sio mchangiaji, basi mnapigiwa mahesabu ya michango yote ambayo alitakiwa kulipa. Kuna jamaa tulilipa laki 6 ndio padri akakubali kuja. Ukiona padri hajaja kabisa ujue ndugu wameshindwa kulipa "deni" la michango!
Kili imani yako ukiwa hai utazikwaje kama ulikataa kuikili?
 
Ndiyo maana nimesema wewe siyo mkatoliki tena, itakuwa unajilazimisha tu ili uwe huru ubadili dini uwe Muslim, maelezo yako yanakuelezea na kuonyesha imani yako juu ya dini inaelekea upande hupi.
Huyo ni mkatoliki kabisa na asemacho ni kweli bila chenga. Hata mm ni mkatoliki naunga mkono home yake. Katoliki ukusanyaji wake wa fedha hata hao TRA wakasome.

Ili wakuhesabu unafaa huduma zao, lazma wajue kama unasali jumuia. Na huko jumuia ndio kuna michango na mikusanyo ya fedha isiyo mithilika. Kwa nyongeza tu, hata shule za katoliki bei ipo juu kama za watu binafsi, na zina michango na mahitaji ya malipo ya ajabu sana. Hata Mia ikipungua wanamtimua mtoto. Kwanza kuzipata tu hizo shule kwa mzazi alieshiriki michango ya ujenzi ni shida, hata kama mtoto ana vigezo.

Mleta mada kaeleza vyema sana, kuwa kama vyanzo vya mapato kama kumbi Mashule mahospitali frame za maduka vimejengwa kulisaidia Kanisa, sasa kuna haja gani ya kukakamua namna ya uporaji waumini walioshiriki ujenzi wake kwa fedha zao?

Hakuna mahali imeandikwa kwny biblia kuwa Utaenda mbinguni kwa kutoa sadaka au hutoenda kwakua hutoi sadaka. Unadhania Yesu alipo mwambie yule jamaa kauze ulivyonavyo uwape masikini kisha unifuate, angekuwa hawa mapadiri au wachungaji wa sasa, angesemaje kama sio kusema kauze ulivyonavyo kisha uvilete hapa ndio unifuate.
 
Siku hizi wamejanjaruka hawakatai kuzika hata kama ulikua huhudhurii. Wanachofanya ni kwamba mkienda kuomba huduma ya ibada ya mazishi na kama marehemu alikua sio mchangiaji, basi mnapigiwa mahesabu ya michango yote ambayo alitakiwa kulipa. Kuna jamaa tulilipa laki 6 ndio padri akakubali kuja. Ukiona padri hajaja kabisa ujue ndugu wameshindwa kulipa "deni" la michango!
Hii nimeipenda maana rambirambi zinaweza kuokoa jahazi. Ni uchuro kwa ndugu waliobaki kuona ndugu yao hakuzikwa na Padre!
 
Hayo ya kumwachia Kaisari badala ya kuhoji na kupata logic, hitaji la kuzikwa na padri na mengineyo mengi ndiyo indoctrination tunayozungumzia. Wanufaika walishaanda kauli za kukataza watu kuhoji sana na kujenga hofu kwanza ili wengine wabaki kufuata maelekezo tu.
Hujaelewa hoja yangu! Mimi nazungumzia ubinadamu tu. Masuala ya Mungu mimi siyazungumzii maana hakuna aliyekufa akarudi akatusimulia ni nini kipo huko. Nasema tunajua hapa kwetu mtu ukifa unazikwa na Padre au mchungaji. Hii haikuhusu wewe uliyekufa ila wale ndugu zako wanaobaki duniani inakuwa aibu yao. Ni vyema tukajitahidi kutoletea wasiohusika aibu zisizowahusu
 
[emoji1][emoji1][emoji1]Dini zote hawakupi mwanya wa kuhoji. Yaani mtu mmoja aliyejipa utumishi akisema kasema. And this is how religion was brought to Africa by missionaries to silence any spirit of consciousness. Times have changed na watu wanaanza kuquestion.
Unafikiri ni nani ambaye anazuia usihoji au ambaye anatakiwa kujibu hoja zako kwenye dini?
 
kimsingi miradi ya kanisa haina faida ya moja kwa moja kwa muumini asilani. Utadikia eti wanajenga shule na wakati huwezi kumpeleka mwanao akasoma bure kwenye shule zao. Na hata hospitali zao kama huna hela hutibiwi na wakati sadaka na michango unatoa. Kwa ufupi, haya madhehebu yana fanya biashara tu. na ni wakati muafaka wa sisi waumini kuamka
Halafu bila tone la aibu wanataka serikali iwaondolee kodi.
 
Hiyo mbona imefika kwa kuchelewa sana kanisani kwenu

Muda wa sadaka pastor akafungua kapu na kuruhusu watu watoe sadaka, zoezi lilipo kamilika akaja na ajenda nyingine ya mchango kwa ajili ya mradi wa kanisa wa mashine ya alizeti

Pastor kama kawaida na safari hii akawa anawaimbia na pambio ya kuwa motivate huku akiweka kapu jingine kwa ajili ya mchango wa huo mradi

Zoezi lilipokamika pastor akaja na agenda ingine kuwa leo hapo kanisani wametembelewa na mtoto wa miaka 7 anayesumbuliwa moyo, hivyo anahitaji msaada. Akatoa kapu jingine

Hapo ndio nikaona kuanzia waumini mpaka pastor wote hawana akili, nikajiuliza hizi pesa za sadaka si huwa tunaaminishwa kuwa zinaenda kusaidia watoto yatima na wagonjwa?

Imekuwaje leo mtoto mdogo huyu mgonjwa amekuja hapa halafu kanisa limeshindwa kumpatia sadaka ambazo ndio dedicated kwa ajili ya watu wa namna hiyo?

Mtoto alipata mchango wa 30,000 kwenye kanisa lenye waumini 300 kwa misa moja hiyo ilitokana na ulafi wa mchungaji kwasababu mchango wa matibabu ya mtoto ungeanza kabla ya sadaka watu wengi wangemchangia, ila kwakua pastor alikuwa mlafi akaona hizo pesa zote ziingie kwenye mfuko wake

Very sad [emoji22]
 
Dini zote hizi zilikuja na meli na mashua na waliua za kwetu pambaneni nazo
Ni waafrika tu ndio nadhani tunawaza hivyo, ukiangalia hizo dini zipo sehemu kubwa tu duniani ila hatuoni wengine kulalamika kwamba imani za mababu zao kuachwa na watu kufuata imani zengine.

Imani za asili ya India zimesambaa sana huko Asia katika nchi mbalimbali ila hatuoni hizo nchi kulalamika kwamba watu wao wameacha imani za mababu zao na kufuata dini za wahindi.
 
Huwa nawashangaa watu wanapolalama kwenye institution ambayo kujiunga na kutoka ni hiyari na tena haulazimishwi kutoa chochote.
Kama unaona makanisa yaliyopo hayafai, si kasajili la kwako Wizara ya mambo ya ndani uweke utaratibu unaouona unafaaa?
Sorry bro! Unachojaribu kukitetea hapa ni kipi?
 
Aya ya mwisho tayari inathibitisha wewe siyo mkatoliki.
Huyo jamaa..ni mamluki..sio mkristo fuatiria uzi zake utajua hilo..kaja kuleta hoja za kuvuruga kanisa la Mungu..atabue kutoa ni upendo..muumini wakweli hawezi kuacha kutoa sadaka kanisani.

#MaendeleoHayanaChama
 
Mkuu fikilia Sana imani zingini ni kukomoana tu bora waislamu ya menyewe ni kuswali tu basi.
Wavaa kobazi ni bahili hatari..wategemezi kila kitu wafanyiwe na waarabu..hadi tende wanasubiri waletewe na waarabu.

Ukristo ni dini ya upendo na utoaji..kama huna hela kaa kimya sio kutaka kuharibu utaratibu na tamaduni za wakristo.

#MaendeleoHayanaChama
 
Waislamu wanajali sana muda yaani wao siku ya Ijumaa wanaingia kama saa saba na ushee lakini saa nane tu tayari walishatoka.
Halafu zile sala zao fupifupi yaani ni Kama kanu saa au dakika 20 tu hao duh.
Time management hapa wapo vizuri.
Hata kuhoji tu hujui..sasa unataka watumie masaa mangapi kama kwa siku wanasali zaidi ya mara 5..hao ndio hawana time management.

Wakristo siku 6 piga kazi siku moja ni kupumzika na kuabudu...na zile sala ndogo ndogo binafasi..sasa wepi wanaofanya time management nzuri.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kwakweli waislam ukiugua hata mskitini inasemwa unachangiwa bd kuna wale wa kujitolea kutembelea wagonjwa wasojiweza na kuwapa misaada ya vyakula na dawa
Hivi si mkawe waislamu nani kawakataza..huwezi ubeza ukristo mana hiyo ndio kanuni yake ya upendonna kujari.

#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom