Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Zamani makanisa yalikuwa yanapata sana misaada toka nje lakini kwa sasa nje hawatoi sana misaada (wanasema mioyo yao kuhusu dini imepoa) so inabidi makanisa yajiendeshe yenyewe. Hapo ndipo uhitaji mkubwa wa hela unapoanzia
Makanisa ya kina Masanja, MC pilipili, Mwamposa, Gwajima n.k nayo unayaweka kwenye hili kundi la kunyimwa misaada?
 
Mimi sijaenda church na ninauhakika asilimia 100 kama Yesu atarudi muda huu, hakika mimi nitatwaliwa (chukuliwa) nipae na Yesu kwenda Mbinguni.

Shida wakristo hatuna Neno la Mungu, Tumesahau kabisa nini kilichofanyika Pale msalabani, na tumeona kama karama za Mungu hutolewa kwa fedha.
 
Kwakuwa waislamu wanajitambuwa sana katika hili ni wakati sasa kwa wakristu wote kuamka na kupinga dhulma hii ambayo cha kusikitisha sasa imeingia radmi kanisa katoliki na hakuna hata mkatoliki mmoja aliwahi kuhoji miradi yote ya kanisa hadi mkombozi bank ipo kwa faida ya nani na inalisaidia vipi kanisa?

Tumsifu Yesu kristu.
Viongozi wa Dini watafute kazi za kufanya, waache kutegemea sadaka kuendesha maisha Yao, kazi ya kuingoza ibada malipo yake ni mbinguni.
 
Life is a choice

Missionaries vs Explorers, Traders vs Missionaries & Explorers vs Traders
,
FB_IMG_16493337956968026.jpg
 
kweli dunia imekwisha!!
yaani muumini wa kanisa unalalamika kutoa sadaka?!
hujui umuhimu wa sadaka kwako binafsi na kwa familia yako?!

Elimu inahitajika juu ya Kutoa Sadaka ktk nyumba za ibada.
 
Nilijuwa watetezi hamuwezi kukosekana, hebu nieleze tu miradi ya kanisa katoliki ina faida gani kwa kanisa? Na ile benki yetu ya Mkombozi inalifaidisha vipi kanisa?

Kwani huko nyuma tuliweza vipi kujenga makanisa na mashule kwa sadaka za kawaida bila huu uharamia mpya ulioingia? Ni nini kilichobadirika?

Sisi parokia yetu ilikuwa na vigango vitatu na vyote vimekuwa parokia sasa zenye makanisa makubwa tu, tuliwezaje hayo kwa mwendo wa kawaida bila watu kunung'unika na leo kimebadirika nini?
Kwa ufupi tu, wanapojenga kitegauchumi maanake wanataka kuondokana na michango kutoka kwa waumini, hiyo michango sio ya uhakika sana kama faida itokayo bank, shule, hospital nk
 
Religion is an opium for the poor , you are far better off without it
 
Toa ndugu toa ndugu..ulichonacho..halafu unataka usitoe hilo kanisa litapelekaje injili..unataka usitoe hilo kanisa litalipaje wahudumu..unataka usitoe hilo kanisa litalipaje bills tofauti kama umeme na maji...unataka usitoe hilo kanisa litafanyeje logistics mbali mbali...unataka usitoe maintaince na repairs ya vifaa na miundombinu mbalimbali utatoa wewe.??

Acha kulalamika sana kama huna hela kaa kutulia

Uzuri hujalazimishwa..ila mkristo wa kweli hawezi kuona kama ni wizi mana hayo ndio mahitaji muhimu ya kuendesha taasisi.

Kingine kutoa ni upendo..kiwango itachojaliwa kutoa kinatosha sana.

Kama unaona hufiti nenda huko ambako hawatoi sadaka..hakuna aliyekushikiria unabaki kanisani.

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote.

#MaendeleoHayanaChama
Kwani mkisema sadaka ya maintenance ya kanisa kuna shida gani?
Umesikia jamaa anasema bahasha kila mwezi ya wanandoa na watoto hii ya nini ya kua mkristu tu?
Hapo kuna sadaka ya kwanza na pili kanisani kuna michango ya kwenye jumuiiya mengi tu bado mtu lazima utoe zaka,
Hapo bado kanisa lina miradi kama frame, ukumbi, hospitali,shule,.
Na umechangia ujenzi wa hio miradi,
Sijui unaongea hivo uko kwenye level gani lakini naweza sema 50-60% ya wakatoliki hawatoi hizo pesa kwa kuridhika au moyo mkunjufu wanaumia ila tu hakuna namna
Jaribu kuwasoma waumini utalijua hili.

Ni wakati wa kusema huna kama huna kweli, Na usiache kwenda kanisani bali unaishi maisha ya ukweli ya ukristu.
 
Kwa ufupi tu, wanapojenga kitegauchumi maanake wanataka kuondokana na michango kutoka kwa waumini, hiyo michango sio ya uhakika sana kama faida itokayo bank, shule, hospital nk
Hakuna taasisi yeyote ya kidini inayotufikia kanisa katiliki kwa investment lakini mbona hali inazidi kuwa mbaya?

Wale waislamu wa madhehebu ya Ismailia chini ya kiongozi wao mtukufu Agha Khan ndio wamiliki wa Agha Khan hospital, shule za Agha Khan na Diamond trust bank kama sikosei ni tayari kusahihishwa, lakini wenzetu hawa wananufaika na hivi vitu vinavyomilikiwa na taasisi zao.

Mimi swali langu linabaki palepale, investment zote hizi mkatoliki ananufaika vipi?
 
11 Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika.
Warumi 10:11

14 Basi wamwiteje yeye wasiyemwamini? Tena wamwaminije yeye wasiyemsikia? Tena wamsikieje pasipo mhubiri?
Warumi 10:14

15 Tena wahubirije, wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema!
Warumi 10:15

17 Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.
Warumi 10:17

Mafungu haya kwa mkristo yanampa WAJIBU .
Wajibu wa kupeleka injili ili watu WAMUAMINI

Ni lazima wahubiri WAPELEKWE.
Wataenda
1. Nauli ili kuwafikisha
2. Na vifaa vya kufanyia kazi
Biblia, vyombo vya sauti , machapisho, n.k
3. Watahitaji chakula na mahali pa kulala.
Hivi vyote na vingine vinahitaji pesa kupitia michango mbali mbali akina baba wajichange, watoto na wa mama. Lkn watoe kadri WALIVYOJALIWA wasitoe nje ya uwezo wao, bali watoe kwa moyo wa kupenda.

Kuweka viwango huenda ni kutafuta bajeti lkn sio kufungia mtu kutoa alichobarikiwa.

Kumfungia mtu huduma kwa kuwa HAJATOA ni roho ya KIPAGANI na USHETANI. Hili huenda ndio TATIZO wala si watoaji.

Kumdai mtu kitu asicho nacho ni kufuru, maana awapaye watu RIZIKI ni MUNGU.

Asalaam aleikum
 
Back
Top Bottom