Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Waumini wa makanisa wanakamuliwa sio poa, Ila kwa vile ni ridhaa yao hakuna shida kabisa.

*Kujenga makanisa ni kazi ya waumini.
*Kujenga mashule.
*Kujenga hospitali/vituo vya afya/dispensary ni kazi ya waumini.
*Kujenga nyumba za watendakazi wa makanisa.
*Kuwanunulia magari huku sisi tukipiga mihuri.

Bado tutoe zaka na sadaka kwa uaminifu.

Sisi tunapata nini?
*Tunawapeleka watoto wetu kwenye shule tulizojenga wenyewe na ada tunalipa sawa na wengine.

Anyways, mimi siendi kanisani Ila nikipigiwa simu ya kuchangia kitu natoa tu, nilipatwa na msiba hawakunibagua, labda kwa vile hivyo vimchango nashiriki.
 
Uzuri wake ni kuwa usipotoa si kosa la jinai.
[qoute]na wasiokuwa na pesa za kuamka kwenye mabenchi mara saba kutowa hizo sadaka hawatojisikia vizuri na wataacha kuja kanisani kwa kuteswa kihisa kila watu wakiinuliwa kwenye mabenchi wao hawana kitu.[/quote]
Ni heri jamii inayopata kusikia neno la Mungu walau kwa uchache kuliko ile isiyosikia kabisa.
 
Hiyo mbona imefika kwa kuchelewa sana kanisani kwenu

Muda wa sadaka pastor akafungua kapu na kuruhusu watu watoe sadaka, zoezi lilipo kamilika akaja na ajenda nyingine ya mchango kwa ajili ya mradi wa kanisa wa mashine ya alizeti

Pastor kama kawaida na safari hii akawa anawaimbia na pambio ya kuwa motivate huku akiweka kapu jingine kwa ajili ya mchango wa huo mradi

Zoezi lilipokamika pastor akaja na agenda ingine kuwa leo hapo kanisani wametembelewa na mtoto wa miaka 7 anayesumbuliwa moyo, hivyo anahitaji msaada. Akatoa kapu jingine

Hapo ndio nikaona kuanzia waumini mpaka pastor wote hawana akili, nikajiuliza hizi pesa za sadaka si huwa tunaaminishwa kuwa zinaenda kusaidia watoto yatima na wagonjwa?

Imekuwaje leo mtoto mdogo huyu mgonjwa amekuja hapa halafu kanisa limeshindwa kumpatia sadaka ambazo ndio dedicated kwa ajili ya watu wa namna hiyo?

Mtoto alipata mchango wa 30,000 kwenye kanisa lenye waumini 300 kwa misa moja hiyo ilitokana na ulafi wa mchungaji kwasababu mchango wa matibabu ya mtoto ungeanza kabla ya sadaka watu wengi wangemchangia, ila kwakua pastor alikuwa mlafi akaona hizo pesa zote ziingie kwenye mfuko wake
 
Toa ndugu toa ndugu..ulichonacho..halafu unataka usitoe hilo kanisa litapelekaje injili..unataka usitoe hilo kanisa litalipaje wahudumu..unataka usitoe hilo kanisa litalipaje bills tofauti kama umeme na maji...unataka usitoe hilo kanisa litafanyeje logistics mbali mbali...unataka usitoe maintaince na repairs ya vifaa na miundombinu mbalimbali utatoa wewe.??

Acha kulalamika sana kama huna hela kaa kutulia

Uzuri hujalazimishwa..ila mkristo wa kweli hawezi kuona kama ni wizi mana hayo ndio mahitaji muhimu ya kuendesha taasisi.

Kingine kutoa ni upendo..kiwango itachojaliwa kutoa kinatosha sana.

Kama unaona hufiti nenda huko ambako hawatoi sadaka..hakuna aliyekushikiria unabaki kanisani.

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote.

#MaendeleoHayanaChama
Mkuu, wewe inaelekea ni Mzee wa kamati ya kuhesabu sadaka!
Mtoa Uzi hakusema hataki kutoa Sadaka! Amelalamikia wingi wa sadaka siku hizi! Amelalamikia Kanisa limekuwa kama Pango la Wanyanganyi Yesu aliovunja me,a zao Enzi zake!
Hayo tote uliyoyasema hayakuwepo zamani?? Kanisa lilikuwa linajiendeshaje?? Sadaka ilikuwa ni hiari TU ya Mtu kutoa alicho nacho. Na Huduma za Kanisa ziko pale pale!
Kwa Nini Sasa ukikosa sadaka Moja kati ya rundo zilizopo unafungiwa Huduma za Kanisa, hubatizi ama huzikwi na Kanisa Kwa Sadaka Yako Moja kama ilivyokuwa zamani? SI ndio imegeuza Kanisa 'Pango la Wanyanganyi' anachosema Muumini??
 
Tumsifu Yesu Kristu mpendwa

Nadhani changamoto ipo kwenye ufahamu wa namna ufalme wa Mungu unavyofanya kazi. Sioni tatizo kwako wala mtizamo wako maana ninatambua unachohitaji wewe ni elimu na ufahamu wa jinsi Yesu anavyotenda kazi
Basi tutaanza na neno la Mungu ili iwe rahisi kupokea elimu hii
Tafadhali soma Mathayo 25:14-30
Nitachukuwa mstari 24-26 ili upate kuelewa ufalme wa Mungu unavyofanya kazi
24 - Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya;
25 - Basi nikaogopa, nikaenda nikaificha talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako
.
26 - Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya;

Hoja yako kwa kanisa haina tofauti sana na hadithi hii
Kwani kinachokuumiza wewe ni kanisa kuwa na michango mingi angali wewe ndio unayefanya kazi.
Naamini kama ungali fahamu vyote ulivyonavyo sio vyako sidhani kama ungelalamika. Kitu kinachotugharimu kibinadamu ni ile hali ya kuamini kwamba hii fedha/mali ni YANGU. Pasi na kufahamu yote tuliyonayo ni matokeo ya upendo wa Mungu kwako. Kibinadamu kuamini falsafa hii ni ngumu sana maana Ipo kiroho wakati tunadhani yote tuliyonayo ni matokeo ya juhudi zetu pekee yetu.
Ukisoma mstari wa 28 utaona ni nini matokeo ya ubinafsi wa mtumwa yule.
Yesu anasema duniani kuna mabwana wawili ambao ni fedha na Mungu. Utachagua mwenyewe wa kumtumikia lakini huwezi kuwatumikia wote kwa pamoja, Ukishindwa kufahamu kama vyote ni mali ya Bwana hakika itakuwa ngumu sana kuachilia yote ulionayo kwa Mungu.

Kwa kumalizia jitahidi sana kujifunza kanuni za Mungu hasa kwa kusoma neno lake ili uongeze maarifa ya kimungu kuanzia namna ya kupata fedha/mali, kutumia na kuzalisha uli usipungukiwe ukamkufuru Mungu, maana kumcha Bwana ndio chanzo maarifa na hekima. Tena Suleiman anasema bora hekima na ujipatie hekima na kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.
Mwisho kasome Hosea 4 upate kufahamu nini kinachoangamiza Imani. Usilaumu kanisa jilaumu wewe kwa kuwa gizani.

Uwe na jumapili njema ya matawi na nikutakie kwaresma njema.

Tumsifu Yesu Kristu.
 
Leo ni Jumapili ya matawi Yesu anaingia Jerusalem, lakini nikitafakari imani yangu ya ufuasi wa kristu napata mashaka makubwa sana.

To declare interest mimi nimezaliwa nimejikuta tu ni mkatoliki kwahiyo nipo hivyo mpaka leo, mahusiano yangu na Mungu naamini ni mazuri kiroho lakini mahudhurio yangu kanisani kwa miaka ya karibuni si mazuri huwa nakwenda na kuacha kwenda.

Basi mambo yasiwe mengi last Sunday nikatimba church kwenye parokia yetu mambo niliyokutana nayo huko ni ya kusikitisha na nathubutu kuita kile alichokikemea mwokozi wetu Yesu kristu kwamba wasigeuze nyumba ya baba yake kuwa pango la walanguzi, kwa hakika hicho ndicho kinachoendelea parokiani kwetu si kanisa tena bali ni pango la walanguzi.

Sisi Wakatoliki huko nyuma tulikuwa tukiwacheka Lutheran kwa utaratibu wa sadaka nyingi na bahasha nyingi kumbe sasa utaratibu huo umeingia kwa speed kubwa kwenye kanisa katoliki ibada ya misa moja sadaka mnatowa mara saba, sina hakika na parokia zingine hali ikoje.

Sasa kila mwanaparokia unapewa kadi ya kuchanga pesa ya kuwa mkatoliki mume na mke 10,000)= kwa mwezi na watoto buku mbilimbili kila mwezi hii ni nje ya sadaka harambee na michango mingine, tunakwenda wapi?

Najuwa wapo watetezi waliolewa mvinyo wa dini watatetea uharamia huu kwa utetezi ni lazima tuchangie ujenzi wa kanisa, hakuna anayekataa hilo na tumekuwa tukijitolea miaka yote kwa kiasi, lakini naamini mtu ambaye yuko free minded hawezi kutetea uharamia huu kugeuza kanisa kuwa pango la walanguzi, na wasiokuwa na pesa za kuamka kwenye mabenchi mara saba kutowa hizo sadaka hawatojisikia vizuri na wataacha kuja kanisani kwa kuteswa kihisa kila watu wakiinuliwa kwenye mabenchi wao hawana kitu.

Hiyo sasa tisa kumi ni hawa jamaa zetu born again, nipo hapa nyumbani namsikiliza mtumishi wa Mungu akitangaza viwango vya sadaka ya kugombowa uzao wa kwanza ni laki mbili, uzao wa pili laki na na nusu, uzao wa tatu laki.

Kutokana na uharamia huu na unyang'anyi unaoendelea kupitia mwamvuli wa dini serikali haiwezi kusaidia lolote katika hili kwa sababu ni partners muhimu in crime.

Kwakuwa waislamu wanajitambuwa sana katika hili ni wakati sasa kwa wakristu wote kuamka na kupinga dhulma hii ambayo cha kusikitisha sasa imeingia radmi kanisa katoliki na hakuna hata mkatoliki mmoja aliwahi kuhoji miradi yote ya kanisa hadi mkombozi bank ipo kwa faida ya nani na inalisaidia vipi kanisa?

Tumsifu Yesu kristu.
Yaani wewe na mimi ni mapacha mkuu. Nikienda kanisani mara 1 kwa miaka miwili, basi stimu inakata kwa ninayoyakuta huko. Nimeishia kuwa nasali tu home, nafunga pale inaponibidi (Kama Niko na maombi critical.
 
Leo ni Jumapili ya matawi Yesu anaingia Jerusalem, lakini nikitafakari imani yangu ya ufuasi wa kristu napata mashaka makubwa sana.

To declare interest mimi nimezaliwa nimejikuta tu ni mkatoliki kwahiyo nipo hivyo mpaka leo, mahusiano yangu na Mungu naamini ni mazuri kiroho lakini mahudhurio yangu kanisani kwa miaka ya karibuni si mazuri huwa nakwenda na kuacha kwenda.

Basi mambo yasiwe mengi last Sunday nikatimba church kwenye parokia yetu mambo niliyokutana nayo huko ni ya kusikitisha na nathubutu kuita kile alichokikemea mwokozi wetu Yesu kristu kwamba wasigeuze nyumba ya baba yake kuwa pango la walanguzi, kwa hakika hicho ndicho kinachoendelea parokiani kwetu si kanisa tena bali ni pango la walanguzi.

Sisi Wakatoliki huko nyuma tulikuwa tukiwacheka Lutheran kwa utaratibu wa sadaka nyingi na bahasha nyingi kumbe sasa utaratibu huo umeingia kwa speed kubwa kwenye kanisa katoliki ibada ya misa moja sadaka mnatowa mara saba, sina hakika na parokia zingine hali ikoje.

Sasa kila mwanaparokia unapewa kadi ya kuchanga pesa ya kuwa mkatoliki mume na mke 10,000)= kwa mwezi na watoto buku mbilimbili kila mwezi hii ni nje ya sadaka harambee na michango mingine, tunakwenda wapi?

Najuwa wapo watetezi waliolewa mvinyo wa dini watatetea uharamia huu kwa utetezi ni lazima tuchangie ujenzi wa kanisa, hakuna anayekataa hilo na tumekuwa tukijitolea miaka yote kwa kiasi, lakini naamini mtu ambaye yuko free minded hawezi kutetea uharamia huu kugeuza kanisa kuwa pango la walanguzi, na wasiokuwa na pesa za kuamka kwenye mabenchi mara saba kutowa hizo sadaka hawatojisikia vizuri na wataacha kuja kanisani kwa kuteswa kihisa kila watu wakiinuliwa kwenye mabenchi wao hawana kitu.

Hiyo sasa tisa kumi ni hawa jamaa zetu born again, nipo hapa nyumbani namsikiliza mtumishi wa Mungu akitangaza viwango vya sadaka ya kugombowa uzao wa kwanza ni laki mbili, uzao wa pili laki na na nusu, uzao wa tatu laki.

Kutokana na uharamia huu na unyang'anyi unaoendelea kupitia mwamvuli wa dini serikali haiwezi kusaidia lolote katika hili kwa sababu ni partners muhimu in crime.

Kwakuwa waislamu wanajitambuwa sana katika hili ni wakati sasa kwa wakristu wote kuamka na kupinga dhulma hii ambayo cha kusikitisha sasa imeingia radmi kanisa katoliki na hakuna hata mkatoliki mmoja aliwahi kuhoji miradi yote ya kanisa hadi mkombozi bank ipo kwa faida ya nani na inalisaidia vipi kanisa?

Tumsifu Yesu kristu.

Kutoa Ni hiari, hulazimishwi
 
Nimetoka kanisani kwangu Lutheran na sadaka tumetoa moja tu ndiyo utaratibu wetu.
 
Siku hizi mamilooo, usipotoa ni kosa kwani wanaangalia registaa, hivyo huduma za kikanisa kama vile ubatizo, ndoa nk haupati.

Kama ninhivyo wanakosea. Maana unamtolea Mungu sio mwanadamu.
 
Waumini hawalalamiki wakifikiri wakitoa pesa watauona ufalme wa mbingu.
Kanisa lina miradi mingi ambayo inaingiza faida kubwa, watu wanaenda kanisani kupata faraja ya Mungu na sio kufanywa kitega uchumi.
 
Back
Top Bottom