Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Leo ni Jumapili ya matawi Yesu anaingia Jerusalem, lakini nikitafakari imani yangu ya ufuasi wa kristu napata mashaka makubwa sana.

To declare interest mimi nimezaliwa nimejikuta tu ni mkatoliki kwahiyo nipo hivyo mpaka leo, mahusiano yangu na Mungu naamini ni mazuri kiroho lakini mahudhurio yangu kanisani kwa miaka ya karibuni si mazuri huwa nakwenda na kuacha kwenda.

Basi mambo yasiwe mengi last Sunday nikatimba church kwenye parokia yetu mambo niliyokutana nayo huko ni ya kusikitisha na nathubutu kuita kile alichokikemea mwokozi wetu Yesu kristu kwamba wasigeuze nyumba ya baba yake kuwa pango la walanguzi, kwa hakika hicho ndicho kinachoendelea parokiani kwetu si kanisa tena bali ni pango la walanguzi.

Sisi Wakatoliki huko nyuma tulikuwa tukiwacheka Lutheran kwa utaratibu wa sadaka nyingi na bahasha nyingi kumbe sasa utaratibu huo umeingia kwa speed kubwa kwenye kanisa katoliki ibada ya misa moja sadaka mnatowa mara saba, sina hakika na parokia zingine hali ikoje.

Sasa kila mwanaparokia unapewa kadi ya kuchanga pesa ya kuwa mkatoliki mume na mke 10,000)= kwa mwezi na watoto buku mbilimbili kila mwezi hii ni nje ya sadaka harambee na michango mingine, tunakwenda wapi?

Najuwa wapo watetezi waliolewa mvinyo wa dini watatetea uharamia huu kwa utetezi ni lazima tuchangie ujenzi wa kanisa, hakuna anayekataa hilo na tumekuwa tukijitolea miaka yote kwa kiasi, lakini naamini mtu ambaye yuko free minded hawezi kutetea uharamia huu kugeuza kanisa kuwa pango la walanguzi, na wasiokuwa na pesa za kuamka kwenye mabenchi mara saba kutowa hizo sadaka hawatojisikia vizuri na wataacha kuja kanisani kwa kuteswa kihisa kila watu wakiinuliwa kwenye mabenchi wao hawana kitu.

Hiyo sasa tisa kumi ni hawa jamaa zetu born again, nipo hapa nyumbani namsikiliza mtumishi wa Mungu akitangaza viwango vya sadaka ya kugombowa uzao wa kwanza ni laki mbili, uzao wa pili laki na na nusu, uzao wa tatu laki.

Kutokana na uharamia huu na unyang'anyi unaoendelea kupitia mwamvuli wa dini serikali haiwezi kusaidia lolote katika hili kwa sababu ni partners muhimu in crime.

Kwakuwa waislamu wanajitambuwa sana katika hili ni wakati sasa kwa wakristu wote kuamka na kupinga dhulma hii ambayo cha kusikitisha sasa imeingia radmi kanisa katoliki na hakuna hata mkatoliki mmoja aliwahi kuhoji miradi yote ya kanisa hadi mkombozi bank ipo kwa faida ya nani na inalisaidia vipi kanisa?

Tumsifu Yesu kristu.
Usipotoa sadaka na michango hilo kanisa lako litajiendesha je?.
Achen kulalamika na kuweka excuse nyingi kumtumikia Mungu.
Naomba usome:-
1Yohana 2:19;
Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu. Maana kama wangalikuwa wa kwetu, wangalikaa pamoja nasi. Lakini walitoka ili wafunuliwe kwamba si wote walio wa kwetu.
Jambo kubwa nikuacha kulalamika maana hutapata dhawabu yoyote.
Leo hii watu wanawanyenyekea wanasiasa kuliko watumish wa Mungu maana wanasiasa wana connection nyingi.
Kama unaona utumishi ni mzigo acha kuabudu
 
Tena usijaribu kuzungumzia kuhusu swala la miradi ya kanisa. Miradi mingi imajaa upigaji mkubwa sana. Watu wanatumia sadaka za waumini kujineemesha kupitia kamati za fedha na miradi kanisani.
Una Elimu kiasi gani kuhusu usimamizi na uendeshaji wa miradi??.
NAjua utabisha kwa sababu unatetea kanisa lako.

Ila Uhishahidi upo wa kutosha kama utahitaji.
 
Tena usijaribu kuzungumzia kuhusu swala la miradi ya kanisa. Miradi mingi imajaa upigaji mkubwa sana. Watu wanatumia sadaka za waumini kujineemesha kupitia kamati za fedha na miradi kanisani. NAjua utabisha kwa sababu unatetea kanisa lako.

Ila Uhishahidi upo wa kutosha kama utahitaji.
Sasa si uuweke hapa huo ushahidi, shida iko wapi??.
 
Kwa hiyo huyu alitaka Wakatoliki wawe wanagawiwa pesa kutokana na miradi hiyo??.
Hivi wewe mbona una andika ujinga?
Jibu swali!
Miradi ya kanisa Katoliki inawasaidia vipi waumini?
Kama haifai kuwagaia pesa kwanini kuwachangisha ili kuanzisha hiyo miradi?
Kanisa limekuwa taasisi ya wizi, inayotaka kuvuna isikopanda.
 
Katekista!!! Acha kupotosha ukweli. Misa takatifu katika ibada ya mazishi iliendeshwa na mpakwa mafuta.
Mzee Kwanini tuandikie mate wakati wino upo??,Ingia YouTube angalia mazishi ya Mzee Kingunge yalivyokuwa.
 
Sina elimu yoyote, kwa akili yangu tu inatosha kusema uwekezaji wa kanisa huendeshwa kwa gharama za waumini ambao hawagusi faida…. wao ni kuchanga tu na faida hairudi kwao.
Basi nikushauri tu kuwa si busara hata kidogo kuongea juu ya Jambo fulani ikiwa hujawahi kufanya research yoyote na huna ushahidi.
 
Mdau anauliza, mbona zamani haikuwa hivyo? Kuna bills na huduma gani zinazofanya kuwe na utitiri wa sadaka na matoleo mengi tofauti na zamani?
Zamani makanisa ya afrika yalikua yanapokea misaada sana kutoka ulaya na marekani kwa sasa misada hiyo imepungua sana..hivyo makanisa yanajitagemea.

#MaendeleoHayanaChama
 
Siku hizi mapadre wamekuwa sio watumishi wa wakristu bali watumikiwa.
Najiuliza kwa hizi anasa wanazoendekeza zinazonyonya waumini kama wale wamisionari waliokuja kuinjilisha wangekuwa hivi ukristo ungeishia huko huko ulaya.

Natoa mfano mmoja, mimi ninasali kanisa katoliki Kinyerezi (parokia ya Mt Bonaventura)
Hii parokia ina nyumba nzuri ya mapadre ambayo tuliinunua kwa majirani waliozunguka kanisa, mapadre wameishi hapo si zaidi ya miaka 6.
Ni nyumba nzuri ya kisasa kabisa.

Ajabu ni kwamba wametangaza inabidi tuchange ili mapadre wajengewe nyumba ya ghorofa. Yani ile ya chini pamoja na uzuri wake wanaona sio hadhi yao.
Waumini tunaotakiwa kuchanga wengine hatuna nyumba, au nyumba zetu mbovu mbovu, lakini tukamuliwe ili padre aishi ghorofani.
Hilo nimeapa sitachanga na niko tayari ku mchallenge paroko directly
Kwani wamesema usipotoa watakufungilia mashitaka??.
 
F*#ck that!
Mie nilishasema nikifa hata manispaa ikinizika hamna shida. I don't care. BTW, Roman Catholic wana double standards sana katikaa hili.
Rejea kifo cha mzee kingunge ambaye aliasi kwenda kanisani kwa muda mrefu lakini at his funeral alizikwa kikanisa.
Eti? Kwani kabla ya kuletewa hizi dini kwenye ngalawa watu walikuwa hawazikwi?
 
F*#ck that!
Mie nilishasema nikifa hata manispaa ikinizika hamna shida. I don't care. BTW, Roman Catholic wana double standards sana katikaa hili.
Rejea kifo cha mzee kingunge ambaye aliasi kwenda kanisani kwa muda mrefu lakini at his funeral alizikwa kikanisa.
Eti? Kwani kabla ya kuletewa hizi dini kwenye ngalawa watu walikuwa hawazikwi?
 
Acha uongo bhana!!.Kingunge alizikwa na Katekista,wala hakukuwa na Misa napo ni kwa vile tu familia yake ilikuwa mshirika mzuri,pia dakika za mwisho alionyesha kutaka kumrudia MUNGU lkn bahati mbaya hakuwa ametubu.
Nipe ufafanuzi kwa nini unasema alizikwa na Katekesta ila hakukuwa na Misa...?
 
Hii kitu ni kama makanisa ya hizi taasisi yamegeza kwa hawa born again mega churches. Now wote somo ni moja. Toa toa toa toa toa toa hata mahuburi ya kuacha dhambi au kuiona pepo ni 5% @ and 95% Ni TOA TOA TOA TOA na kama hutoi hatuhudumii.
 
Back
Top Bottom