Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

1 Wakorintho 7:32-35
32 - Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;
33 - bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe.
34 - Tena iko tofauti hii kati ya mke na mwanamwali. Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana, apate kuwa mtakatifu mwili na roho. Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mumewe.
35 - Nasema hayo niwafaidie, si kwamba niwategee tanzi, bali kwa ajili ya vile vipendezavyo, tena mpate kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine.


Mathayo 19:10-12
10 - wanafunzi wake wakamwambia, mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.
11 - Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa.
12 - Maana wako matowashi waliozaliwa hali hiyo toka matumboni mwa mama zao; tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi;
tena wako matowashi waliojifanya kuwa matowashi kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea neno hili, na alipokee.
Ni kwa nini vifungu vya Biblia unavyonukuu wewe uone ndio sahihi na mimi nimekuwekea verse moja tu ya Timotheo unataka kuaminisha umma wa JF kwamba hiyo siyo biblia?

Au tukubaliane kwamba Biblia ni magumashi inajipinga yenyewe?

Namuarika Kiranga sasa.
 
Toa ndugu toa ndugu..ulichonacho..halafu unataka usitoe hilo kanisa litapelekaje injili..unataka usitoe hilo kanisa litalipaje wahudumu..unataka usitoe hilo kanisa litalipaje bills tofauti kama umeme na maji...unataka usitoe hilo kanisa litafanyeje logistics mbali mbali...unataka usitoe maintaince na repairs ya vifaa na miundombinu mbalimbali utatoa wewe.??

Acha kulalamika sana kama huna hela kaa kutulia

Uzuri hujalazimishwa..ila mkristo wa kweli hawezi kuona kama ni wizi mana hayo ndio mahitaji muhimu ya kuendesha taasisi.

Kingine kutoa ni upendo..kiwango itachojaliwa kutoa kinatosha sana.

Kama unaona hufiti nenda huko ambako hawatoi sadaka..hakuna aliyekushikiria unabaki kanisani.

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote.

#MaendeleoHayanaChama
Jinga kabisa wewe
 
Mkuu, hata ukitoa unaweza usipewe huduma vilevile!

Mimi mama yangu mzazi alikua kiongozi wa jumuia huko kijijini na alikua mtoa sadaka asie na kifani, shughuli zote za ujenzi wa kanisa alishiriki kikamilifu kwa maisha yake yote mpaka amezeeka.

Bahati mbaya akaja kupata tatizo la kiafya ambalo limemuweka kitandani zaidi ya miaka 10 sasa. Cha ajabu eti kila mwaka analetewa bahasha ya zaka na kanisa linatishia kwamba akifa halitamzika kama sisi watoto hatutakua tunatoa hela za kwetu na zake!

Sasa mimi najiuliza, mtu ambae amelala kitandani hilo fungu la 10 analitoa wapi? Tangu amelala kitandani, kanisa limemsaidia vipi? Michango yote aliyochanga tangu akiwa binti mdogo mpaka sasa ni mzee, haijatosha tu? Ni mpaka tone la mwisho??
Poleni sana
 
Leo ni Jumapili ya matawi Yesu anaingia Jerusalem, lakini nikitafakari imani yangu ya ufuasi wa kristu napata mashaka makubwa sana.

To declare interest mimi nimezaliwa nimejikuta tu ni mkatoliki kwahiyo nipo hivyo mpaka leo, mahusiano yangu na Mungu naamini ni mazuri kiroho lakini mahudhurio yangu kanisani kwa miaka ya karibuni si mazuri huwa nakwenda na kuacha kwenda.

Basi mambo yasiwe mengi last Sunday nikatimba church kwenye parokia yetu mambo niliyokutana nayo huko ni ya kusikitisha na nathubutu kuita kile alichokikemea mwokozi wetu Yesu kristu kwamba wasigeuze nyumba ya baba yake kuwa pango la walanguzi, kwa hakika hicho ndicho kinachoendelea parokiani kwetu si kanisa tena bali ni pango la walanguzi.

Sisi Wakatoliki huko nyuma tulikuwa tukiwacheka Lutheran kwa utaratibu wa sadaka nyingi na bahasha nyingi kumbe sasa utaratibu huo umeingia kwa speed kubwa kwenye kanisa katoliki ibada ya misa moja sadaka mnatowa mara saba, sina hakika na parokia zingine hali ikoje.

Sasa kila mwanaparokia unapewa kadi ya kuchanga pesa ya kuwa mkatoliki mume na mke 10,000)= kwa mwezi na watoto buku mbilimbili kila mwezi hii ni nje ya sadaka harambee na michango mingine, tunakwenda wapi?

Najuwa wapo watetezi waliolewa mvinyo wa dini watatetea uharamia huu kwa utetezi ni lazima tuchangie ujenzi wa kanisa, hakuna anayekataa hilo na tumekuwa tukijitolea miaka yote kwa kiasi, lakini naamini mtu ambaye yuko free minded hawezi kutetea uharamia huu kugeuza kanisa kuwa pango la walanguzi, na wasiokuwa na pesa za kuamka kwenye mabenchi mara saba kutowa hizo sadaka hawatojisikia vizuri na wataacha kuja kanisani kwa kuteswa kihisa kila watu wakiinuliwa kwenye mabenchi wao hawana kitu.

Hiyo sasa tisa kumi ni hawa jamaa zetu born again, nipo hapa nyumbani namsikiliza mtumishi wa Mungu akitangaza viwango vya sadaka ya kugombowa uzao wa kwanza ni laki mbili, uzao wa pili laki na na nusu, uzao wa tatu laki.

Kutokana na uharamia huu na unyang'anyi unaoendelea kupitia mwamvuli wa dini serikali haiwezi kusaidia lolote katika hili kwa sababu ni partners muhimu in crime.

Kwakuwa waislamu wanajitambuwa sana katika hili ni wakati sasa kwa wakristu wote kuamka na kupinga dhulma hii ambayo cha kusikitisha sasa imeingia radmi kanisa katoliki na hakuna hata mkatoliki mmoja aliwahi kuhoji miradi yote ya kanisa hadi mkombozi bank ipo kwa faida ya nani na inalisaidia vipi kanisa?

Tumsifu Yesu kristu.
Upigaji umeingia sehemu nyingi Sana.Mimi mtanisamehe nilishachaga kwenda kanisani.

Nimekuwa mkristo mfu.
 
Nipe ufafanuzi kwa nini unasema alizikwa na Katekesta ila hakukuwa na Misa...?
Mzee Misa huongozwa na Wapakwa mafuta tu, yaani Padre au Askofu.Akiongoza Katekista hiyo sio misa bali ni Ibada tu.Ili iitwe misa lazima iwe na sehemu kuu mbili yaani Liturujia ya Neno na Liturujia ya Ekaristi Takatifu,sasa Mwenye mamlaka ya kuadhimisha sehemu zote Liturujia hizi mbili ni padre au Askofu, Kumbe Katekista yeye anaadhimisha tu sehemu ya Liturujia ya Neno, hawezi kuadhimisha Liturujia ya Ekaristi Takatifu.
 
🇹🇿Waumini wanaongezeka kwa kasi ya exponential function

🇹🇿 Kila makao mapya yanapoibuka sehemu yanakusanya wakristu wengi hivyo lazima nyumba za ibada zijengwe

🇹🇿 Vilivyokuwa vigango vinapanda hadhi ya kuwa parokia hivyo lazima miundombinu ya kiparokia ijengwe

🇹🇿 Zamani tulitegemea misaada ya wazungu kujenga makanisa lakini sasa tunasimama wenyewe

🇹🇿 Sisi hatutegemei matajiri wamepiga fedha zao kwenye biashara halafu waje wajitakase kwa kutujengea nyumba za ibada

🇹🇿Sisi hatutegemei nyumba zilizoachwa wakfu

🇹🇿Hivyo michango ni zoezi la mpaka kufa utawaacha wengine waendelee na haimaanishi usipo changa utakuwa na utajiri au ukichanga utafilisika hapana
Umepuyanga sana ndugu, hakuna sehemu nimepinga sadaka wala michango kanisani.

Rudi post namba nilichoandika utaelewa napinga nini.

Kwa taarifa yako parokia yetu ina miaka 40 na mimi ni ministrant wa kwanza wa parokia na tumezaa parokia tatu, mimi siyo intruder naandika ninachokijuwa ma nimekulia kanisani lakini siyo kanisa hili la leo.

Mhadhama Polycaply Cardinal Pengo akiwa ndio Askofu wetu mkuu wa jimbo kuu la Dsm alikuwa akiwa na shida ya pesa ya matumizi alikuwa akituomba jimbo zima kila mwana kaya amchangie pesa ya matumizi sh 100 tu, ambayo ukijumlisha wana kaya wote wa jimbo kuu la Dsm alikuwa anapata tsh million 400 cash. Je ni nani wa kumnung'unia Kadinali Pengo kwa kuomba achangiwe tsh 100 tu?

Msidhani hatuna akili, sasa ukiacha Charismatic ambao mliwapinga, subiri movement za UAMSHo ndani ya kanisa katoliki kuwakombowa mazezeta wasiojielewa wanaodanganywa na kauli mbiu ya Vaticano kwa Roma ikiongea ni Finito causa.

UAMSHO unakuja zaidi ya ule wa kina sheikh Farid.
 
Walutheri wanazo sadaka nyingi Ni kweli, ila Cha ajabu wanazidi kukusanya washarika kila uchao na kwa huduma za kiimani na kiroho katoliki hamuwafikii hata robo,,
 
Ukifa hawakuziki. Hapo ndipo wametushika pabaya
Mkuu Aikambee; Hivi bro, ulishaona mtu amekufa halafu akaacha kuzikwa??? Ukisha RIP watu bila kujali urembo wa nje eti uzikwe na Padri, Shemasi, Katekista, Mchungaji etc.Iwepo kwaya, cjui nani, nini-UTAZIKWA TU. Watakaokuzika ni watu wenzio bila kujali imani zao. Kwani zamani (Kabla ya hizi dini)watu wakifa walikuwa hawazikwi? Ifike mahali Upatikanaji wa hizi huduma kusitumike kama fimbo ya kutuchapia! eti unamwadhibu Marehemu. Hii sio sawa.
 
Mzee Misa huongozwa na Wapakwa mafuta tu, yaani Padre au Askofu.Akiongoza Katekista hiyo sio misa bali ni Ibada tu.Ili iitwe misa lazima iwe na sehemu kuu mbili yaani Liturujia ya Neno na Liturujia ya Ekaristi Takatifu,sasa Mwenye mamlaka ya kuadhimisha sehemu zote Liturujia hizi mbili ni padre au Askofu, Kumbe Katekista yeye anaadhimisha tu sehemu ya Liturujia ya Neno, hawezi kuadhimisha Liturujia ya Ekaristi Takatifu.
Shukurani kwa ufafanuzi.....Ni Marehemu wa aina gani anastahili kuongozwa na Padri ama Askofu, na huyu anaeongozwa na Katekesta sifa zake ni zipi.?
 
Upigaji umeingia sehemu nyingi Sana.Mimi mtanisamehe nilishachaga kwenda kanisani.

Nimekuwa mkristo mfu.
Sawa,baki hivyo hivyo,na uwaambie na ndugu zako wote kuwa siku ukifariki wasiwasumbue Watumishi wa MUNGU kuja kukufanyia ibada ya mazishi.Maana watu km nyie huwa mnakuja kuleta shida mkiwa mmefariki na Ndugu zenu wanaanza kulilaumu Kanisa kuwa halipo fair Kumbe ninyi wenyewe mlijichagulia kuishi pasipo kuwa na mahusiano mema na MUNGU,kwa kujitenga na Kanisa (Excommunication).
 
Badili heading mkuu usijumuishe au usisemee makanisa yote. Andika kuna kitu hakipo sawa kanisa la RC.
Umewahi kujiuliza kwanini hakukuwa na michango miaka ya nyuma na sasa IPO?
 
Siku hizi mapadre wamekuwa sio watumishi wa wakristu bali watumikiwa.
Najiuliza kwa hizi anasa wanazoendekeza zinazonyonya waumini kama wale wamisionari waliokuja kuinjilisha wangekuwa hivi ukristo ungeishia huko huko ulaya.

Natoa mfano mmoja, mimi ninasali kanisa katoliki Kinyerezi (parokia ya Mt Bonaventura)
Hii parokia ina nyumba nzuri ya mapadre ambayo tuliinunua kwa majirani waliozunguka kanisa, mapadre wameishi hapo si zaidi ya miaka 6.
Ni nyumba nzuri ya kisasa kabisa.

Ajabu ni kwamba wametangaza inabidi tuchange ili mapadre wajengewe nyumba ya ghorofa. Yani ile ya chini pamoja na uzuri wake wanaona sio hadhi yao.
Waumini tunaotakiwa kuchanga wengine hatuna nyumba, au nyumba zetu mbovu mbovu, lakini tukamuliwe ili padre aishi ghorofani.
Hilo nimeapa sitachanga na niko tayari ku mchallenge paroko directly
Mkuu ukitaka kujuwa mimi ni mkatoliki kindakindaki ni kwamba Kinyerezi kilikuwa ni kigango cha kanisa la Parokia ya Segerea na hiyo nyumba ni ya kisasa na imenunuliwa kwa Tsh million 400 kutoka kwa mwanaparokia wa hapohapo kinyerezi.

Watu wasidhani tunaandika hapa kuchangamsha baraza, ni kwamba imetosha hatuwezi tena kukubaliana na uhuni huu eti kisa kuna wapakwa mafuta amesema abcd.
 
Mzee Misa huongozwa na Wapakwa mafuta tu, yaani Padre au Askofu.Akiongoza Katekista hiyo sio misa bali ni Ibada tu.Ili iitwe misa lazima iwe na sehemu kuu mbili yaani Liturujia ya Neno na Liturujia ya Ekaristi Takatifu,sasa Mwenye mamlaka ya kuadhimisha sehemu zote Liturujia hizi mbili ni padre au Askofu, Kumbe Katekista yeye anaadhimisha tu sehemu ya Liturujia ya Neno, hawezi kuadhimisha Liturujia ya Ekaristi Takatifu.
Padre au Askofu wote wametumwa fedha
 
Mkuu ukitaka kujuwa mimi ni mkatoliki kindakindaki ni kwamba Kinyerezi kilikuwa ni kigango cha kanisa la Parokia ya Segerea na hiyo nyumba ni ya kisasa na imenunuliwa kwa Tsh million 400 kutoka kwa mwanaparokia wa hapohapo kinyerezi.

Watu wasidhani tunaandika hapa kuchangamsha baraza, ni kwamba imetosha hatuwezi tena kukubaliana na uhuni huu eti kisa kuna wapakwa mafuta amesema abcd.
Upo sahihi kabisa mkuu, imagine ile nyumba eti haina hadhi ya padre kuishi
Nadhani wanataka waipate pepo hapa hapa
 
Wakati unatusifia Waislamu, sisi huku wenyewe tunatamani tungekuwa na moyo wa kutoa sadaka kama wenu.

Sisi ni changamoto watu wazito kutoa sadaka, madrasa na misikiti mingi inahitaji ukarabati na shule pia. Ila watu wetu wazito mno wa kutoa sadaka. Sadaka mpaka zitokee kwa waarabu ndio madrasa zijengwe
Pandikizi!
 
Kwani wamesema usipotoa watakufungilia mashitaka??.
Hakuna mashtaka lakini unapata restrictions ktk huduma.
Haya mambo yakiachwa yaendelee tunazidi kuwapa umungu wasioustahili

Walianza na kutokuwapa huduma za ndoa, ubatizo nk wale wasiochangia, wakaja na kukataa kutoa ibada ya maziko, tukinyamaza kesho itakuwa unaingia ibadani kwa ID
 
Mzee Kwanini tuandikie mate wakati wino upo??,Ingia YouTube angalia mazishi ya Mzee Kingunge yalivyokuwa.

Nipe ufafanuzi kwa nini unasema alizikwa na Katekesta ila hakukuwa na Misa...?
Kwa ninavyojuwa mimi ibada ya misa ya mazishi ikishafanyika kanisani na kuongozwa na Padre si kazima Padre kwenda makaburini, ni katekista anaachiwa hilo jukumu.

Labda mwambie akujibu swali hili ni kwa nini watu wengine hawakuishi maisha yoyote ya utakatifu lakini wanazikwa na Askofu na siyo Padre?

Ikumbukwe Askofu ndio daraja la juu kabisa katika kanisa kuliko Kadinali, ingawa makadinali wengi ni maadkofu ila hata Padre au Shemasi anaweza kuteuliwa kuwa Kadinali kwa mujibu wa canon law na imeshatokea Padre Ujerumani aliteuliwa kuwa kadinali lakini siyo Askofu, anakuwa tu ni mjumbe wa Conclave kumchaguwa Papa inapotokea uchaguzi wa Papa mpya.
 
Back
Top Bottom