Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Duuh, pole mkuu ila kiukweli kwa miaka ya karibuni,katoliki kuna shida nyingi sana,lakini kwa vile waumini haturusiwi kuhoji basi mambo yanakwenda kama yalivyopangwa,michango imekua mingi kupitiliza,zamani mtu anajivunia kuwa mkatoliki kutokana kutokana na jinsi kanisa linavyoendeshwa.

Hili nina uhakika wakatoriki wengi hatupo vizuri katika kuichambua na kuijua biblia, that's why tunapokuwa hata ktk mijadala ya kidini huwa hatuna majibu kwasababu hatusomi na kuijua biblia, viongozi wa kanisa huwa wamejikita ktk michango ambayo mingine sio muhimu kabisa.

Mnaweza mkatumia miaka minne kujenga kanisa,likiisha mtaambiwa mnunue gari la padri [emoji2],kapu la mama,mambo ni mengi
[emoji1][emoji1][emoji1]Dini zote hawakupi mwanya wa kuhoji. Yaani mtu mmoja aliyejipa utumishi akisema kasema. And this is how religion was brought to Africa by missionaries to silence any spirit of consciousness. Times have changed na watu wanaanza kuquestion.
 
Siku moja nimemtembelea mzee wangu nilipofika akaniambia anadaiwa elfu hamsini kanisani kwa ajili ya harambee.Akanieleza kuwa kila jumuiya imepangiwa kiasi flani cha fedha ambazo zimegawanywa kwa kila nyumba.Mzee wang anakaribia miaka 80..Na alinieleza kuwa siku ya harambee kila familia wanakuwa wanasomwa kanisani mnapita mbele kwenda kukabidhi hicho kiasi cha fedha na kama huna lazima utoe sababu za maana hapo na linakuwa deni mpaka ulilipe. Mambo yamekuwa magumu mno siku hizi.
Dini hizi aisee[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
 
Hivi ile sanamu tunayotembea nayo shingoni ni lazima kuvaa?
Hebu nikuuulize, uliwahi kujiuliza ilikuwaje wewe ukawa dhehebu ulilopo? Je ulishawahi peleleza nani alikuwa chambo mpaka ukajikuta uko humo ulipo?
 
Sisi parokia yetu imezaa parokia tatu, unaweza kuelewa machozi na damu tuliyopitia.

Tuna nyumba ya masista, tuna nyumba ya mapadri ya zamani, ikajengwa ghorofa likaja hilo ghorofa likaonekana dogo utadhani mapadre wetu ni matembo tukajenga ghorofa nyingine mpya kubwa.

Tumemnunulia paroko Prado, tuna dispensary tuna maternity tuna Ambulance tuna nursery school, kama hiyo haitoshi kuna nyumba nne jirani tumezinunuwa tumevunja ndio umeanza upuuzi eti tujenge nyumba ya mama bikira Maria.

Yani the way nilichojifunza hakuna kipindi mtaachwa mpumuwe ni kutwishana mizigo mwaka mzima.
Guys wake up! Hawa jamaa wanapenda maisha mazuri usipime. Yaani unakuta mnamnunulia padri orado wakati hata boda huna. Mzazi wako aliyekuzaa hana hata sehemu ya kuishi ila ukoradhi hata hrla ya kula usimtumie umjengee padre gorofa! Ama kweli haya maajabu ya Afrika
 
Waislamu wanajali sana muda yaani wao siku ya Ijumaa wanaingia kama saa saba na ushee lakini saa nane tu tayari walishatoka.
Halafu zile sala zao fupifupi yaani ni Kama kanu saa au dakika 20 tu hao duh.
Time management hapa wapo vizuri.
Dini zote hizi zilikuja na meli na mashua na waliua za kwetu pambaneni nazo
 
[emoji1][emoji1][emoji1]Dini zote hawakupi mwanya wa kuhoji. Yaani mtu mmoja aliyejipa utumishi akisema kasema. And this is how religion was brought to Africa by missionaries to silence any spirit of consciousness. Times have changed na watu wanaanza kuquestion.
Dogmatism
 
Nikwambie kitu, dunia hii kati ya wafia dini na wafuasi wa shetani ni wafuasi wa shetani ndio wenye mafanikio nadhani ndio huko kubalikiwa usemako.

Hii dunia uchumi mkubwa unamilikiwa na mashoga na wamebarikiwa mno.

Verse kama hizi endeleeni kuzitumia kuwalaghai maskini ili muendelee kuwapora hata hicho kidogo walichonacho.
Hayo ni maoni yako na kundi lako, maoni yasiyo na uthibitisho wowote.
Usitumie uongo kuhalalisha maovu yako na unajua fika uongo ndio silaha kubwa ya Ibilisi.
 
Mkuu kwa iyo situation ilokukuta haihitaji kufikiria mara 2 kua kanisa linakunyonya.

Sasa kma anaumwa mbona kanisa halimsaidii kitu ila wao ndo wanataka?

Laiti angekua Muislamu huyo waislamu wangejichanga wangemuhudumia badala ya yy kudaiwa huduma

Uislamu ni dini ya haki
Hao Waislamu wa wapi unaowazungumzia [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]hawahawa wa mtaani kwetu au
 
guys ! sikuzote kaa mkijua padre au mchungaji hawezi kukupeleka kwa mbingu( kama waamini mbingu). Matrndo yako ukiwa hai yatakupeleka. Hivyo basi wakuzike wasikuzike hawasaidii chochote. Hata ukizikwa na jiji poa tu
Sikubaliani na falsafa yako! Umesahau kuwa imeandikwa kuwa litakalofunguliwa duniani litafunguliwa mbinguni? Je, unajua ni mateso yepi waliobaki duniani hasa ndugu zako wanapata kwa Padre kutokuzika? Kuzikwa na Padre muhimu sana na hii haikuhusu uliyefariki bali waliobaki hai
 
Kwani usipozikwa na kanisa inakuharibia nini wewe uliyekufa??
Hata ndugu wa marehemu waliobaki hai haiwasaidii chochote. Ni basi tu tumeshafanya mazoea ya kuona umuhimu wa kuzikwa na viongozi wa dini kutokana na indoctrination yenye malengo mahususi kutoka kwa wanufaika wake.
 
Sikubaliani na falsafa yako! Umesahau kuwa imeandikwa kuwa litakalofunguliwa duniani litafunguliwa mbinguni? Je, unajua ni mateso yepi waliobaki duniani hasa ndugu zako wanapata kwa Padre kutokuzika? Kuzikwa na Padre muhimu sana na hii haikuhusu uliyefariki bali waliobaki hai
Ulishawahi kusikia wafu wawili ambao enzi za uhai wao matendo yao yalikuwa ni ya aina moja yaani kutoenda kanisani, kutotoa michango n.k. lakini kutokana na umaarufu na/au utajiri wa mmoja wao akazikwa na padri/mchungaji na mwingine akakataliwa kuzikwa na kanisa? Kwamba kwa vile la huyo mtu maarufu au tajiri "limefunguliwa duniani" hata huko mbinguni limefunguliwa kiasi kwamba na ndugu zake waliobaki hai mateso watakayopata yatapungua tofauti na mateso watakayopata ndugu wa yule asiye na umaarufu au utajiri?
 
Ulishawahi kusikia wafu wawili ambao enzi za uhai wao matendo yao yalikuwa ni ya aina moja yaani kutoenda kanisani, kutotoa michango n.k. lakini kutokana na umaarufu na/au utajiri wa mmoja wao akazikwa na padri/mchungaji na mwingine akakataliwa kuzikwa na kanisa? Kwamba kwa vile la huyo mtu maarufu au tajiri "limefunguliwa duniani" hata huko mbinguni limefunguliwa kiasi kwamba na ndugu zake waliobaki hai mateso watakayopata yatapungua?
Umeambiwa ya kaisari mwachie yeye na ya mungu mwachie mungu! Maana yake ya duniani waachie wanadamu walio hai na ya mbinguni mwachie Marehemu! Nani alikufa akarudi duniani kutusimlia? Kuzikwa na Padre ni muhimu na akikataa inaacha simanzi kwa wanaobaki hai.
 
Umeambiwa ya kaisari mwachie yeye na ya mungu mwachie mungu! Maana yake ya duniani waachie wanadamu walio hai na ya mbinguni mwachie Marehemu! Nani alikufa akarudi duniani kutusimlia? Kuzikwa na Padre ni muhimu na akikataa inaacha simanzi kwa wanaobaki hai.
Hayo ya kumwachia Kaisari badala ya kuhoji na kupata logic, hitaji la kuzikwa na padri na mengineyo mengi ndiyo indoctrination tunayozungumzia. Wanufaika walishaanda kauli za kukataza watu kuhoji sana na kujenga hofu kwanza ili wengine wabaki kufuata maelekezo tu.
 
Back
Top Bottom