Kuna Kitu Rais Samia Amekisema Kuhusu Kurejea Kizimkazi “Post 2025”. Nashauri na Nasisitiza Wenye Uwezo Kusaidia, Tumsaidie Kumshauri Ukweli!

Kuna Kitu Rais Samia Amekisema Kuhusu Kurejea Kizimkazi “Post 2025”. Nashauri na Nasisitiza Wenye Uwezo Kusaidia, Tumsaidie Kumshauri Ukweli!

Wanabodi
Hili sio bandiko la kila mtu, ni bandiko la wale tuu wenye jicho la 3 na sikio la tatu.

Leo Rais Samia, akiwahutubia maofisa ugani, Ikulu ya Chamwino, kuna kitu Rais Samia amekisema kuhusu uchaguzi mkuu wa 2025, pale aliposema atarejea lini Kizimkazi. Rais Samia ameuzungumzia uchaguzi wa 2025 not expressly but impliedly

Juzi kati nilipandisha bandiko humu nikiuliza kuhusu Wasaidizi wa Rais Samia kama wanamsaidia kwa kumwambia ukweli Wasaidizi wa Magufuli walimuogopa hadi kushindwa kumsaidia, Je Wasaidizi wa Samia wanamsaidia kwa kumweleza ukweli au nao wanamuogopa? Tumsaidie au..?

Kauli hiyo ya Rais Samia sio tuu ina maana kubwa sana kwa uchaguzi wa 2025 tuu, bali ni kauli ya uthibitisho bado kuna wasaidizi wa rais, ambao hawamwambii Rais Samia ushauri wa ukweli kuhusu mambo mbalimbali ukiwemo urais wa 2025.

Mimi ni miongoni mwa watu wanaounga mkono urais wa JMT 2025, twende na mwanamke Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye!

Nimewasisitiza watu wenye uwezo wa kusaidia, wasaidie, kwa kumshauri Rais Samia ushauri wa ukweli wa urais wa 2025.

Mimi pia ni miongoni mwa watu hao wenye uwezo wa kusaidia, na nimeisha saidia kwa kutoa ushauri wangu katika bandiko la sauti HII

Kauli hiyo inaonyesha Rais Samia tayari ameisha hakikishiwa na watu wake, kuwa 2025 rais ni yeye, hii maana yake ni rais wetu wa 2025 tayari tunaye, yupo na ameisha chaguliwa, (amechaguliwa na nani?), hivyo siku ya uchaguzi ni kumthibitisha tuu!.

Hivyo nashauri, wale wenzetu ambao ni Presidential hopefuls wa urais wa JMT kwa uchaguzi Mkuu wa 2025, nawashauri save your time and money, rais wa JMT 2025, tayari tunaye!, zoezi la upigaji kura za urais uchaguzi wa 2025, sio kumchagua rais bali kukamilisha tuu taratibu za takwa la kikatiba kuwa uchaguzi ni kila baada ya miaka 5, hivyo hata kama rais tayari tunaye, bado tutapiga tuu kura sio kumchagua rais bali kutimiza tuu takwa la kikatiba la kufanya uchaguzi kila baada ya miaka mitano hata kama uchaguzi huo sio uchaguzi, bali ni igizo tuu la uchaguzi kumthibisha tuu rais aliyepo!. Swali kama hili pia nililiuliza kabla ya uchaguzi wa 2020 Kwa kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020?

Tena nimewasikia watani zangu fulani wakisemezana kumsimamisha jembe lao, jibaba la shoka na shujaa wao, nawashauri wamsimamishe mgombea mwanamke, wanawake ndio wapambane, maana jibaba dume la shoka kushindwa na mwanamke, si ni itakuwa ni aibu sana?. Iwapo Watanzania wataamua 2025 twende na Mwanamke, mnaonaje tukiwashauri CHADEMA wasimamishe Mwanamke? Maana Mwanaume kushindwa na Mwanamke ni aibu!

Nawatakia Jumamosi Njema

Paskali
Yapo mambo yanaonekana na Kuna mambo hayaonekani. Mambo mawili makubwa yanaweza kutokea 2025. Mh Rais kukubali wosia wa wazee kuwa hakuwa ktk mnyororo wa kuwa Rais na mbele yake Kuna miba ambayo akitaka kuendelea basi akubali kuikanyaga ila maumivu yake yatakuwa makali kiasi atajisemea laiti ningesikiliza nikashuka nikapumzika. Nadharia ya pili ni conspiracy ambapo jambo lolote laweza kutokea 2025 yaani hakuna atakaye weza kuamini kama vile ilivyotokea huko USA. Bila kupepesa macho kuongoza nchi sio lelemama wala sio jambo la jinsia ukweli nikwamba utashi wakisiasa nimuhimu sana kwa kule tunaelekea. Sioni kwa uwezo wangu Mungu kanipa kama Mh Rais miaka 5 itakuwa rahisi kwake itakuwa ni miaka migumu sana kiasi anaweza kusema naomba kushuka ila ataambiwa huwezi kushuka ulisha shauriwa 2025 sasa maliza kiapo chako naogopa sana maana utakuwa usiku mzito sana. Well Sina uwakika kama majasusi ya Taifa hili kongwe yatashindwa pindua meza 2025 kuweka wanaye mtaka mambo ni mengi Muda mchache ila Mungu ibariki Tanzania na watu wake🕊️🙏
 
Mimi baada ya kuisikia hiyo kauli ya kwamba "mpaka 2028 nikijiandaa kwenda kupimzika kizimkazi "nilishituka sana inaonesha ameshahakishiwa
Tanzania Raha sana unapofikiri unajuwa nchi ndipo inakujuwa zaidi. Nikikumbuka mwamba na Urais wa Milele nachoka kabisa. Hakuna alie amini is the same 2025 hakuna atakaye amini🤐
 
Unajidanganya . Wezi wa kura ndio watakao iharibu nchi , Mbeya itakauka na kugeuka kuwa jangwa .
Narudia tena nafasi ya kuharibu Nchi Ili mkimbilie Kwa bwana zenu Ulaya haipo na hamtakuja kuipata so usipotexe mda na Nguvu na jambo ambalo huna uwezo nalo.

Mtaishia kutoa matamko kama kina Mwambukusi wa TLS 😂😂
 
Kwa hiyo Pasco unamaanisha TANGANYIKA KUPATA Uhuru Hadi 2030???!!!

Na ikitokea RAIS 2030 akawa Hussein Mwinyi au Mchengerwa maana yake WATANGANYIKA/WADANGANYIKA au MACHOGO KUPATA Uhuru Hadi 2040.
Hahahaaaa, nimecheka sana. Na zanzibar itafikia level ya mauritius, kisha watavunja muungano tuanze upya na Tanganyika yetu
 
"Wanabodi....,
...rais wa JMT 2025, tayari tunaye!, zoezi la upigaji kura za urais uchaguzi wa 2025, sio kumchagua rais bali kukamilisha tuu taratibu za takwa la kikatiba kuwa uchaguzi ni kila baada ya miaka 5, hivyo hata kama rais tayari tunaye, bado tutapiga tuu kura sio kumchagua rais bali kutimiza tuu takwa la kikatiba la kufanya uchaguzi kila baada ya miaka mitano hata kama uchaguzi huo sio uchaguzi, bali ni igizo tuu la uchaguzi kumthibisha tuu rais aliyepo"!.....
Mkuu Paskali, ukiitwa ukaambiwa uthibitishe hizi kauli zako, je utaweza?
 
Hawa ndiyo Watanzania tulionao. Kama umeandika kama kada wa chama Sina Shida na wewe. Ila kama umeandika kama mtanzania msomi na mchambuzi wa masuala ya kisiasa big shame on you. We are democratic and no body is officially sworn in yet after 2025 race. How do you dare to say that someone from hell is elected ready? Be impartial plz. Civil votes will count on 2025.
MAYALA kadiri yangu hili andiko kuandika vizuri sana, free from bias.

Amekuwa very objective, anasomesha wazi kuwa inawezekanaje mtu ajadili habari ya 2028 -2029 ?? ili Hali 2025 ni mwakani ambapo patakuwa na uchaguzi, kwa kauli ya Rais ni kwamba ana uhakika wa kushinda uchaguzi hata kabla ya uchaguzi!!

Maana nyuma yake Kuna wizi wa kura, matumizi ya vyombo vya Dora, plus watanzania wasiojitambua.

Lakini katika free and fair election, atarudi KIZIMKAZI misa ya kwanza tu.

Ni kazi ya watanzania kuamka na kuzuia kiongozi ambaye anauza maliasili, na rasilimali za Tanganyika.

Mama huyu akifaulu 2025, Urais wake utakuwa wa damu,watu kutekwa na kupotezwa,ambao watakuwa wanamkosoa.

Atakuwa anatumia rasilimali za BARA kujenga Zanzibar akishirikiana na kakake HUSSEIN.

Andiko la Paschal Mayala ni alarming sign, anatuamsha watanzania tukatae kwa matendo kauli ya Rais, kujitangaza indirect kuwa yeye atakuwa Rais 2025.🤔🤔🤔

Hii inatafakarisha sana,
Mama anakuwa kama ameagana na MUNGU ambaye ameshikilia hatima ya maisha UHAI.

Namaliza kwa kusema "ANAYELIRUKA SHIMO AMEAGANA NA NYONGA"
Cc:KIZIWI 🐸
Cc😛askal Mayala
 
Uchaguzi wa Tanzania ni sawa na WA Maduro wa Venezuela, yaani mtu anjiteua kabla hata ya uchaguzi na chaguzi hizi za maigizo it's just a waste of time and money
 
Back
Top Bottom