Kuna Kitu Rais Samia Amekisema Kuhusu Kurejea Kizimkazi “Post 2025”. Nashauri na Nasisitiza Wenye Uwezo Kusaidia, Tumsaidie Kumshauri Ukweli!

Kuna Kitu Rais Samia Amekisema Kuhusu Kurejea Kizimkazi “Post 2025”. Nashauri na Nasisitiza Wenye Uwezo Kusaidia, Tumsaidie Kumshauri Ukweli!

Mkuu shida tuliyonayo ni moja tu!
Ni kutokuwa na Tume huru ya Uchaguzi.
Maana hii ambayo tumeambiwa ni Tume huru ni Tume ya Mama ya kumsaidia kubaki hadi 2030!
Kama Uchaguzi ungekuwa huru wananchi wangeamua kwenye Sanduku la Kura.
Nje ya hapo hata ungetoa ushauri gani au hata washauri wa mama wangemwambia Ukweli au Uongo haisaidii.
 
'MIMI NI...'
Unajiona nani ndani ya taifa hili, ndugu?

Njaa tu!
Moja ya udhaifu mkubwa sana wa Watanzania, ni kutojitambua, kwa wao ni wananchi wa kawaida, wanajiona they are nothing!, kumbe hawajitambui kuwa mwananchi ndie the most important and valuable asset kwenye nchi, huyu ndiye mwenye nchi, ndiye mwenye katiba!. Rais wa nchi, na mihimili yae ya Serikali, Bunge na Mahakama, wote hawa ni watumishi wa kumtumikia mwananchi, na ni mwananchi amemuajiri Rais wa nchi kwa kura yake, na ndiye anayemlipa mshahara wake kwa kodi yake, hivyo usinidgharau kabisa mimi mwananchi wa kawaida, nina uwezo wa kumtuma chochote muajiriwa wangu, na akiharibu kazi, nina uwezo wa kumfuta kazi!. The real powers lies with the people!, ila masikini Watanzania wengi hawajitambui nguvu yao na hawajui powers zao!. Mimi najitambua na kila uchao, nashauri, na kwa taarifa yako, tunasikilizwa sana tuu!.

Kufuatia kulijua hili, na mimi nimejaaliwa kauwezo kidogo ka kutoa elimu kwa umma, kuwasaidia Watanzania wenzangu, nimejitolea kuwasaidia kuijua katiba yaa, kuujua uwezo wao, kuzijua haki zao, na kutimiza wajibu wao, kupitia makala maalum za magazeti ya Mwananchi kila Jumatano, Nipashe kila Jumapili na kipindi cha TV kila Jumapili
Na sasa tunamsaidia
View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04
Karibu na wewe tukusaidie kujitambua sio unapelekwa pelekwa kama ling'ombe
P
 
Wanabodi
Hili sio bandiko la kila mtu, ni bandiko la wale tuu wenye jicho la 3 na sikio la tatu.

Leo Rais Samia, akiwahutubia maofisa ugani, Ikulu ya Chamwino, kuna kitu Rais Samia amekisema kuhusu uchaguzi mkuu wa 2025, pale aliposema atarejea lini Kizimkazi. Rais Samia ameuzungumzia uchaguzi wa 2025 not expressly but impliedly

Juzi kati nilipandisha bandiko humu nikiuliza kuhusu Wasaidizi wa Rais Samia kama wanamsaidia kwa kumwambia ukweli Wasaidizi wa Magufuli walimuogopa hadi kushindwa kumsaidia, Je Wasaidizi wa Samia wanamsaidia kwa kumweleza ukweli au nao wanamuogopa? Tumsaidie au..?

Kauli hiyo ya Rais Samia sio tuu ina maana kubwa sana kwa uchaguzi wa 2025 tuu, bali ni kauli ya uthibitisho bado kuna wasaidizi wa rais, ambao hawamwambii Rais Samia ushauri wa ukweli kuhusu mambo mbalimbali ukiwemo urais wa 2025.

Mimi ni miongoni mwa watu wanaounga mkono urais wa JMT 2025, twende na mwanamke Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye!

Nimewasisitiza watu wenye uwezo wa kusaidia, wasaidie, kwa kumshauri Rais Samia ushauri wa ukweli wa urais wa 2025.

Mimi pia ni miongoni mwa watu hao wenye uwezo wa kusaidia, na nimeisha saidia kwa kutoa ushauri wangu kusaidia taifa langu.

Kwa upande wa CCM nimeeashauri katika bandiko la sauti HII

Na kwa upinzani pia nimewashauri Kama Upinzani unataka mafaniko ya kweli 2025, Iachane na Urais, Ujikite Serikali za Mitaa, Ubunge na Udiwani, Urais labda 2030!

Kauli hiyo inaonyesha Rais Samia tayari ameisha hakikishiwa na watu wake, kuwa 2025 rais ni yeye, hii maana yake ni rais wetu wa 2025 tayari tunaye, yupo na ameisha chaguliwa, (amechaguliwa na nani?), hivyo siku ya uchaguzi ni kumthibitisha tuu!.

Hivyo nashauri, wale wenzetu ambao ni Presidential hopefuls wa urais wa JMT kwa uchaguzi Mkuu wa 2025, nawashauri save your time and money, rais wa JMT 2025, tayari tunaye!, zoezi la upigaji kura za urais uchaguzi wa 2025, sio kumchagua rais bali kukamilisha tuu taratibu za takwa la kikatiba kuwa uchaguzi ni kila baada ya miaka 5, hivyo hata kama rais tayari tunaye, bado tutapiga tuu kura sio kumchagua rais bali kutimiza tuu takwa la kikatiba la kufanya uchaguzi kila baada ya miaka mitano hata kama uchaguzi huo sio uchaguzi, bali ni igizo tuu la uchaguzi kumthibisha tuu rais aliyepo!. Swali kama hili pia nililiuliza kabla ya uchaguzi wa 2020 Kwa kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020?

Tena nimewasikia watani zangu fulani wakisemezana kumsimamisha jembe lao, jibaba la shoka na shujaa wao, nawashauri wamsimamishe mgombea mwanamke, wanawake ndio wapambane, maana jibaba dume la shoka kushindwa na mwanamke, si ni itakuwa ni aibu sana?. Iwapo Watanzania wataamua 2025 twende na Mwanamke, mnaonaje tukiwashauri CHADEMA wasimamishe Mwanamke? Maana Mwanaume kushindwa na Mwanamke ni aibu!

Nawatakia Jumamosi Njema

Paskali
Uwe unavuta bangi isiyokuwa na mbegu
 
Unajipendekeza kishamba sana na bahati mbaya una gundu. Hopeless!
Tangu mwanzo nimesema hili sio bandiko la kila mtu, ni la watu maalum tuu wenye viwango fulani vya uelewa, kama unadhani bandiko hili ni la uchawa, inamaana bandiko hili limekuzidi kimo, umetoka kapa!.
Pole.
P
 
Walimu wa siasa wanaowafundisha viongozi wetu Wana roho ngumu sana aiseh!!
Baada ya Chuo cha Chama Kivukoni kuchukukuliwa na serikali, viongozi wetu wamekuwa hawapikwi kisiasa, upishi ndio umeanza upya sasa pale Kibaha.
Nataka niwashauri kwenye mtaala waweke topic ya karma ili kuzuia wasiliwe vichwa!.
P
 
Tangu mwanzo nimesema hili sio bandiko la kila mtu, ni la watu maalum tuu wenye viwango fulani vya uelewa, kama unadhani bandiko hili ni la uchawa, inamaana bandiko hili limekuzidi kimo, umetoka kapa!.
Pole.
P
Kwanza, hiyo fallacy ya kusema 'andiko si la kila mtu' hutumiwa na watu wenye uwezo mdogo wa kujenga hoja.
Pili, kama nilivyokueleza awali, hoja zako za MIMI NI, MIMI NI, hiyo ni mental disorder unayohitaji kuitafutia tiba.

Uchawa wako hauhitaji jicho la tatu kuung'amua. Hata mtoto wa chekechea atajua wewe mnafiki, na unajikomba ili upate teuzi tu.

Msomi hopeless wewe!
Na watu wa aina yako ndiyo mnaizamisha nchi yetu!
 
Moja ya udhaifu mkubwa sana wa Watanzania, ni kutojitambua, kwa wao ni wananchi wa kawaida, wanajiona they are nothing!, kumbe hawajitambui kuwa mwananchi ndie the most important and valuable asset kwenye nchi, huyu ndiye mwenye nchi, ndiye mwenye katiba!. Rais wa nchi, na mihimili yae ya Serikali, Bunge na Mahakama, wote hawa ni watumishi wa kumtumikia mwananchi, na ni mwananchi amemuajiri Rais wa nchi kwa kura yake, na ndiye anayemlipa mshahara wake kwa kodi yake, hivyo usinidgharau kabisa mimi mwananchi wa kawaida, nina uwezo wa kumtuma chochote muajiriwa wangu, na akiharibu kazi, nina uwezo wa kumfuta kazi!. The real powers lies with the people!, ila masikini Watanzania wengi hawajitambui nguvu yao na hawajui powers zao!. Mimi najitambua na kila uchao, nashauri, na kwa taarifa yako, tunasikilizwa sana tuu!.

Kufuatia kulijua hili, na mimi nimejaaliwa kauwezo kidogo ka kutoa elimu kwa umma, kuwasaidia Watanzania wenzangu, nimejitolea kuwasaidia kuijua katiba yaa, kuujua uwezo wao, kuzijua haki zao, na kutimiza wajibu wao, kupitia makala maalum za magazeti ya Mwananchi kila Jumatano, Nipashe kila Jumapili na kipindi cha TV kila Jumapili
Na sasa tunamsaidia
View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04
Karibu na wewe tukusaidie kujitambua sio unapelekwa pelekwa kama ling'ombe
P

Tatizo hujaelewa muktadha katika hoja yako mwenyewe.
U- MIMI unaozungumzia hapa na ulioutumia katika andiko lako, ni vitu tofauti.
Unatajataja mimi, mimi sababu unataka mamlaka za uteuzi zikuzingatie. Na hicho ndicho ninachokueleza kuwa ni mental disorder!

Wasisitize vijana wako watafute mali wangali na nguvu ili wasije wakaishi kama wewe kama muda wao wa magharibi.

Kujikweza tu!
 
Uanauke wake unatusaidia nini, tunahitaji mtu yeyote mwenye kudeliver regardless ni mwanamke au ni mwanamme msukuma au Mndali, Muislam au mkristo au asiye na dini
Huyu Pasko ana-play gender card ili aonekane mtu anayejali mambo hayo. Kimsingi anajikosha tu.
 
MIMI SIYO MCHAWI WALA MALAIKA ILA KAMA SAMIA ATAKUWA RAIS 2025 TANZANIA ITAINGIA KWENYE GIZA ZITO AMBALO TOKA NCHI YETU KUWEPO ALIJAWAI KUTOKEA ..na hilo giza litasababisha hasara kubwa sana na funzo kubwa sana ndani ya nchi yetu. Hiyo hasara ndani yake kutakuwa na damu za wanadamu wa kutosha.
labda giza kwa maana ya kidini lakini kwa lugha za kidunia umeme umeshaanza kutengamaa. SSH anafanya mengi mazuri huko mikoani kwa ujumla lakini asijiamini sana, hakuna ajuaye kesho inafanana vipi.
 
Back
Top Bottom