Kuna kitu Rwanda inachokitafuta Tanzania! (Serikali, nchi yetu ni salama kiasi gani?)


Duh!awapigie magoti kwalipi?waliomwaga damu si wamarekani au waingereza ni watoto wa kinyarwanda,nahiyo tabia ya watanzani kupigia magoti wakoloni ndio inawapa amani na kuwaacha masikini,na siku mtajaribu kusimama peke yenu mtaona jinsi mtakavyo sambaratika yani mtakua zaidi ya DRC,huo upuuzi wanyarwanda hawautaki,najua watapambana na hizo dhoruba lakini watashinda,usipokua jasili huwezi kwamua raia wako katika umasikini na ujinga.
 
Ki rwanda kidogo sana kwa tz isee .... na ni ajabu kuilinganisha israel iloshikilia dunia na hao watoto wadogo hata A hawajajua kuandika .. ni thread ya kitoto ...
 
Aisee hawa wanyarwanda noma inawezekana Kabisa TISS hawakupenda Tanzania waende Congo hii vita ni Kama ya bwana kikwete plus membe against kagame na wenzake naamini mahusiano yetu na rwanda yatakuwa mazuri baada ya 2015

Fuatilia hii story kwa makini,achana na propaganda za Kagame,masuala ya TISS ayapo kama hivyo,kuna baraza la Usalama la Taifa ndilo lenye jukumu la kumshauri Rais kwenye mambo ya kiusalama,na pia nchi aipeleki jeshi nje ya nchi kwa utashi wa Rais tu kuna vigezo vingi vinaangaliwa,ingawaje kikatiba anayo mamlaka na pia ndiye amiri jeshi mkuu
 

Nimetoa sababu 3 kwann Tanzania ina haki ya msingi kuishauri Rwanda juu ya mambo ya Usalama wa eneo la maziwa makuu.. Umepiga kelele the only thng umeishia kuongea ni wakimbizi. Sasa nakuongezea swali unataka kusema katika makambi ya wakimbizi Tanzania hakujawahi kuwekwa wakimbizi kutoka Rwanda..??
Pili em jibu zile hoja nyngne ili twende kisomi sio malumbano ya vijiweni.
 
Last edited by a moderator:
Kagame amekutuma uje kulialia ili asipigwe? Mnajisifia halafu hamna kitu.. Kagame kawaambia M23 waandike barua kwa Bunge la Tanzania eti.. Oooh msipeleke majeshi Congo hamjui vita vya msituni mtajutia uamuzi wenu... Kichapo mpaka mkakimbilia Uganda.. Na mkipigana na sisi ndani ya siku 5 mtakuwa koloni letu.
 
samahani wewe jina lako la kikazi ni nabii nani?
 
Kiongozi umenena vema, Rwanda wako vizuri sana na wana field ya kivita kwanzia jeshi hadi wananchi, sis hapa hata hao wajeda baadhi tu ndio wana field ya kivita kwa watanzania tulio weng hatujui vita ni nn, laiti cku moja Tanzania ikipaniki ikaenda kuivamia Rwanda basi naamini kabisa ile mikoa ya Kagera na Kigoma tutawasahau.
Over
 

Ndio walio mwaga damu ni Wanyarwanda Lkn mibaraka yote RPF ilipewa toka kwa hayo mataifa!

Sisi Tuko imara weye kijana! Wewe eneza propaganda ya kumsafisha PK Lkn Huyo Kiongozi wako hasafishiki ata kidogo!
 

Muhalifu anaweza kua mwanasiasa lakini kabla ya kuingia ulingoni lazima sheria zifanyekazi.
Kung'ang'ania unakosema sikuoni atamaliza muda wake 2017,ninacho fahamu wapinzani kama nyie mnachotaka sio kagame aondoke bali mnataka chama kiondoke,kwani hata akiondoka pk RPF itabaki na system itabaki kua ileile kama CCM,ninge waona mashujaa kama mngeweza kuiondoa CCM,lakini hilo hamuliwezi mmekalia kuangalia ya majirani zenu.
 

umeniharibia valentine day yangu kuwafananisha wauaji kama taifa teule shenzi type, rwanda my foot!
 
Hta kama kuna ukweli fulani ila hii habari imeandikwa kipropaganda mno na kujaziwa chumvi sana.

Tatizo ni wepesi wa serikali yetu yenyewe kuwapa wageni kipao mbele kwa kila kitu! waalimu kutoka nchi jirani,Ma managers wa mahotel kutoka nchi jirani, Wawekezaji wasio kuwa na takwimu zinazostahili na on top wanawapa fedha zetu kuanzishia miradi, Makampuni haya ya security yamejaa wageni, kwa mtiririko huu unadhani mchi itabaki salama? maana hujui adui ameingia kwa style ipi, tukilalamika tunaambiwa na hao hao viongozi wetu hususani mawaziri "watanzania ni wavivu na ni wezi makazini" si maanishi wafukuzwe ninyi mawaziri ijengeeni nchi au taifa hili la tanzania liheshimiwe na wageni na wawe nahofu ya uhalifu na nikwakufanya hivi tu KUWEKEZA KWA WATANZANIA WENYEWE KAMA MALI HAI WATU!
Na msipokaa makini mtakuja kuwa na waziri mkuu mnyarwanda! na uasi ukianza sijui tutaumalizia vipi fikirieni sana kuhusu CONGO ilivyo kubwa lakini machafuko yamedumu kwa muda gani na nikinanani wameyaanzisha!
Sawa puuzieni mengine ya Nyerere la kini hili la usalama wa taifa igeni basi kwake!
 
Walikuja wafaransa wenyewe na mashine zao na kupima kilakitu na kusema silaha iliyotumiwa ilikua kambini kanombe,sasa sijui hiyo report yako niyawapi na yalini?usije niletea story za wapinzani wa serikali ya kigali.

Leo hamuwataki Intarahamwe, wakati mlikua mnawatumia mlikua mnaona raha?
 
Ndio walio mwaga damu ni Wanyarwanda Lkn mibaraka yote RPF ilipewa toka kwa hayo mataifa!

Sisi Tuko imara weye kijana! Wewe eneza propaganda ya kumsafisha PK Lkn Huyo Kiongozi wako hasafishiki ata kidogo!

Sikiliza ndugu yangu,mtu anaweza kukubaliki lakini kama mwanaume kwako sio kwasababu alikubariki alale na mkeo au kukuamulia jinsi ya kuendesha maisha yako,nafikiri wakati umefika wa kila mtu ku win,na maana win-win sio win- lose.
 


Umeandika kwa kufikiria Lkn Mkuu? Mfumo Wa kulinda nchi Au Wa usalama hauko km siasa Au ni wakupigiwa debe km propaganda!
 

Ingekua ni pk kaambia wapinzani wake haya uliyo niandikia ungesema ni dikteta,sasa wewe sijui nikuite nini?mbona raia wakawaida unaleta vitisho kwa mtu anayetoa maoni yake ungefanywa rais ungefanya maovu mangapi?.
 
Sikiliza ndugu yangu,mtu anaweza kukubaliki lakini kama mwanaume kwako sio kwasababu alikubariki alale na mkeo au kukuamulia jinsi ya kuendesha maisha yako,nafikiri wakati umefika wa kila mtu ku win,na maana win-win sio win- lose.


Sasa utamsafisha vp Huyo Kiongozi wako na hizo tuhuma za kimbari?
 
Taifa teule ni lipi? Taifa teule kama unavoliita mbona na wao ni majangil wakubwa wanawachinja wapalestina kama kama Tembo wa Tanzania, waislael mm cwatofautish na wauza pembe za ndovu
 
Umeandika kwa kufikiria Lkn Mkuu? Mfumo Wa kulinda nchi Au Wa usalama hauko km siasa Au ni wakupigiwa debe km propaganda!

Kama umesoma vizuri utaelewa nimemaanisha nini! ulinzi siku zote unajulikana ni njia ya kujihami na adui! na adui siku zote anatafuta udhaifu wa mtu aliye jihami naye! sidhani kama nilicho andika ni propoganda au napiga debe kama uzanivyo nilicho andika ni somo! mfano, hakuna kitu kinamuuma mwanaume kama kuibiwa mke, ila inamchukua mda sana mwanamume huyo kujua ukweli na anapokuja kujua ninani mbaya wake pengine ni rafiki yake wa karibu! hapa mbinu ni adui anacheza na udhaifu wako tu!
 
Umeandika kwa kufikiria Lkn Mkuu? Mfumo Wa kulinda nchi Au Wa usalama hauko km siasa Au ni wakupigiwa debe km propaganda!

Mnaelekea pagumu,tanzania ilikua nchi ya amani bila ubaguzi sasa huyo shetani wa ubaguzi na ukabila kawaingilia,sasa mumeanza kusakama waha,wahangaza,wahaya,wanyambo eti ni watusi,poleni sana,kwa ushauri wangu hilolitakua kosa kubwa na ambalo mtajutia,kwani mtaipoteza amani na kuirudisha itawagharimu sana,mungu apushilie mbali huyo pepo wa ukabila.
 
Patrick Elias
Mfano marekani na NATO wanapigana na kakikundi tu taliban waulize mziki ulivyo mnene.

Taliban kutumia guerilla tactics ndo mziki mnene?

Ku plant roadside bombs au kutumia suicide bombers ndo mziki mnene?

Usha compare Nato casualities to taliban casualities?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…