Kuna kundi la vijana walamba asali wametumwa kumchafua na kumharibia Waziri Mkuu

Kuna kundi la vijana walamba asali wametumwa kumchafua na kumharibia Waziri Mkuu

Abraham Lincolnn

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2018
Posts
2,754
Reaction score
4,975
Kama heading inavyojieleza,

Kwa siku hizi mbili nimeshuhudia nyuzi pamoja na post nyingi katika mitandao ya kijamii yenye malengo ya kumchafua Waziri mkuu Mh. Kassim Majaliwa Kassim wakimtuhumu kuwa ndiye anayemwangusha namba moja.Baadhi ya post zimekuwa zikimtuhumu kwamba amekuwa huchukui hatua pale inapompasa.Binafsi ninasimama upande wa PM kwa hoja zifuatazo:

Kwanza kabisa kwa mujibu wa katiba ya JMT mwenye mandate ya kuteua na kuunda baraza lote la mawaziri ni Rais wa JMT, PM hana mamlaka ya kuteua au kuwajibisha mawaziri, Mwenye mamlaka hayo ni Rais.PM hupatiwa baraza akiwa kama mtendaji mkuu na msimamizi. Hana nguvu ya kuwawajibisha mawaziri kikatiba, ni sawa na kiranja mkuu, hawezi kumfukuza mwanafunzi shule, Mwenye uwezo huo ni mkuu wa shule. Je, kama Mwalimu mkuu hana uwezo kiutendaji wa kuwawajibisha na kuchukua hatua dhidi ya wale aliowateua, PM atafanya nini?

Pili, kuna ule msemo wanasema "Never outshine your master" ikiwa na maana kwamba kamwe usiwe mtendaji au usitende vyema kumzidi 'boss' wako. Nadhani hiyo ndiyo mindset inayotawala katika serikali kwa sasa.Sote tunafahamu utendaji wa aliyekuwa waziri wa fedha na sasa VP Mh Philip Mpango, alipoingia katika kiti chake alianza kwa spidi kali wengi wakasema anaonekana yeye ndiye Rais lakini sote tunafahamu kilichofuatia, Hatimaye akanywea ghafla na ile kasi yake ikapotea kabisa. Kwa mentality hii ni vigumu kwa PM kutenda kazi zake katika 100% capacity kwa kuhofia kibarua chake.

Tatu, Hakuna asiyejua kwamba hivi sasa genge la walamba asali limerejea kwa kasi kubwa, Aidha Namba moja huenda hafahamu au anafahamu au naye analamba asali pamoja nao. Unapofanya kazi katika mazingira haya inakulazimu kuwa makini mno ili kulinda kibarua chako! Wengi wanafahamu utendaji wa PM na ni wazi kabisa kasi yake ni kubwa hata imani, uzalendo na utendaji wake ni zaidi ya boss wake na namna ya utendaji wake ni tofauti kabisa na Boss wake hivyo inamlazimu kupunguza kasi ili kwenda sambamba.Rejea aliyekuwa spika alipozungumza ukweli sote tunafahamu yaliyomkuta.

Hitimisho, Bila kupepesa macho ni wazi kwamba kati ya awamu ambayo inaonekana kufeli na kutokukubalika miongoni mwa watanzania wengi isipokuwa wale walioweka vidole vyao katika buyu la asali, Ni awamu hii ya Sita.Kwa utafiti usio rasmi, watanzania 9 kati ya 10 wanaonekana kutoridhishwa na utendaji wa serikali iliyopo.Kwa kutambua hili baadhi ya vijana walamba asali wametumwa kumchafua na kumuangushia jumba bovu PM ili kumsafisha namba moja kwa madhumuni ya kisiasa.

Kuna msemo wa kiswahili "mfa maji haishi kutapatapa" Nadhani mpango wao umeshafeli kwa maana hakuna mtanzania mjinga asiyetambua yanayoendelea. Tangu lini kiranja mkuu akaacha shule kisa wanafunzi wamelala njaa? Katiba imempa madaraka Rais kuisimamia na kuiongoza serikali yake na si PM inashangaza kuona mnataka kumtupia lawama PM! Hii inaonyesha udhaifu na kutowajibika kwa uongozi wa ngazi ya juu. INASIKITISHA
 
Naona mnampigania sana, kwa nini asijipiganie mwenyewe, hawezi kujibu hoja.
 
Kama heading inavyojieleza,

Kwa siku hizi mbili nimeshuhudia nyuzi pamoja na post nyingi katika mitandao ya kijamii yenye malengo ya kumchafua Waziri mkuu...
Waziri Mkuu alikula wapi kiapo kwa rais wa awamu ya sita?

Rais Mpya anapoapa maana yake serikali yote inapaswa kuteuliwa tena. Hilo ni moja

Jengine ni kuwa Waziri Mkuu anaonekana kupwaya kabisa kwenye usimamizi wa maafa na majanga yanayogusibu daily

Tunaona uwajibikaji wake ni hitaji la msingi
 
Majaliwa ni hopeless ila hilo genge linalompinga hata mimi nimeligundua. Haiwezekani alaumiwe yeye kwa kila kitu as if tulimchagua awe Rais. Yanajirudia yaleyale ya ufisadi mkubwa wa serikali kisha lawama zote kwa Lowassa na Kikwete akiachwa kama malaika.
 
MAJALIWA anamiliki timu ya mpira wa miguu ya Namungo hizo fedha za kuendesha timu anapata wapi!Maamuzi yake mengi ni dhaifu huyu ni mwizi kama wezi wengine
Zilongwa mbalì, zitendwa mbali, punguza pombe!!!!.
 
MAJALIWA anamiliki timu ya mpira wa miguu ya Namungo hizo fedha za kuendesha timu anapata wapi!Maamuzi yake mengi ni dhaifu huyu ni mwizi kama wezi wengine
Mwigulu anamiliki timu ya Mpira, Kampuni ya mabasi, Kampuni ya ku bet (m-bet) pesa anatoa wapi?
 
MAJALIWA anamiliki timu ya mpira wa miguu ya Namungo hizo fedha za kuendesha timu anapata wapi!Maamuzi yake mengi ni dhaifu huyu ni mwizi kama wezi wengine
Jamani Baba wa watu mpole vile unamuingiza kwenye kashfa za wizi? amemuibia nani?
 
Kama heading inavyojieleza,

Kwa siku hizi mbili nimeshuhudia nyuzi pamoja na post nyingi katika mitandao ya kijamii yenye malengo ya kumchafua Waziri mkuu...
Eti uPM mnataka mumpe eti

Makambaaa

Hii nchi ngumu sanaaa
 
Mwigulu anamiliki timu ya Mpira, Kampuni ya mabasi, Kampuni ya ku bet (m-bet) pesa anatoa wapi?
Samahani mkuu inamaana waziri mkuu akiwa kapwaya ndio atafute waziri mwingine mbovu Ili kulinda ubovu wake

Sio waziri mkuu tu hata hao wengine ambao hujawataja wote wabovu saana. Tunachohitaji kama raia mwema mtanzania mzalendo mh waziri mkuu ni mzigo anapaswa kujihudhuru

Nyote mnaontete mnaweza kutoa mrejesho wa kamati alizounda upoje ?
 
Wanamuogopa maana wameona nyota yake inang'aa sana kwa raia kuliko kwa keyboard warriors
Nyota ipi unayoizungumzia mkuu ,au kushindwa kitekeleza majukumu yake kama waziri mkuu

Jamaa ni mwongo mwongo saana hawezi kuamnika kwenye jamii iliyostarabika .Ninyi nyote mnaontete a mtakuwa mmekula posho toka kwake na si vingine
 
Huyo Majaliwa Ni muongo muongo hakuna Mtu anapenda kuongea uongo Hadi msikitini

Eti Rais ni Mzima wa Afya yupo anachapa Kazi kauli hii aliiongea kabra ya siku moja ya kifo Cha Rais Magufuli akiwa msikitini.


tangu siko hiyo namchukulia kama muhuni asiyekubari kuwajibika
 
MAJALIWA anamiliki timu ya mpira wa miguu ya Namungo hizo fedha za kuendesha timu anapata wapi!Maamuzi yake mengi ni dhaifu huyu ni mwizi kama wezi wengine
Hamilik Yeye ni.mmoja wa wafadhir wa timu.....!! Ika bwana tozo ile timu ya kwake...akianguka na timu inaanguka akiinuka na timu inainuka...[emoji125][emoji125]
 
Back
Top Bottom