Kuna madhara yoyote ya kuweka "Neutral Gear" kwenye magari Automatic?

Kuna madhara yoyote ya kuweka "Neutral Gear" kwenye magari Automatic?

Ni udereva wa kishamba kuweka Neutral gear(iwe manual au automatic)eti kusevu mafuta. Tumia gia kubwa au weka D wakati wa kushuka miteremko mikali ili gari iwe nzito kuepuka ajali . Nikama unaongezea breki
 
Kwanini nikanyage mafuta wakati lengo langu ni kuokoa mafuta kwa kutumia available potential energy ya slope iliyopo badala ya kuunguza mafuta yangu unnecessarily?
Hivi slope unayoshuka ina kilometers ngapi na unataka kuokoa litres ngapi za mafuta? Tuanzie hapo kwanza,maana kwa barabara zetu za Tz sijasikia kuna mteremko wa barabara unaozidi kilometers 5
 
Hivi slope unayoshuka ina kilometers ngapi na unataka kuokoa litres ngapi za mafuta? Tuanzie hapo kwanza,maana kwa barabara zetu za Tz sijasikia kuna mteremko wa barabara unaozidi kilometers 5
Kigamboni bridge kuna mteremko wa kama 700m hivi
 
Mkuu kwa gari automatic za kisasa gari ikishakuwa kuwa mwendo wa kwenda Mbele ukiweka gear ya parking au reverse kamwe haiwez kuengauge. Utaskia tuu mlio kwamba disc lock zinatema tuu
Sio kweli, labda hizo gari kama zimetoka mwaka huu. Mm huwa na engage R hata kama gari inaserereka mbele inaingia na inarudi revrse. Japo najua sio sahihi
 
He neutral inapunguza matumizi ya mafuta??napitatuu
 
Umekokotoa na risk of potential car /gearbox damage,na umefanya ulinganisho/ cost benifit analysis juu ya mafuta utakayoserve na gari likiharibika?
Gari linaharibika vipi kwa kuweka free, mbona una-assume kana kwamba tumekubaliana juu ya hilo, gari kuharibika huo ni mjadala pia, tuanze mjadala wa gari kuharibika sasa, lete evidence, data na all that have you to support your arguement.
 
Yeah, modern, fuel injected (sio carburettor) rngines ziko efficient kiasi hicho
Itakata mafuta only if hujakanyaga pedal, ukikanyaga it means you want to move faster than the slope provides, hivyo engine power itatumika ku-gain speed, haiwezi kuzima
 
Kuna mtu kasema uweke N ukiwa kwenye Jam au Foleni,hii sio sahihi kwasababu gari linaweza likarudi nyuma au kwenda mbele uuka gonga gari lingine,kwasababu gari linakuwa Free kutegemeana na slope iko upande gani,kwa gari ndogo una weza ku tumia N kama upo kwenye tambalale au mteremko usio mkali,ila kwa magari makubwa kama malori ni hatari sana,tuliwahi pona kupata ajali kwa mchezo huo,scania 113 tukiwa tunashuka kwa mtetemko maeneo ya kwa tenende mbeya,gari iliwekwa N,tulipo maliza mteremko jamaa anarudisha kwenye Gear kumbe gari ilikuwa isha zima kitambo,Mungu saidia aka tupia gear kubwa kwa nguvu na kushtua na klach gari ndo ikawaka,otherwise kama ingegoma,tulikuwa tunaingia korongoni na semi ikirudi kwa nyumba,kuwa makini sana unapo upply N inaweza kukusababishia matatizo makubwa...
 
Wewe kama ni mbahili wa mafuta jitahidi utumie gari yenye Manual Gearbox ni mwendo wa kupiga kofi tu kwenye mteremko
 
Wacha wenye meno wasuguane mpaka tupate Jibu.
1.Hata mm hapo kwnye Sensa kutumia Mafuta badala ya umeme sikumuelewa huyu Bandugu.
2.Nadhani kinachodertermine ulaji wa mafuta ni uchomaji wa mafuta kupitia Nosel kwnye plug na hii inatokana na kuminya acellerater ambapo Utupwaji wa mafuta ya Pressing ya acellerater inaonekana kwenye RPM... kama RPM ipo low Basi mafuta pia hutupwa kidogo.
Maana yake Basi Netraul hupelekea RPM kua Chini na matokeo yake mafuta kutumika kidogo. (Akili zangu binafsi/bila mwalimu).

Haishauriwi kueka Gari Neutral ukiwa kwenye mteremko, kwa sababu gari iyashuka kwa haraka sana, unapokuwa katika gia wakati unateremka, speed ya ushukaji inakuwa controlled, inasaidia kusimama haraka na breki, ila ikiwa inashuka fasta wakati unabrake utachelew kusimama na breki zitalika na kupata moto fasta.

Tumia neutral pale ambapo gari inahitaji kuvutwa ikiwa imekuharibikia.

Sensor zinahusika sana kwenye suala zima la unywaji wa mafuta. Kuna Mass Airflow Sensor na nyengine Oxygen Sensor.
MAF inakaa maeneo yanayoingiza hewa kwenye mashine, utaikuta maeneo ya Air cleaner na O2 inakaa kwenye exhaust manifold/maffler ya mwanzo kutoka kwenye engine. Unapokanyaga accelerator, thottle body inafungua mdomo kupitisha hewa kwenda kwenye combustion chamber, hapa hii MAF inaiambia ECU kuna hewa kiasi fulani imeingia, baada ya information hio ECU inajua ni kiasi gani cha mafuta yanahitajika kwenye engine. Baada ya mripuko kwenye engine, hewa ilokuwemo ndani inatolewa kwenda kwenye Exhaust, huku ndio kuna O2 sensor, ambayo itaiambia ECU ya gari kiasi cha oxygen kilichomo kwenye hewa ilotolewa, hapa ECU itatambua uripuaji uliofanyika kama Hew ilikuwa nyingi kuliko mafuta au mafuta yalikuwa mingi kuliko hewa, na kuifanya ECU hio kufanya marekebisho ili hew na mafuta yawe sawa. Sensor hizi mbili zikifeli, Gari litakunywa mafuta na perfomance itakuwa mbaya.

Plug ama coils zikiwa mbaya, gari itakuwa ina miss, hii ni kwa sababu kwenye engine, cylinder yenye plug/coil mbovu itakuwa haichomi mafuta yanayoingia, In theory, mafuta yanayokwenda ndio yale yale, ila yanakuwa wasted bila ya kupatikana nguvu yoyote, itakuwa inakunywa mafuta bila sababu. Pia chengine kinachochangia unywaji wa mafuta, ni fuel injectors, hizi zinatakiwa zikipuliza mafuta ni mfano kama vapor tu, lakini ikianza kutoa mafuta mfano wa mkojo, gari litakuwa lina mripuko mbovu na mafuta yatakuwa yanakwenda mengi sana. kama umelaza gari, asubuhi ukaliwasha, utakuja kuona gari linatoa moshi mwingiiiiiii, hii ni kwa sababu kwenye hio cylinder mafuta yalikuwa yakichuruzika ndani kdg kdg, ila usiogope, once they are all burned out gari haitotoa moshi (ukiwa umebadili injector).
 
haina shida ila sasa ukiweka uwe na kumbukumbu nzuri usije ukajisahau ukapeleka kwenye "P" mzee baba yatakua mengine
Gari Automatic hasa za toyota hauwezi kuhama kutoka neutral kwenda P bila kubinya kile kidude cha kati na P haiingii bila kukanyaga brake...
 
Fundi wangu alisema neutral inaharibu difu kwa sababu gari inapokuwa kwenye mwendo mkubwa alafu iko N unaporudi D gia hulazima kubadilika haraka sana ndani ya sekunde ili kuendana na mwendo stahili, kitendo hiko ndio kinaharibu difu.
 
Fundi wangu alisema neutral inaharibu difu kwa sababu gari inapokuwa kwenye mwendo mkubwa alafu iko N unaporudi D gia hulazima kubadilika haraka sana ndani ya sekunde ili kuendana na mwendo stahili, kitendo hiko ndio kinaharibu difu.
hakuna kinachoharibika wakati wa kutumia N gear kwani mwendo wa speed unaonekana na RPM unaisoma unachotakiwa jua huu mwendo ni speed na RPM ngapi unachomeka gear ya D
The transmission control module (TCM) is located inside the transmission housing, instead of being located outside it. The advantage of this is to reduce external wiring as well as to provide a constant environment for TCM operation which encourages longevity. One aspect of the advanced nature of the electronics is at idle (along with required foot brake depression on e.g. Opel Astra), it automatically selects neutral gear to reduce internal temperatures and improve fuel economy.
kwanza inaokoa mafuta na majotojoto kwenye injini na maOil ndio maana hapo namuunga mkono FRANCIS DA DON
 
Wacha wenye meno wasuguane mpaka tupate Jibu.
1.Hata mm hapo kwnye Sensa kutumia Mafuta badala ya umeme sikumuelewa huyu Bandugu.
2.Nadhani kinachodertermine ulaji wa mafuta ni uchomaji wa mafuta kupitia Nosel kwnye plug na hii inatokana na kuminya acellerater ambapo Utupwaji wa mafuta ya Pressing ya acellerater inaonekana kwenye RPM... kama RPM ipo low Basi mafuta pia hutupwa kidogo.
Maana yake Basi Netraul hupelekea RPM kua Chini na matokeo yake mafuta kutumika kidogo. (Akili zangu binafsi/bila mwalimu).
Akili zako changanya na za kupewa sasa[emoji16][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom