Kuna magroup ya WhatsApp ya DAWASA maeneo yote Dar, Waziri Aweso omba links za maeneo yenye malalamiko upate uhalisia

Kuna magroup ya WhatsApp ya DAWASA maeneo yote Dar, Waziri Aweso omba links za maeneo yenye malalamiko upate uhalisia

Precious Diamond

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2023
Posts
593
Reaction score
1,376
Salam,

Tunaendelea katika episode nyingine ya 'MZINDUE AWESO MAJI YAREJEE', na leo tumpe mbinu nyingine ya kujua uhalisia wa kinachotokea mtaani. Yaani hii wiki inaenda kuisha kule Mbezi Beach maji yametoka haijazidi siku moja, afu Waziri Wizara ya Maji huko anajitapa tu maji yapo na chawa wake wajinga wanamwambia maji yapo aachane na kelel za mtandaoni, useless kabisa!

Sasa Aweso Wizara ya Maji mbinu hii nakupa uache kutupa majibu yako yenye 0 research, kwenda kwenye maeneo ya wananchi physically unaweza kusema huwezi kujigawa, hamna tabu, basi tumia njia hii itakayokusaidia kupata taarifa za ukweli katika maeneo yote kwa wakati mmoja.

Kwenye maeneo yetu tuna groups za WhatsApps za DAWASA, ambayo kote mameneja wa DAWASA wapo ambao wanasimama kama wawakilishi wako na ndio ambao wanakulisha taarifa za uongo na wewe unazibeba kama utafikiri huna uwezo wa kuzihakiki.

Omba links zote za group za WhatsApp kwenye maeneo yote yenye malalamiko halafu unakuja kujitamba maji yapo, ingia kwenye group hizo zote kwa kutumia namba tofauti ambayo watendaji hawa hawana, waambie waseme kero zao sababu umeona wananchi wanasema maji hayapo wakati kwa ufahamu yako unajua maji yapo ya kutosha. Wizara ya Maji

Wananchi watafunguka utapata uhalisia wake, ukipata majibu tunaomba pia uje useme umegundua nini na nani anakwamisha wananchi tuspate maji. Ukiendelea kukaza fuvu na njia zote unazo za kupata habari za uhakika utakuwa umeamua mwenyewe kujiharibia.

Kwenye malalamiko ya wananchi hao machawa wako wanaokaa kusifia kwenye kila kitu waweke pembeni ufanye kazi, hata ukiondolewa wao hawana hasara, watahamia kwa Boss mpya.

Ukishupaza shingo na hapa utakuwa sikio la kufa Wizara ya Maji
 
Anabweka ovyo tu huyo na kufukuza watu lakini bado matatizo yanaendelea kuwepo hata baada ya kuwaondoa watendaji waliokuwepo na kuweka wengine. Inaonekana shida ya maji iko juu ya uwezo wa hao mameneja au taasisi kama taasisi na inahitajika nguvu zaidi kutoka serikalini. Haiwezekani waziri anaondoa watendaji kwa mbwembwe zote zile lakini hata hawa wapya wasilete mabadiliko yoyote yanayowezesha wananchi kupata maji. Wananchi wanataka maji siyo kelele na mbwembwe za waziri zisizoleta tija yoyote.
 
Huyo nae Sasa kawa Msanii. Shida ya maji hapa Dar haiitaji mtandao ya kijamii kuona au kupima tatizo la maji. Akiwa kwenye V8 lake am wambie dereva wake asimame a muulize mama au mtoto yeyote kama hapo wana maji au mara ya mwisho maji kutoka hapo ni lini?
 
Ishu ya maji Mbezi Beach nimemvua nyota waziri Aweso.

Ile siku katoka hadharani anatamka kabisa kwamba kulikuwa na tatizo dogo limeshatatuliwa sasa mbezi beach wanapata maji bila shida nilimshangaa sana aisee
 
Salam,

Tunaendelea katika episode nyingine ya 'MZINDUE AWESO MAJI YAREJEE', na leo tumpe mbinu nyingine ya kujua uhalisia wa kinachotokea mtaani. Yaani hii wiki inaenda kuisha kule Mbezi Beach maji yametoka haijazidi siku moja, afu Waziri Wizara ya Maji huko anajitapa tu maji yapo na chawa wake wajinga wanamwambia maji yapo aachane na kelel za mtandaoni, useless kabisa!

Sasa Aweso Wizara ya Maji mbinu hii nakupa uache kutupa majibu yako yenye 0 research, kwenda kwenye maeneo ya wananchi physically unaweza kusema huwezi kujigawa, hamna tabu, basi tumia njia hii itakayokusaidia kupata taarifa za ukweli katika maeneo yote kwa wakati mmoja.

Kwenye maeneo yetu tuna groups za WhatsApps za DAWASA, ambayo kote mameneja wa DAWASA wapo ambao wanasimama kama wawakilishi wako na ndio ambao wanakulisha taarifa za uongo na wewe unazibeba kama utafikiri huna uwezo wa kuzihakiki.

Omba links zote za group za WhatsApp kwenye maeneo yote yenye malalamiko halafu unakuja kujitamba maji yapo, ingia kwenye group hizo zote kwa kutumia namba tofauti ambayo watendaji hawa hawana, waambie waseme kero zao sababu umeona wananchi wanasema maji hayapo wakati kwa ufahamu yako unajua maji yapo ya kutosha. Wizara ya Maji

Wananchi watafunguka utapata uhalisia wake, ukipata majibu tunaomba pia uje useme umegundua nini na nani anakwamisha wananchi tuspate maji. Ukiendelea kukaza fuvu na njia zote unazo za kupata habari za uhakika utakuwa umeamua mwenyewe kujiharibia.

Kwenye malalamiko ya wananchi hao machawa wako wanaokaa kusifia kwenye kila kitu waweke pembeni ufanye kazi, hata ukiondolewa wao hawana hasara, watahamia kwa Boss mpya.

Ukishupaza shingo na hapa utakuwa sikio la kufa Wizara ya Maji
Waziri mpumbavu kabisa niliyewahi mshudia kwenye maisha yangu hapa Tanzania. yeye anajua kupayuka na KUPIGA MIKELELE NDIYO SULUHISHO LA MATATIZO. ipo siku tutamuanika huyu tunawajua wale matapeli anaojifungia nao masaa kwa masaaa wakijadili uhuni na ufisadi
mji hauna maji badala ya kuja na solution wewe unataka uingizwe kwenye ma group ya watsap? nn ambacho hukijui?
 
watu wanalia na maji mjini ,lakini hiki kipande cha Kurasini hapa Mivinjeni kuna bomba lina miaka ya zaidi ya miwili linamwaga maji.
wanaziba sijui na gundi ya unga wa muhogo halitoboi hata miezi 2 linamwaga tena.Maji yanamwagika tu,jua kali mjini lakini kile kipande unakuta madimbwi.Wajaribu kuzuia upotevu wa maji ni hasara na kuna sehemu watu hawapati maji
 
watu wanalia na maji mjini ,lakini hiki kipande cha Kurasini hapa Mivinjeni kuna bomba lina miaka ya zaidi ya miwili linamwaga maji.
wanaziba sijui na gundi ya unga wa muhogo halitoboi hata miezi 2 linamwaga tena.Maji yanamwagika tu,jua kali mjini lakini kile kipande unakuta madimbwi.Wajaribu kuzuia upotevu wa maji ni hasara na kuna sehemu watu hawapati maji
Wizara ya Maji kuna ujumbe wenu hapa
 
Anabweka ovyo tu huyo na kufukuza watu lakini bado matatizo yanaendelea kuwepo hata baada ya kuwaondoa watendaji waliokuwepo na kuweka wengine. Inaonekana shida ya maji iko juu ya uwezo wa hao mameneja au taasisi kama taasisi na inahitajika nguvu zaidi kutoka serikalini. Haiwezekani waziri anaondoa watendaji kwa mbwembwe zote zile lakini hata hawa wapya wasilete mabadiliko yoyote yanayowezesha wananchi kupata maji. Wananchi wanataka maji siyo kelele na mbwembwe za waziri zisizoleta tija yoyote.
 
Back
Top Bottom