Kuna mahusiano kati ya ndoto na maisha ya kawaida?

Kuna mahusiano kati ya ndoto na maisha ya kawaida?

Ndoto ya aina hii uliwahi kumtokea mume wangu.

Yeye hakuwa na uhusiano mzuri na bibi yake, anasema wakati wako wadogo yeye alikuwa mtundu sana hivyo bibi yake alikuwa hampendi na mpaka alivyokuwa hali hiyo iliendelea ila hakujali na wala haikumsumbua. Siku moja alillala akaota bibi yake amekuja amemuomba msamaha na kumwambia amsamehe kwasababu anataka kwenda mbali ila hakusema wapi. Wakasameheana ndotoni. Aliposhtuka usingizini akasema hii sio ndoto ni kweli, akampigia simu mama ake na kumwambia nenda ukamuage bibi ila sijui kama utamkuta. Kesho yake asubuhi mama ake ndo aliepiga simu na kutoa taarifa ya msiba.
Hizi ndoto kweli zipo ila haziwatokei watu wote.

Zinaitwa ndoto maono au ndoto taarifa
 
Zinaitwa ndoto maono au ndoto taarifa

How I wish niwe naota kama hivyo. Yani ndoto zangu ni za tamthilia au series nazoziangalia, stori ikiwa ya kutisha sana pia naweza kuiota kama ilivyo na mbaya zaidi Mimi ndo nnaekuwa mhusika mkuu. Na mara nyingine huota ndoto za kawaida ambazo hazijawahi kuwa na maana yoyote katika maisha yangu wala ya yoyote yule na nyingine ndo huwa sizikumbuki kabisaa.

Nahisi nahitaji kupractice lucid dreams
 
How I wish niwe naota kama hivyo. Yani ndoto zangu ni za tamthilia au series nazoziangalia, stori ikiwa ya kutisha sana pia naweza kuiota kama ilivyo na mbaya zaidi Mimi ndo nnaekuwa mhusika mkuu. Na mara nyingine huota ndoto za kawaida ambazo hazijawahi kuwa na maana yoyote katika maisha yangu wala ya yoyote yule na nyingine ndo huwa sizikumbuki kabisaa.

Nahisi nahitaji kupractice lucid dream

Practice meditation ufungue mlango wa sita, hii ni level nzuri kuliko lucid dreams
 
Mi nahisi hiyo ni ndoto ya kawaida ila huenda inajirudia kwasababu huwa unaifikiria sana

Wakati mwingine ndoto ni mkusanyiko wa mawazo yetu, yale mawazo ambayo tungekuwa tukiyawaza ubongo huwa bado unayafanyia kazi ndomana tunaota.

Huwa unaota muda gani?

Huwa naota usiku na alfajiri sana sana
 
Sali kabla ya kulala. Pia angalia ni vitu gani huvipitisha kichwani kwako kabla ya kupata usingizi.
 
ndugu zanguni naomba mnisaidie maana ya ndoto hii maana nimeiota mara kwa mara, huwa naota niko kwenye mto mkubwa sana smtyms nakuwa nimekaa pembeni, wakati mwingine navuka huo mto ,wakati mwingine naogelea na naweza ota nahangaika tu mtoni hapo...plz wat doez t mean jmn? Honestry inanitesa sana.
 
Ndoto ni kile unachokiwaza mara kwa mara kutwa.. Ndoto hubeba uhalisia
Kama lile unaloota halitakutokea leo bas sku nyingne

Mnashauriwa kusali kabla ya kulala kuepeuka kuota ndoto mbaya maana unaweza ukaita unaliwa na simba porini na kufa na kweli ukafa kweli asubuh usiamke teh
 
Mimi toka niko Pre-form one imekuwa kawaida yangu sana kuota nafanya mtihani na wakati wote nikiingia kwenye pepa naikuta vivyo hivyo na kila kitu kinaenda kama kilivyokuwa kwenye ndoto.
Ndoto ambayo sitaisahau ni pale nilipoota nafanya mtihani wa Kemia maswali yote yalikuwa mboga kabisa ila sikuweza kumaliza maswali kwa kuwa nilichelewa kuingia kwenye pepa; sasa baada ya kuona nimeota kuwa nimechelewa kuingia kwenye pepa ile tu nilivyostuka toka kwenye ndoto niliamua kukaa hadi asubuhi ili nisichelewe pepa na kweli sikuchelewa ila nilivyingia kwenye chumba cha mtihani na kukuta maswali yote ni simple na ni yale yote niliyoota nikawa dharau kwa pepa ile cha ajabu muda uliisha kabla sijamaliza mtihani-lilibaki swali moja na niliscore 97% ila nilijuta japokuwa kwa upande mwingine nilifurahi kwa kuwa nilikuwa nimeota kuwa sikuweza kumaliza mtihani wangu huo.
 
Back
Top Bottom