Kuna Mbunge nimemsikia mjengoni akiomba Serikali iajiri wanaojitolea. Hii haikubaliki

Kuna Mbunge nimemsikia mjengoni akiomba Serikali iajiri wanaojitolea. Hii haikubaliki

Rudi kesho kaombe kujitolea..kwani shida nini..mtoto wakiume unalialia kama demu..kaza jombaa..sio lazima wote tuajiriwe.

Mbona kuna wadau hawana hata cheti cha 4m4 ila wanamaisha kuzidi hata mwenye phd.

#MaendeleoHayanaChama
 
Pamoja na kusoma kwako kote bado hujajua kwanin ulienda shule kusoma?
 
Kwa kweli braza post yako haipo clear kabisa. Sasa unasema "mimi napinga kuajiri wanaojitolea, " sasa in maana wewe hutaki hao ndg waliojitolea waajiriwe?

Sent from my TECNO CC7 using JamiiForums mobile app
 
Kujitolea ni dhana pana.Ninaimani maana yake itajumuisha watu wote walio kwenye hali ya kujitolea bila kujali ni private au public kulingana na maslahi wanayoyapata watu pale walip😵pen Schools ni moja kati ya taasisi zinazojitolea moja kwa moja kwa kuisaidia serikali kuwarudisha kundini kondoo waliopotea.Wanaohudumu huko huwa ni watu wasiokuwa na mishahara isipokuwa posho zinazotegemea idadi ya wapokea huduma.Open Schools zinazomilikiwa na wadau binafsi ndizo zinazoongoza kutoa fursa ya kujitolea kwa vijana wengi wanaohitimu fani za ualimu kuliko hata shule za umma.
Rai yangu kwa Mh.Rais na Waziri (OR-TAMISEMI) hiki kigezo kama watakitumia ni muhimu kikawa na ukamilifu ndani yake ili kuondoa dhulma.
Ni muhimu servers za tamisemi zikawa updated ili kuingiza open schools zote vinginevyo kigezo hiki ni batili na hakina lengo lenye lengo.
Pia,maafisa elimu ngazi ya kata washirikishwe moja kwa moja na maafisa elimu wilaya ili kukusanya taarifa za wanaojitolea moja kwa moja kutoka kwenye shule za umma na open schools zote zilozo kwenye maeneo yao kwa kuwaona kwa macho wahusika wakitekeleza majukumu yao siyo hii ya ku-upload barua,ni ubatili na kujilisha upepo.
 
Mtoa mada haujamaliza kutoa hoja, unalalamika mwishowe inakuwa ngumu kupata mantiki....hebu tuambie tatizo ni nini? Na kipi kifanyike?
 
Wanaojitolea ndio walistahili zaidi kuanza kipao mbele kama wewe ulivyokua ukijitolea ila hayo ni maneno tuu kama ulijitolea na ulikosa sasa inakuaje unahisi watapata wanaojitolea? Piga kazi popote kambi.
Je nafasi za kujitolea hutangazwa wapi?.Huoni hiyo ni namna ya kutoleta usawa kwenye Ushindani wa kupata kazi?.Yaani mtu aamue ku volunteer kufanya kazi bila ajira kinyemela ndo aje kunufaika kwenye Ushindani ,why?
 
Kuna andiko linasema "mwenye nacho huongezewa".

Huwezi kupingana na agizo la mwenyezi Mungu.
Biblia uliielewa kweli ... Mwenye nacho alieongelewa pale hafanani kabisa na Mambo yenu ya kidunia
 
Back
Top Bottom