muhomakilo jr
JF-Expert Member
- Jul 28, 2013
- 15,301
- 13,858
Wewe mpuuzi.Kuna mpenzi wangu nilikua nampenda Sana na bado na mpenda Sana ila nimekuja kuomba ushari hapa.
Ipo hivi huyu mwanamke nilikua namhudumia kila kitu ila ikafika mahali akaanza kunijibu dharau na kuniambia hataki mahusiano na mwanaume yoyote "labda atokee mwenye pesa nyingi ambae hata nikimuomba elfu hamsini ananipa hapo hapo"
Wakati huo najinyima ili yeye aweze kula nikamfungulia mpaka ofisi ya Tigo pesa nampa pesa ya matumizi kodi namlipia ila ikatokea akanichana ukweli kwamba hanitaki tena na aka ni Block nikaona isiwe kesi nikaamua kumpotezea ila kwakua nilikua nampenda nikawa nikipita ofisini kwake namuachia hata elfu kumi ya kula..
Kumbe aliyekuwa anampa jeuri ni jamaa flani ndio maana akanipiga chini alafu jamaa ana mke na watoto kabisa sasa kilicho tokea jamaa kampa mimba alafu anamnyanyasa na hampi pesa ya matumizi na ndugu wamemkataa hana msaada popote.
Nashangaa jana kaniita amenipokea kwa magoti analia anaomba msamaha kiukweli nilishindwa kutoa maamuzi kwa haraka wala sikumfokea nikampa elfu ishirini walau apate kituchakula maana jamaa hamjali
Mimi nilikua namjali sana kwakile kidogo nilichokua nacho kuliko huyu jamaa mwenye pesa nyingi na hamjali anamfokea kila wakati hapa nawaza nichukue maamuzi gani maana moyo unaniuma anavyo teseka japo kanifanyia tukio kama hili nimemwambia asitoe mimba nitailea ila kakazana anataka kutoa hivyo nimeacha
aamue.
Anachotaka kufanya ameniomba msamaha anajuta sana. Najua kilicho mrudisha nisababu anashida nimeona nisimlipe mabaya bali ni msamehe na nimsaidie kwenye hili tatizo Lake.
Sijamfokea wala kumlaumu kwa chochote kile hata yeye mwenyewe ameshangaa Sana yale yote aliyo nitendea lakini bado namlipa wema