Kuna mtaalamu wa kuongea na wafu?

Kuna mtaalamu wa kuongea na wafu?

Asante sana kwa ufafanuzi mzuri sana , katika hangaika zangu kutaka kujua kama mpendwa anaweza sikia nili apta habari kwamba kuna Swahaba kipindi cha Mtume ali kwenda kaburini , kitu kama alilalia kaburi au ali busu kabisri ( sina uhakika) wengine wakashangaa, wakaambiwa kwamba Marehemu ana sikia kwa masikio yenye uwezo mkubwa kushinda tulio nayo , hivyo na umenijibu hivyo napata amani kwamba nikenda pale Kaburini nifanye kitu sahihi kwa dua kw akumuombea na kutoa sadaka na pia nimpigishe story .nataka nimwambie nampenda sana na nilikua naye bega kwa bega na nitaendelea kumpenda daima . Nashukuru sana , maana sasa atajuta maana nikiaza mpigisha story nadhani atachoka na mpaka ata pjaribu kupiga miayo maana huwa kama simalizi ,lol , na jisikia kama kesho fasta niende pale Kaburini nikaongeee naye na kumuombea dua . I hope sitakua nime kufuru .
Nashukuru sana sana.
Kaburini hakuna kitu zaidi ya mzoga tu,fanya meditition kokote ulipo spirit ipo haifi ,unaokufa ni mwili tu
 
Mkuu Hiví Kwa Mfano marehemu alitamka kuwa usimpende MTU Fulani na usije ukamsaidia Kwa chochote Hata kama anashinda Kwa sababu ya ugomvi wao lakini wewe ukawa unauwezo na huoni sababu ya kuishi Kwa Chuki na MTU wakati Huna ugomvi naye ZAIDI ya jurithishwa Chuki.

Je, ukiamua kuishi Kwa upendo na kumtendea wema adui Wa marehemu nini kitatokea ?
Marehemu kama alikwambua pumba kabla hajafa sio lazima kufata ujinga wake
 
Anasikia vizuri sana, mpaka vishindo vya miguu kusogelea kaburi na kuondoka anasikia! Dua na maombi anasikia! Asichoweza kufanya ni kusogea, kuongea, kuvuta pumzi!

Dua/Maombi hata kama anafanyiwa kilometa 1,000 au kilometa 6,000 kutoka alipozikwa yeye, anaambiwa na malaika fulani anakufanyia dua/maombi fulani!

Na kama ulikua hujui, hata pindi watu waliokua hai, aliowaacha hai wakimsahau kumfanyia dua/maombi, huwa anahuzunika sana kwanini amesahauliwa!! Na kwa waislamu ndio maana huwa na ratiba kila baada ya muda fulani (Miezi au kila mwaka/miaka) huwafanyia dua/maombi wapendwa wao waliotangulia mbele ya haki (Utaskia; Juzi tulifanya khitma ya wazee wetu au wapendwa wetu waliotangulia mbele ya haki, tulijisahau miaka bana)!!
Hizi ni imani tu hazina uhalisia,mwili ukifa unaoza unaisha hakina kitu
 
[mention]Mshana Jr [/mention] njoo umpe msaada au mtafute [mention]Yericko Nyerere [/mention] mkali wa mizimu
 
Je, kuna mtaalamu yupi aliye Dar anaweza ongea na wapendwa waliotangulia mbele za haki?
Uganga wa kuongea na wafu Tanzania haujasambaa sana, mara nyingi tunauona kwenye muvi za Marekani, huko itakuwa ndio kuna imani hizo. Sijawahi kusikia hata uswahilini mtu kaenda kwa mganga kuongea na mfu, inaonesha imani hiyo sio sehemu ya imani za huku kwetu ni imani ya kigeni
 
Uganga wa kuongea na wafu Tanzania haujasambaa sana, mara nyingi tunauona kwenye muvi za Marekani, huko itakuwa ndio kuna imani hizo. Sijawahi kusikia hata uswahilini mtu kaenda kwa mganga kuongea na mfu, inaonesha imani hiyo sio sehemu ya imani za huku kwetu ni imani ya kigeni
Ilikuwepo kitambo. Sema tumepoteza uasilia wetu. Na wazee wakawa wabinafsi kurithisha watoto wao. So Imepotea kama ambavyo madawa yetu yamepotea na wazee walivyokuwa wanajitibu ila wachina na wahindi wao waliweza kurithisha mpk Leo wako vzr kwenye matibabu. "walikimbia utumwa WA FIKRA".
 
Uganga wa kuongea na wafu Tanzania haujasambaa sana, mara nyingi tunauona kwenye muvi za Marekani, huko itakuwa ndio kuna imani hizo. Sijawahi kusikia hata uswahilini mtu kaenda kwa mganga kuongea na mfu, inaonesha imani hiyo sio sehemu ya imani za huku kwetu ni imani ya kigeni
Kweli nimejaribu fuatilia sana lakini sija sikia kitu kama hicho kwa Tanzania
 
Andaa mil 66.13 nije nikakupandishie huyo mtu hapo kaburini uongee naye physical.
Kumrudisha je? Kama napata hiyo pesa , nitakachoffanya tunandikishiana halafu unamleta naongea naye halafu ndio nakupa pesa .
 
Back
Top Bottom