Kuna mwamba alirudia Form II mara 8 katika shule nne tofauti na zote akafeli

Kuna mwamba alirudia Form II mara 8 katika shule nne tofauti na zote akafeli

Boss la DP World

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2021
Posts
2,318
Reaction score
8,464
Huyu mwamba alikuwa anafahamika sana kwa kupata mitihani ya form two iliyovuja na alikuwa anaipata ile yenyewe, alikuwa na moyo wa kuwapiga pindi wenzake na kuwakaririsha majibu, akiingia kwenye chumba cha mtihani anafeli kwa kishindo, yaani F zote, wenzake wanafaulu.

Alikuwa ni mtoto wa mwalimu wa Primary, mama yake aliamini katika elimu na elimu pekee, alianza primary kijijini kwao, akafaulu sekondari ya kijijini kwao alivyofika form II akafeli mara 2 mfululizo akafukuzwa (miaka hiyo ilikuwa ukifeli mara 2 unatimuliwa)

Mama yake akamtafutia nafasi City Secondary - Dodoma mjini, ni shule ya private, mwamba akafeli mara 2 akatimuliwa, mamayake akafanya mchongo akapata shule ya Central, akafanya mtihani akafeli mara 2, mama yake akacheza makaratee, akapata nafasi shule ya Jamhuri jamaa bila ajizi akajiunga akafeli mara 2.

Mama yake akampeleka chuo cha Donbosco pale Dodoma akasomea plumbing akawa fundi bomba (huenda mama yake aliona mabomba mengi ni ya duara kama namba 0)

Mshikaji sahivi anaendelea na ufundi na anaishi maisha ya standard nzuri tu. Siamini kama kuna mtanzania amemzidi huyu mwamba kwa experience ya kidato cha 2.

Mwenyewe anaamini NECTA walikuwa na kisa naye.
 
Huyo hadi nimemwonea huruma. Kuna mbunge wa viti maalum kwa tiketi ya CHADEMA kutoka kaskazini.. nikiwa darasa la 3 yeye yuko la 7.

Nae pia kasotea sana ku-risiti kidato cha nne kwasababu wakati niko kidato cha nne bado alikuwa anarudia mtihani. Shukrani kwa kigogo wa CHADEMA aliyemsaidia kuingia kwenye siasa hadi kupenya kwenyw viti maalum ingawa wenyewe wanamwita Covid19 kwa sasa.
 
Arsenalf.c anakubalije kupitwa na kupokonywa ubingwa na city f.c 😁🙃
 
Kwa hiyo na mara zote 8 alikuwa akiipata hiyo mirihani?
Hebu tufahamu alikuwa akizipata wapi hizo nyaraka nyeti hivyo…!!
 
Huyu mwamba alikuwa anafahamika sana kwa kupata mitihani ya form two iliyovuja na alikuwa anaipata ile yenyewe, alikuwa na moyo wa kuwapiga pindi wenzake na kuwakaririsha majibu, akiingia kwenye chumba cha mtihani anafeli kwa

Mwenyewe anaamini NECTA walikuwa na kisa naye.
Anda kiwango cha Disqualification Hons
 
Kama ni kabla ya mwaka 2010 , paper ya form 2 ilikua inatungwa kikanda na kusahihishwa kikanda. Kanda ya Kati paper ilikua inavuja hatari, Yan kwa shule za mjin pale kama Dom sec,merriwa, viwandani, Jamhur, hijra, central,kndege, nk sidhan kama Kuna mwanafunzi aliyekua anakosa paper hata kama ni nusu Yan baadhi ya sections. Mtu akifeli bas alikua mjinga kweli
 
Mwamba kabarikiwa uvumilivu, kanyimwa akili lakini ana ujasiri wa kutokata tamaa kizembe zembe, mungu hakunyimi vyote
 
Back
Top Bottom