Kuna office nimeitembelea leo,office nzima mpaka mkurugenzi hawajui kuongea Kiingereza

Kuna office nimeitembelea leo,office nzima mpaka mkurugenzi hawajui kuongea Kiingereza

Kiingereza ni lugha tu kama lugha zingine mfano Kimatumbi, kisukuma kiswahili n.k

Mnafundishwa kimatumbi shuleni? Maana mtu unasomea kingereza shuleni ila huna uwezo wa kukutumia, Sasa cha nini kujisumbua...
 
Aliekwambia ukurugenzi ni kujua kiingereza nani.
Ni kukosa kujiamini tu...Mimi mtu akija kwangu ataongea Kiswahili kama hataki atajua mwenyewe! Kama lafudhi yao huipati vizuri ndio ufanye Siri! Mwambie aongee kwa hatua😐
 
Hii nchi ina vituko sana.

Kuna wageni kutoka marekani wametembelea Tanzania kujifunza mambo flani flani,boss wangu akaniteua mimi na wenzangu wawili tuwaongoze kwenye shughuli zao zilizowaleta.

Cha ajabu kuna office tumeenda leo,office nzima hakuna anayeweza kuongea kiingereza kizuri,hadi mkurugenzi wa office ni zero kwenye kiingereza, eti mkurugenzi akanivuta pembeni akaniambia hayuko vizuri kiafya hivyo anaomba anikabidhi kwa meneja wake ili atusaidie shida yetu,

Meneja nae akazuga eti yuko busy lkn baadae akanivuta pembeni akaniambia huwa anapata shida kuelewa accent ya kimarekani hivyo anaomba niwe namtafsria wanachoongea hawa wageni.
Nimeshangaa sana aisee.
Wew unaejuwa kiingereza unawazidi nini hasa?!
 
Ni kawaida mkuu, sio wote ni wazuri kwenye kingereza hasa cha kuongea tena na wenye lugha yao.

Mngekua mnaandika na yeye anajibu labda angeweza ila sio kuongea papo kwa hapo
 
Ach
Hii nchi ina vituko sana.

Kuna wageni kutoka marekani wametembelea Tanzania kujifunza mambo flani flani,boss wangu akaniteua mimi na wenzangu wawili tuwaongoze kwenye shughuli zao zilizowaleta.

Cha ajabu kuna office tumeenda leo,office nzima hakuna anayeweza kuongea kiingereza kizuri,hadi mkurugenzi wa office ni zero kwenye kiingereza, eti mkurugenzi akanivuta pembeni akaniambia hayuko vizuri kiafya hivyo anaomba anikabidhi kwa meneja wake ili atusaidie shida yetu,

Meneja nae akazuga eti yuko busy lkn baadae akanivuta pembeni akaniambia huwa anapata shida kuelewa accent ya kimarekani hivyo anaomba niwe namtafsria wanachoongea hawa wageni.
Nimeshangaa sana aisee.
Acha ulimbuke dogo.
 
Vituko ni vingi kwemye maofisi wanapotembelea wageni. Huko mashuleni ndio utashangaa zaidi mkuu wa shule na makamu wake kukimbia na kukuachia msala uzungumze kiingereza na wageni wanaokuja shuleni. Nasema inaudhi sana na kukera bosi kuingia mitini kisa hajui kuongea kiingereza vema wakati amesoma mpaka form six hadi chuoni na degree anayo. Pumbavu sana, wakiambiwa wakasome ufundi VETA na hizo degree zao povu linawatoka na kudai wamedharauliwa
 
unashanga mkurugenzi wa ofisi wakati rais wa China taifa kubwa duniani katika kila kitu na yeye pia hajui kingereza
China hawahitaji sana English lakini wewe Mswahili unahitaji sana English.
 
Sio kesi man lugha za watu hizi.Mbona wenyewe hawajui kiswahili?

Ukweli ni kwamba hakuna mtanzania aliyepita mfumo wa formal education atashindwa kujua English ya kujieleza hii ya is and was.Tatizo mnapenda waongee kama watoto wa malkia na wakikosea mnaleta mada kama zote humu.
Jeni Mhagama
 
Hii nchi ina vituko sana.

Kuna wageni kutoka marekani wametembelea Tanzania kujifunza mambo flani flani,boss wangu akaniteua mimi na wenzangu wawili tuwaongoze kwenye shughuli zao zilizowaleta.

Cha ajabu kuna office tumeenda leo,office nzima hakuna anayeweza kuongea kiingereza kizuri,hadi mkurugenzi wa office ni zero kwenye kiingereza, eti mkurugenzi akanivuta pembeni akaniambia hayuko vizuri kiafya hivyo anaomba anikabidhi kwa meneja wake ili atusaidie shida yetu,

Meneja nae akazuga eti yuko busy lkn baadae akanivuta pembeni akaniambia huwa anapata shida kuelewa accent ya kimarekani hivyo anaomba niwe namtafsria wanachoongea hawa wageni.
Nimeshangaa sana aisee.
mura kyagata nomonto waweito ole serengeti tantoli emelemo..
👇👇👇
Though I can not speak much English
 
Mkuu mbona Wachina hawajui Kiingereza tena utakuta Mchina ni Engineers kabisa, Au Mtaalamu wa Maswala ya Mafuta na gas lakini Kiingereza hajui, Utakuta anataka kwenda mjini anamwambia Dereva ampeleke mjini sasa lugha ya Kiingereza anayosema inafurahisha, utasikia ana Mwambia dereva Me you to Town( ana maanisha apelekwe mjini).
Wachina hawahitaji Kingereza sana, wao ni mojawapo ya utamaduni wa kale zaidi duniani, wana watu bilioni 1.4, ni uchumi namba mbili kuwa ukubwa duniani.
 
Lugha yetu ya taifa ni kiswahili. Kiingereza ni lugha ya biashara ya kimataifa.
Sio lazima kila mtu ajue kiingereza .
Kama swala la wageni sisi tunatembelewa na wageni toka mataifa mbalimbali kama china , ufaransa, Germany, swideni, hispania nk na haiwezekani mtu kujifunza lugha za dunia nzima.
Kuhusu wepesi wa lugha inategemeana na uzoefu kwani waweza kuta kimasai ni lugha nyepesi kuliko kiingereza.
Hukumu za mahakama zinaandikiwa Kingereza
 
unashanga mkurugenzi wa ofisi wakati rais wa China taifa kubwa duniani katika kila kitu na yeye pia hajui kingereza
Nilitaka kuandika kama wewe umeshanisaidia.Xi Jipin wa China,Putin wa Urusi wote hawa hawajui kingereza lakini mataifa yao yako juu.
 
Hakuna cha kushangaa hapo. Watanzania kwa kiasi kikubwa tunazungumza Kiswahili katika maisha yetu ya kila siku.

Ni vile tu hamjui. Kiswahili kina nguvu sana Tanzania kwa sababu ya kutumiwa katika mfumo wa elimu ya msingi.

Hata hao watoto wa medium wa day school wakirudi nyumbani wanazungumza Kiswahili, hivyo uwezo wa kuzungumza Kiingereza kwa Watanzania unaendelea kudumaa.

Waulize wazee waliosoma middle school ambavyo wanakijua Kiingereza
Kiswahili chenyewe kwa wengi bado ni tatizo mtu anasema karamu badala ya kalamu, awachezi badala ya hawachezi au ridhiki badala ya riziki.
 
Acha ubwege, nchi kama Spain, Italy, France au ukienda kusini mwa Ubelgiji, kule madaktari, wanasheria na hata wafanyakazi waserikalini hawajui kiingereza.
Uongo, hizo nchi zote raia akisoma Kingereza lazima akijue vizuri sana.
Macron anaongea Kingereza kizuri.
 
Back
Top Bottom