Tetesi: Kuna pikipiki na bajaji zinazotumia umeme wa jua. Hivi askari wa usalama barabarani wana taarifa na pikipiki hizo?

Tetesi: Kuna pikipiki na bajaji zinazotumia umeme wa jua. Hivi askari wa usalama barabarani wana taarifa na pikipiki hizo?

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
15,835
Reaction score
23,776
Katika hali isiyo ya kawaida inasemekana Jeshi la Polisi limelala usingizi wa PONO [samaki huyu hulala usingizi wiki mbili mfulilizo kwenye matumbawe].

Hali hiyo imekuja baada ya uwepo wa PIKIPIKI, VESPER NA BAISKELI za kisasa zenye kutumia umeme wa jua na umeme wa maji ambazo huchajiwa.

Swali la kujiuliza: Je, hivi pikipiki hata kama zikikugonga hazina bima wala namba, akikimbia huwezi mkamata, wanabeba mizigo na abiria kama nyingine, tatizo ni sheria ya barabarani haizitambui, sheria tuliyoridhi kwa mkoloni yaani THE ROAD TRAFFIC ACT, ambayo inaelezea chombo cha moto lazma kiwe na injini inayoendeshwa na propeller or mashine, of which hizi ni za umeme.

Rais Magufuli ana nia njema ila ana watendaji wabovu kuliko maelezo, yaani watunga sheria, ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali, jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani walipasa kuishauri serikali, WAONDOKE TU RAIS AFANYE MWENYEWE KAMA HAWAWEZI WANASHINDA MITANDAONI KUJIBIZANA KWENYE MITANDAO YA NGONO KWA WIFI YA BURE HUKO MAWIZARANI.

Serikali inakosa mapato mengi kwakuwa hivi vyombo vingesajiliwa vingeingiza mapato kwa taifa.

A.jpeg
A.jpeg

AA.jpeg
AAAA.jpeg
AAA.jpeg



B
 
Hawajalala make wiki jana wamenilamba 30,000 kisa jamaa hakufunga mkanda ni nilimchukua mita moja kutoka pale walipo nikawa sijamcheki kama hajafunga mkanda. Tene siku hizi kila afande ni tajiri, akichomoa waleti yake kama saa mbili za usiku, inachenji chenji nyingi kupita mmiliki wa duka.
 
Hauoni kuwa hizo sheria zimepitwa na wakati zinapaswa kubadilishwa na kuvitambua hivyo vyombo vya usafiri ? Teknolojia imebadilika na wao wanapaswa kubadilika.
Ndiposa mjue tunalipa watu mishahara wamelala tu maofisini.
Tunahitaji watu wenye kuona mbali, wanasheria wenye weeledi sio wavaa suti za kubana huku kichwani hakuna kitu
 
haswa hizi pikipik za umeme ndo zimejaa mjini balaa na speed yake kama pkpk zinazotumia mafuta tu, nadhani sheria ibadilishwe.
 
Hawajalala make wiki jana wamenilamba 30,000 kisa jamaa hakufunga mkanda ni nilimchukua mita moja kutoka pale walipo nikawa sijamcheki kama hajafunga mkanda. Tene siku hizi kila afande ni tajiri, akichomoa waleti yake kama saa mbili za usiku, inachenji chenji nyingi kupita mmiliki wa duka.
Kama kweli ulicho andika ni sahihi, Kuna tatizo kubwa. Hizo pikipiki huku mikoani zina zaidi ya miaka 3! Kumbe hazisajiliwi? Mamlaka husika zipo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio sawa kuwazuia au kuchukua rushwa kwa vyombo vya Moto Kama hivyo... Tena walitakiwa wapongezwe kwa kutumia nishati mbadala inayotunza mazingira na umeme watanunua wa tanesco sio mafuta ya Saudi Arabia..
Wakati wanapongezwa wasajiliwe, walipe kodi
 
Ni kweli, The Road Traffict Act ya TZ inaongelea Self-Propelled Vehicles tu. Nchi kama India walishafika mbali sana kwao zilianza na Insurances then baadae watu wa mazingira wakawatetea ambapo bima yao inalipwa na common fund kama zilivyo Hit-And-Run Insurances za India


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Guta linabeba mzigo sawa na Suzuki Carry na lipo hatarishi zaidi lkn halikamatwi na traffic kwa sababu sheria ipo kimya


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Watanzania ni watu kwenye roho mbaya,mada kama huzi huezi kuzikuta Nigeria,Burundi au hata Kenya,hizi ni roho za kichawi,nashukuru mungu baba yangu alikufa miaka mingi iliyopita kabla ya kizazi hiki ni aibu kuishi Na watu kwenye roho ya wivu kiasi hiki,mwenye ile Pikipiki Na mweye baiskeli yupi rahisi zaidi kukimbia, every little thing you do to progressive, none ambitious people crush it.them nuh have no ambition at all

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom