#COVID19 Kuna siku Watanzania watapanga foleni za kilomita kadhaa ili kuchanja

#COVID19 Kuna siku Watanzania watapanga foleni za kilomita kadhaa ili kuchanja

Kwa hali ninavyoiona ya hii Korona kuondoka na watu, kuna siku watanzania watapanga foleni za kilomita kadhaa ili wapate chanjo.

Nilienda kupata chanjo siku ya jumanne. Nilikuwa niko peke yangu na mtoa chanjo. Tulizungumza mambo kirefu sana. Nilikaa pale kama nusu saa hivi. Mbaya zaidi wafanyakazi wa afya wengi sana nao wanakwepa kuchanja. Jamaa fulani alinipa uchambuzi kuwa wafanyakazi wengi wa afya kinachowafanya wasichanje ni uoga wa sindano!!

Kingine nilichokiona, unapewa cheti cha mkononi na kingine unaweza download. Inaonekana kama umedhamiria kutochanja ila unataka upate cheti, unaweza 'ukachonga' na mtoa chanjo ukapata cheti.

Mbaya zaidi serikali nayo imechukulia mzaha hili suala. Gwajima, Dr anaenda kumpa Steve Nyerere ubalozi wa chanjo. Ataelimisha nini watu juu ya chanjo?

Siku inakuja watu watapanga foleni za kilomita kadhaa ili kupata chanjo
Labda chanjo ya UKIMWI ila sio hii ya mafua
 
Nikuulize, hiyo chanjo ni kwa ajili ya variant ipi ya Corona, na kikija variant mpya je?

Nikuulize, ukishachanja, unaacha kuvaa barakoa, unaweza kujichanganya na watu, unakuwa huwezi kuambukizwa, kuambuzi wengine , kuugua na kufariki kwa Corona?

Side effects za muda mfupi, wa kati ma mida mrefu wa hizo chanjo ni zipi?
Tushazisikia sana hii gonjera, nenda kawaimbie watoto. Ni ushauri tu. Otherwise you are just wasting your time.
 
Utungaji huu, wengi wameanzisha uzushi kama huu. Mtaani kwetu hivi, kule vile. Umesikia chanjo inaweza sababisha kuganda damu unaamua kutunga "mtaani kwetu."
Ila mtu akisema mtaani kwao kila siku watu wanakufa na corona unaamini.
 
Kwa hiyo vifo vya 3% kwa aiborne disease unaona si kitu. Pengine labda sijui lengo lako. Wewe unapinga chanjo sababu ugonjwa umekuzwa?
Issue ya ugonjwa kukuzwa hilo ni jambo moja na kuhusu hizi chanjo za majaribio ni suala lengine pia. Wewe hujui hofu iliyotengenezwa kwenye corona imechangia kuleta athari kwa kiasi gani.
 
Yap, wengi wazushi. Hawajui hata kwanini hawataki kuchanja. Wanaamua kuunda hadithi.
Tatizo mi wewe ambae unachagua katika hizo hadithi ni zipi uzisikilize kwa sababu ndio unachotaka kusikia na zipi hutaki kusikiliza kwa sababu si unachotaka kusikia, leo akija mtu akisema tu mtaani kwao kila siku wanazika watu kwa corona basi hutomuona mzushi wala hutomuhoji kajuaje kuwa hivyo vifo vyote ni vya corona.
 
Tatizo mi wewe ambae unachagua katika hizo hadithi ni zipi uzisikilize kwa sababu ndio unachotaka kusikia na zipi hutaki kusikiliza kwa sababu si unachotaka kusikia, leo akija mtu akisema tu mtaani kwao kila siku wanazika watu kwa corona basi hutomuona mzushi wala hutomuhoji kajuaje kuwa hivyo vifo vyote ni vya corona.
Wapinga chanjo hawataki kukubali ushahidi wa wazi kuwa chanjo inasaidia. Wanatunga stori mbadala kuonyesha kuwa chanjo inaua.
 
Kwa hali ninavyoiona ya hii Korona kuondoka na watu, kuna siku watanzania watapanga foleni za kilomita kadhaa ili wapate chanjo.

Nilienda kupata chanjo siku ya jumanne. Nilikuwa niko peke yangu na mtoa chanjo. Tulizungumza mambo kirefu sana. Nilikaa pale kama nusu saa hivi. Mbaya zaidi wafanyakazi wa afya wengi sana nao wanakwepa kuchanja. Jamaa fulani alinipa uchambuzi kuwa wafanyakazi wengi wa afya kinachowafanya wasichanje ni uoga wa sindano!!

Kingine nilichokiona, unapewa cheti cha mkononi na kingine unaweza download. Inaonekana kama umedhamiria kutochanja ila unataka upate cheti, unaweza 'ukachonga' na mtoa chanjo ukapata cheti.

Mbaya zaidi serikali nayo imechukulia mzaha hili suala. Gwajima, Dr anaenda kumpa Steve Nyerere ubalozi wa chanjo. Ataelimisha nini watu juu ya chanjo?

Siku inakuja watu watapanga foleni za kilomita kadhaa ili kupata chanjo
Haiwezi kutokea kwa sababu si kila anayeambukizwa anakufa au kuugua
 
Variants ni nyingi. Ikitokea variants ambayo haisikii hii chanjo ya J&J ntaenda tena kuchanja. Na ntaendelea kujikinga na Corona sababu kuna variants zingine na chanjo siyo 100%
Sawa, utaendelea kuchanja tena na tena na tena na tena na tena hadi utakapokufa au sio?

Na vipi kuhusu kama utakapoachanja, utaacha kuvaa barakoa, utaweza kujichanganya, hautagua, hautaambukizwa, hautaambukiza wengine na hutakufa kwa Corona?

Na je kuhusu side effects zake za muda mfupi, muda wa kati na za muda mrefu, ni zipi?
 
Nikuulize, hiyo chanjo ni kwa ajili ya variant ipi ya Corona, na kikija variant mpya je?

Nikuulize, ukishachanja, unaacha kuvaa barakoa, unaweza kujichanganya na watu, unakuwa huwezi kuambukizwa, kuambuzi wengine , kuugua na kufariki kwa Corona?

Side effects za muda mfupi, wa kati ma mida mrefu wa hizo chanjo ni zipi?
Team samia huyu hawezi kukujibu atapita kama hajaona
 
Back
Top Bottom