#COVID19 Kuna siku Watanzania watapanga foleni za kilomita kadhaa ili kuchanja

#COVID19 Kuna siku Watanzania watapanga foleni za kilomita kadhaa ili kuchanja

Kwa hali ninavyoiona ya hii Korona kuondoka na watu, kuna siku watanzania watapanga foleni za kilomita kadhaa ili wapate chanjo.

Nilienda kupata chanjo siku ya jumanne. Nilikuwa niko peke yangu na mtoa chanjo. Tulizungumza mambo kirefu sana. Nilikaa pale kama nusu saa hivi. Mbaya zaidi wafanyakazi wa afya wengi sana nao wanakwepa kuchanja. Jamaa fulani alinipa uchambuzi kuwa wafanyakazi wengi wa afya kinachowafanya wasichanje ni uoga wa sindano!!

Kingine nilichokiona, unapewa cheti cha mkononi na kingine unaweza download. Inaonekana kama umedhamiria kutochanja ila unataka upate cheti, unaweza 'ukachonga' na mtoa chanjo ukapata cheti.

Mbaya zaidi serikali nayo imechukulia mzaha hili suala. Gwajima, Dr anaenda kumpa Steve Nyerere ubalozi wa chanjo. Ataelimisha nini watu juu ya chanjo?

Siku inakuja watu watapanga foleni za kilomita kadhaa ili kupata chanjo
Israeli wamechanja kuliko ncho yoyote duniani. Lakini ndio wanapigwa na korona kuliko nchi zingine. Hivi sasa wanaongelea kuchoma booster ya nne.

SWALI ni kuwa, je, kinachowasumbua ni korona kweli au ni hizo chanjo?

Hiki ndicho kitakachotokea kwetu. Kadiri wanaochanjwa wanavyoongezeka, na wagonjwa nao watakuja kuongezeka. Halafu tutaambiwa kovidi imeongezeka. Kwa sababu ya hofu, wasiojua kinachoendelea ni kweli watapanga foleni. Hapo ndipo tutakuwa tayari tumeingia kwenye mtego uliosetiwa, ambao hivi sasa unatenda kazi israeli, uingereza nk.
 
Tumekuwa na Tatizo Kuu la kutaka Kusikia Unachokitaka au Kuona na Kifanywe Unachokitaka Mhusika na sio Uhalisia. Wewe ukitaka kukubali kubali, usipotaka acha. Juzi nipo ofisini, kuna jirani yangu hakuwa amefungua ofisi yake, nikampigia kumuuliza kama atakuja akaniambia hana uhakika sababu walikuwa kwenye mazishi ya jirani yao. Picha nzima ikapatikana jana, kumbe aliyefariki aliwahi kuchanjwa! Baada ya muda maradhi yakawa yanapishana pishana hayamkauki, Jumanne hali ikawa tata akaaga dunia. Hapo Jeshi la Wokovu tena Kurasini nikakutana na same stori ukiachana na za huku mtaani kwetu. Wewe endelea kubisha, hakuna wa kubishana na wewe.
Nyingi ni stori tu. Ukiangalia percent ya wanaoganda damu, na wewe kusema watu kadhaa mtaani kwenu tu. Haviendani. Usizushe mambo.
 
Israeli wamechanja kuliko ncho yoyote duniani. Lakini ndio wanapigwa na korona kuliko nchi zingine. Hivi sasa wanaongelea kuchoma booster ya nne.
SWALI ni kuwa, je, kinachowasumbua ni korona kweli au ni hizo chanjo?

Hiki ndicho kitakachotokea kwetu. Kadiri wanaochanjwa wanavyoongezeka, na wagonjwa nao watakuja kuongezeka. Halafu tutaambiwa kovidi imeongezeka. Kwa sababu ya hofu, wasiojua kinachoendelea ni kweli watapanga foleni. Hapo ndipo tutakuwa tayari tumeingia kwenye mtego uliosetiwa, ambao hivi sasa unatenda kazi israeli, uingereza nk.
Chanjo imepunguza sana vifo Israeli. Ripoti moja ilionyesha kuwa kwa idadi sawa ya wagonjwa vifo vilitoka 101 hadi 25.
 
Ndio maana mapema kabisa nikakuambia kuwa wewe tayari una majibu yako na unataka kila atakayechangia apite kwenye majibu au mawazo uliyonayo.
Kuna fact za kisayansi zipo wazi. Zinaonyesha incidences za kuganda damu zipo kiasi gani. Sasa mtu kusema watu kadhaa mtaani kwake wamepatwa na hiyo kitu ni uzushi na hearsay. Uzushi juu ya chanjo ni mwingi sana. Mnazusha ili kulisha mtazamo wenu.
 
Kucheza bila mashabiki maana yake nini?

Sasa kucheza pasipo mashabiki ndio ina maana wasiochanjwa hawaruhusiwi uwanjani?

Ingekuwa kuna wanaoruhusiwa (walio chanjwa) na wanaozuiwa (wasiochanjwa) mfano wako ungekuwa sahihi...

Udhibiti wa mikusanyiko isiuo ya lazima hauna mahusiano na kuchanja au kutochanja...
 
Mi nimechanja lakini kitoto changu kichanga sitaki kichanjwe! Kuna nesi hapa amenivuta sikio niwe makini.

Naona hakuna muitikio wa chanjo kwa watu wazima wanaamua kuipunguzia kwa vitoto huko leba
Manesi hawahawa wa Kibongo unawaamini!? Za kuambiwa changanya na za kwako.
 
Sasa kucheza pasipo mashabiki ndio ina maana wasiochanjwa hawaruhusiwi uwanjani?

Ingekuwa kuna wanaoruhusiwa (walio chanjwa) na wanaozuiwa (wasiochanjwa) mfano wako ungekuwa sahihi...

Udhibiti wa mikusanyiko isiuo ya lazima hauna mahusiano na kuchanja au kutochanja...
Kuna level ya chanjo inatakiwa. Mfano nchi za Ulaya baada ya karibu watu zaidi asilimia 60 kuchanjwa, mashabiki wameruhusiwa viwanjani.
 
So una ukweli kuwa chanjo hazisaidii kitu?
Wa kutosha sana. Jambo la kwanza kabisa, ukishaita hizi ni chanjo, unakuwa umeshatekwa. Bila kutambua ukweli kwamba hizi si chanjo, utazidi tu kuongea kana kwamba unatetea chanjo. Hizi si chanjo. Hizi ni gene therapy ambazo lengo lake

1. Kupunguza watu duniani.
2. Kusajili watu wote duniani kwenye database (Ndio maana WHO wameanza kuleta maelekezo ya namna ya kusajili watu. Unaweza kusoma hapa: Digital documentation of COVID-19 certificates: vaccination status: technical specifications and implementation guidance, 27 August 2021
Na hapa WHO inatumiwa tu lakini wahusika ni bill gate, WEF, na globalists wengine.
3. Kufanya transhumanism - yaani kuwageuza watu kuwa version ya Human 2.0

Kwa kifupi ulimwengu unaswagwa kama ng'ombe wanaoingizwa kwenye josho. Soon ulimwengu utajikuta umeingizwa kwenye tight spot ambayo kutoka haitawezekana.

Mimi nakupa challenge hii.
Kama unapenda kweli tuongee jambo hili, mimi niko tayari kwenda step by step, tuanzie mwanzo hadi tufike hapa tulipo.

Maana hapa nakatakata tu vitu.

Hiki kiitwacho chanjo ni part tu ya mega-scheme.

Lakini wengi wanatazama tu chanjo-kovid - chanjo-covid.

Do you know the bigger picture?
 
Wa kutosha sana. Jambo la kwanza kabisa, ukishaita hizi ni chanjo, unakuwa umeshatekwa. Bila kutambua ukweli kwamba hizi si chanjo, utazidi tu kuongea kana kwamba unatetea chanjo. Hizi si chanjo. Hizi ni gene therapy ambazo lengo lake

1. Kupunguza watu duniani.
2. Kusajili watu wote duniani kwenye database (Ndio maana WHO wameanza kuleta maelekezo ya namna ya kusajili watu. Unaweza kusoma hapa: Digital documentation of COVID-19 certificates: vaccination status: technical specifications and implementation guidance, 27 August 2021
Na hapa WHO inatumiwa tu lakini wahusika ni bill gate, WEF, na globalists wengine.
3. Kufanya transhumanism - yaani kuwageuza watu kuwa version ya Human 2.0

Kwa kifupi ulimwengu unaswagwa kama ng'ombe wanaoingizwa kwenye josho. Soon ulimwengu utajikuta umeingizwa kwenye tight spot ambayo kutoka haitawezekana.

Mimi nakupa challenge hii.
Kama unapenda kweli tuongee jambo hili, mimi niko tayari kwenda step by step, tuanzie mwanzo hadi tufike hapa tulipo.

Maana hapa nakatakata tu vitu.

Hiki kiitwacho chanjo ni part tu ya mega-scheme.

Lakini wengi wanatazama tu chanjo-kovid - chanjo-covid.

Do you know the bigger picture?
Hii ni paranoia, ni dalili ya kichaa.
 
Back
Top Bottom