#COVID19 Kuna siku Watanzania watapanga foleni za kilomita kadhaa ili kuchanja

Naona mvutano, waliochanja wanasubiri wasiochanja wafe na wasiochanga wanasubiri waliochanja wafe. Labda ngoma drawal.
 
Majibu umeyaqoute hapo juu halafu unauliza. Madhara ya chanjo hii yameelezwa sana. Siwezi kuyaorodhesha hapa maana ni mengi ma iana ya xhanjo ni nyingi.
 
Sio kweli, mliochanjwa mmeshaingia chaka, shauri yenu na endeleeni kusubiria matokeo!
Utavuna ulichopanda, maamae zenu
 
Mkuu sasa mbona unarudia ya Gwajima? Wapumbavu huwa hawaelimishwi achana nao!
 
Ni vigumu sana kuwaokoa watu ambao ni mind controlled...hili zoezi la microchopping world wide linakwenda kuleta catastrophy kwa wote waliojipeleka kupata Jab..
Hii ni agenda ya kina Bill Gates na Gates pia anatumika, the Hidden Master mwenye kutoa utajiri kwa wanaomcha ndo mwenye true agenda.
 
Majibu umeyaqoute hapo juu halafu unauliza. Madhara ya chanjo hii yameelezwa sana. Siwezi kuyaorodhesha hapa maana ni mengi ma iana ya xhanjo ni nyingi.
Sawa, na ukizingatia chanjo moja ni kama elfu 50 hivi, na tuko milioni 50, halafu tuwe tunachanjwa kila baada ya miezi kadhaa, safi sana.
Haya; tuendelee...
Madhara ya muda mrefu (miaka 10) , utafiti wake ulifanyika kuanzia mwaka gani hadi mwaka gani ili kuyaestablish? Na ni yapi?

Na je, ukichanjwa unakuwa hauwezi kuambukizwa, kuambukiza wengine, kuugua , na kufariki kwa Corona? Unakuwa huna haja ya kuvaa barakoa, kuepuka mikusanyiko na kushikana mikono?
 
Unataka tusubiri miaka kumi ndipo tuanze kuchanja korona?
 
Kwamba Bill Gates ana mpango wa kuwawekea watu microchip!!!
 
Unataka tusubiri miaka kumi ndipo tuanze kuchanja korona?
Nani kasema hayo? Jibu nilichohoji, madhara yake umesema yanafahamika na yamesemwa sana. Sasa utafiti wake ukianza mwaka gani hadi mwaka gani kuweza kuestablisha hizo side effects? Na ni zipi?

Na je, ukichanjwa, unaacha kuambukizwa, kuambukiza, kuugua na kufariki kwa corona? Unaacha kuvaa barakoa, kuepuka mikunsanyiko na kushikana mikono?
 
Kwa namna speed ya waliochanjwa wanavyoondoka na maradhi hayohayo inaleta mashaka sana.

Sisi ambao tunajikinga na kuchukua hatua zote za tahadhari nahisi tupo salama zaidi kuliko waliochanjwa.

Nimeona kulikuwa na mjadala wa ClubHouse ulioendeshwa na Maxence Melo kuhusu chanjo ya uviko ambapo wasemaji wakuu naona karibia wote walikuwa wameshapokea chanjo lakini zaidi ya takwimu zenye kushawishi hofu sikupata analytical points zinazotetea uhakika wa chanjo.
Nilikuwa tayari nimeshafanya booking kupata chanji nilihairisha baada ya watu wawili wa karibu yangu walifariki kwa matatizo ya Uviko ilihali walishapata chanjo.

Pamoja na ubinadamu wa mwendazake lakini alitujengea ujasiri kwa kuondoa hofu lakini kujilinda na hili dude.

Zachary Hanspope amesemekana amefariki kutokana na matatizo haya haya lakini ni miongoni mwa wiopata chanjo. Tunajua kupata chanjo siyo guarantee ya kutopata UVIKO lakini hata ukiupata kunakuwa na chances kubwa za kupona kuliko ambaye hana chanjo.

Kisichosemwa mitandaoni kwa sasa ni kwamba, watu wanapata sana corona lakini wanajitibu kwa njia zilezile walizotumia 2020. Haisemwi kwa sababu itawaumbua wakubwa lakini italeta taharuki zaidi na isije ikatengenezwa zengwe kuleta chanjo demand.
 
Mi nimechanja lakini kitoto changu kichanga sitaki kichanjwe! Kuna nesi hapa amenivuta sikio niwe makini.

Naona hakuna muitikio wa chanjo kwa watu wazima wanaamua kuipunguzia kwa vitoto huko leba
Mkuu imekaaje hii?
 
Hilo swali la pili nimeshakujibu. Hutaki tu kuelewa. Nimekujibu kwenye jibu la kwanza kabisa. Kuhusu madhara. Chanjo hii, J&J ni aina ya Viral vector. Virusi waliopunguzwa nguvu au kufa. Chanjo ya namna hii inatumika miaka na miaka. Ingridients ni zilezile. Kilichobadilika hapo ni badala ya kumuweka kirusi wa polio au ndui aliyekufa wanamuweka kirusi wa Corona. Na madhara ya kirusi wa korona aliyekufa au aliyepungua nguvu yanafahamika.

Tech imekuwa. Data ni nyingi. Huhitaji miaka kadhaa kujua madhara ya dawa/chanjo.
 
Kwanza ufahamu kuwa ukipata chanjo baada ya kupata Corona haitakusaidia. So usishangae sana mtu kupata chanjo na kufa. Na chanjo inachukua wiki zaidi ya mbili kujenga kinga dhidi ya corona.

Pia nikwambie tu. Corona imeonyesha kuwa mortality rate ni kama 3%. Hivyo kama katika watu mia walioumwa, ni watatu tu wanakufa. Hivyo huwezi kusema njia za 2020 zinafanya kazi bila utafiti wa kina wa kisayansi. Je kuna waliotumia njia za 2020 na wakafa?
 
Ndio nikauliza, hayo madhara ya kirusi cha Corona yanayofahamika, utafiti wake hadi kuyafahamu, ulianza kufanyika kuanzia mwaka gami hadi mwaka gani? Na ni yapi? (Kirusi cha Corona ninachozungumzia ni cha Covid19)

Na je, ukichanjwa unakuwa hauwezi kuambukizwa, kuambukiza, kuugua na kufariki kwa corona? Unaacha kuvaa barakoa, kuepuka mikusanyiko na kushikana mikono? (Jibu la kwanza linajibu vipi haya?)
 
Kuna jamaa yangu alikuwa mbishi Sana akawa anasema Corona haipo ni siasa tu so sad tumemzika mwezi uliopita kwasababu ya COVID-19 alikuwa mtu mwema na muhimu Sana kwangu [emoji24][emoji24][emoji24]

Sent from my TECNO B1f using JamiiForums mobile app

Siku yake ilifika. Hakuna Corona haipo ni Propaganda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…