Tetesi: Kuna Tetesi za kufanyika mabadiliko ya Utawala Zanzibar

Tetesi: Kuna Tetesi za kufanyika mabadiliko ya Utawala Zanzibar

Zbar kwa Wa Zbar...waelewane nchi isonge mbele......!!! Tuwatakieheri......amaniitawale ndani nchi yao......wenye haki wapewe haki pia !!! Wafanye mseto milele....kila uchaguzi waangalie nani ana nyingi....aongoze nchi mwingine Makamu!!! Tuwaaachie
Wavunje vyama vyao vya asili ili watengeneze chama kipya chenye muunganiko wa CCM/CUF.
 
Sijashika bango. Hii tetesi isikutoe udenda. Chukulia ni tetesi tu.
Mkuu usibishane na huyoo...waga anajifanya mtabiri ,alitabiri kitu kibaya sana juu ya MTU fulani lkn haikutokea,akaukimbia uzi wake.
So in short, jamaa anajifanya kuwa na taarifa fulani kumbe ni popoma kabisaaa....
 
Kuna tetesi zinaendelea kuzagaa kule Zanzibar kuhusu kufanyika mabadiliko ya Utawala . Taarifa zinasema kunatarajiwa kuwa na serikali ya umoja wa kitaifa hivi karibuni zitakazowashirikisha CCM na CUF.

Vyanzo vyetu vinadokeza kumekuwa na usiri mkubwa wa jambo hili baina ya pande mbili na usiri wa walio nyuma ya mpango huo zikihusishwa jumuiya za kimataifa kwa kushirikiana na mamlaka za ndani.

Siku za hivi karibuni kwa upande wa CUF, viongozi wa Zanzibar wamezidisha juhudi za kuwaeleza wanachama wao kile wanachokiita haki yao na kutumia kurugenzi zao za uchaguzi na usalama na ulinzi kuzunguka wilaya zote za Zanzibar kuwatayarisha kupokea mabadiliko. Kuna vikao vingi vya ndani vimefanyika na hadi kufikia kuwaarifu kujiandaa kupamba.

Na kwa upande wa CCM kuna taarifa za kuwa na vikao vingi ingawa usiri umezidi juu ya kile hasa kinaendelea.

Tetesi hizi zilizidi baada ya Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif kuarifu kwamba alitarajia isingezidi miezi mitatatu kutoka Agosti 2017 kwamba haki ya wazanzibari ingepatikana ingawa iliarifiwa baadae kwamba siku zilisogea na kusogezwa mbele.

Kinachoendelea sasa ni ukimya na minongono mingi katika vounga vya Zanzibar bila ya kuonekana dalili yoyote ya matayarisho ya mabadiliko.


Wenye taarifa tunaomba ufafanuzi.


Kishada.
Hizo ndoto zako una ota mchana Lazima washughulikie Tatizo la Bara kwanza
 
kuna muda maalum wakujua lini zitakuwa habari kamili....?
 
Ni kwa nafasi ya makamu wa rais tu au na baraza la wawakilishi?
 
Kuna tetesi zinaendelea kuzagaa kule Zanzibar kuhusu kufanyika mabadiliko ya Utawala . Taarifa zinasema kunatarajiwa kuwa na serikali ya umoja wa kitaifa hivi karibuni zitakazowashirikisha CCM na CUF.

Vyanzo vyetu vinadokeza kumekuwa na usiri mkubwa wa jambo hili baina ya pande mbili na usiri wa walio nyuma ya mpango huo zikihusishwa jumuiya za kimataifa kwa kushirikiana na mamlaka za ndani.

Siku za hivi karibuni kwa upande wa CUF, viongozi wa Zanzibar wamezidisha juhudi za kuwaeleza wanachama wao kile wanachokiita haki yao na kutumia kurugenzi zao za uchaguzi na usalama na ulinzi kuzunguka wilaya zote za Zanzibar kuwatayarisha kupokea mabadiliko. Kuna vikao vingi vya ndani vimefanyika na hadi kufikia kuwaarifu kujiandaa kupamba.

Na kwa upande wa CCM kuna taarifa za kuwa na vikao vingi ingawa usiri umezidi juu ya kile hasa kinaendelea.

Tetesi hizi zilizidi baada ya Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif kuarifu kwamba alitarajia isingezidi miezi mitatatu kutoka Agosti 2017 kwamba haki ya wazanzibari ingepatikana ingawa iliarifiwa baadae kwamba siku zilisogea na kusogezwa mbele.

Kinachoendelea sasa ni ukimya na minongono mingi katika vounga vya Zanzibar bila ya kuonekana dalili yoyote ya matayarisho ya mabadiliko.


Wenye taarifa tunaomba ufafanuzi.


Kishada.
Hahahaa ulishaleta habari nne hapa ya kuwa mtakabidhiwa serikalini karibuni..na zote nilikuambia uwache kuwadanganya watu.. la leo naona umekuja na habari tofauti kidogo na zilizopita kwa kusema serikali ya umoja wa kitaifa.Inawezekana una nia nzuri kwa wafuasi wako ya kuwa hutaki uwape habari moja kwa moja ya kuwa musubiri uchaguzi au mnavuta muda kwani mmeshawadanganya sana kwa kwa upumbavu wao wamewaamini sana then kuwapa habari ya hafla tu ya kuwa sefu amepwerewa na hakuna kitu kwani uwongo wake umefikia tamati unaweza kuwauwa watu.. then kuwazoesha kwa kuwaambia kutakuwa na serikali ya umoja wa kitaifa na baada wala realize wenyewe jinsi walivyokuwa wapumbavu

Pole sana
 
Mazungimzo ya hali ya juu kabisa yapo na hatua ya mwisho ilikuwa ni kuhakikiwa zile kura za raisi zilizobakia kutangazwa katika uchaguzi wa 25 Oct 2015.

Kinachozuwia implementation ni masharti ambayo CCM hawayakubali kwa sababu ya aibu watakayoipata na sio jengine. Wako tayari kumpa seat yake ya VP1 ambayo mpaka sasa iko vacant. Mind you, vyama vidogo vilipoingia kwenye uchaguzi wa marejeo waliahidiwa atakayetokea wa pili kwa wingi wa kura atakuwa VP1 na ndio maana wakatumia nguvu zote kuhalalisha the rerun.

Masuauala ya kujiuliza mimi na wewe ni mengi lakini tujiulize suala moja tu

1. Kuna VP2 sasa hicho kiti cha VP1 kaekewa nani wakati uchaguzi wa pili umeisha na washindi wameshapatikana? Kama hakuna VP1 ina maana mpaka sasa hivi serikali haijakamilika kwa miaka 2 sasa na ina run kwenye stand by mode!
 
maadamu imesemwa humu kwenye jamii forum basi jambo hilo linaukweli maana hata ya Nyarandu yalianza kusemwa humu
 
Zanzibar nako wanataka nusu Mkate?
 
Hao CUF wasubiri tu hd 2020,hakuna mabadiliko yoyote nje ya sanduku la kura..!!
 
Napinga vibaya sana kushirikiana na ccm , lakini naiheshimu sana katiba ya Zanzibar ili nisiwe kama Jecha
 
Mzigo wa dripu ushasambazwa kwenye maskani...... Kipindi product iliadimika, lakini tayari imepatikana kwa bei nafuu sasa.
Haya wacha waendelee kununua dripu ikifika 2020 ndio watajua.
 
Wikiendi iliyopita Naibu katibu Mkuu wa CUf Zanzibar alinukuliwa akiwachallenge viongozi wa CCM waje hadharani kama afanyavyo Maalim Seif wakane kama hakuna kitu cha namna hiyo.

Wenye taarifa rasmi twambieni.
Kutokuja hadharani kupinga anayoyasema Seif haimaanishi kuwa ni kweli anachosema Seif. Kumbuka, Wanae tangu 95 wakimchezea ndevu, anaejihangaisha ni yeye Maalim kukaa hadharani akiwaahidi watu. CCM hawana haja ya kumjibu mana ata wakimjibu watapata nini?
 
Back
Top Bottom