Kuna ubaya gani kwa serekali yetu kulitwaa eneo la vingunguti na kujenga makazi ya kisasa

Crocodiletooth

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2012
Posts
20,561
Reaction score
24,428
Ipo haja ya serekali yetu kuona umuhimu wa suala hili, kwa ni eneo ambalo lipo kilometre chache sana kutoka city center, linastahili kuwa upgraded n kufanana na maeneo ya upanga na kwingineko, pia ni eneo ambalo linaeweza kupangwa tukapata kariakoo 2,mpangilio wa ujenzi ufanywe kwa wenye maeneo yao mradi utakapomalizika wapatiwe nyumba zao permanent na hati zao.
 
Kilichofanyika Magomeni Kota inabidi iwe mwongozo. Kama waliweza kuvunja zile nyumba na wakajenga za kisasa na wakazi wa awali wakapata nyumba basi inawezekana kufanya kwingine.
 
Mzee Matola umenikumbusha Kigamboni satellite city, viwanja viliuzwa sana.
Kigamboni satellite city haijawahi kujengwa wala kuuzwa viwanja. Ule ulikuwa mradi ambao ungeondoka makazi holela maeneo ya Vijibweni (sehemu nzuri sana,location,lakini imejengwa holela). Wakazi wa eneo hilo wangepewa nyumba kama walivyofanya Magomeni Kota. Ni location nzuri sana ila imegeuka slum.
 
Haisee yapo magorofa mengi kweli njia ya kuelekea mwembemdogo magenerator ma concrete mixer yametelekezwa pale haisee sijui nani aliukwaza mradi ule ambao ungekamilika unge kuwa na tija sana japo kwaukweli kigamboni sipapendi kwa moyo wangu wote!
 
Mzee Matola umenikumbusha Kigamboni satellite city, viwanja viliuzwa sana.
Sijui kwa Nini Nina hamu Sana ya kumuona nzi, kiroboto, kunguni na chawa na macho Yangu mwenyewe naked eyes na isiishie hapo tu ning'atwe nao I feel the experience. Hapa nilipo Malibu hayapo haya madudu. Hata kwenye apartments zangu zingine Beverly Hills, Manhattan, Zurich na Geneva hayapo pia. Na uhakika hapo Kigamboni satellite city yatakuwepo tu am pretty sure believe me.
 
Chalii angu njoo pande za Ambureni, Imbaseny,Kikatiti,Kikwe,King'ori ujionee miujiza 😄😄
 
Ujenzi wetu wenyewe tunajitengenezea slams

Ova
 
10% wakihakikishiwa washika dau mbona hilo linawezekana fasta tuu
 
... pabaki hivyo hivyo. Vingunguti na Kiwalani ndio malango ya wageni kuingilia nchini; ndege ni almost zinakuwa zimekaribia kugusa bati za mbanda ya maeneo hayo ambayo yanakuwa yanaonekana kwa uwazi kabisa kutokea juu angani.
 
Maeneo yote ya slums dsm yangevunjwa zikajengwa gorofa kama za magomeni kota..hizi slumz zina haribu sana hadhi ya huu mji.

#MaendeleoHayanaChama

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Haisee yapo magorofa mengi kweli njia ya kuelekea mwembemdogo magenerator ma concrete mixer yametelekezwa pale haisee sijui nani aliukwaza mradi ule ambao ungekamilika unge kuwa na tija sana japo kwaukweli kigamboni sipapendi kwa moyo wangu wote!
Mi napapenda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…