Kuna ubaya kununua nyumba ya jirani inayopigwa mnada na benki?

Kuna ubaya kununua nyumba ya jirani inayopigwa mnada na benki?

Nunua ila usiende mwenyewe . kafungue company, register kila kitu , nenda kwa wakili akafanye yeye ule mchakato , gharama itazidi kidogo ila itakupa privacy in that ile kampuni ndiyo itappear on paper ila nyuma nyuma ww ndie mmiliki
 
BUSARA NI KUTOINUNUA.
Kwa sababu jirani yako hapo yupo amepata matatizo ni matatizo kama msiba au huzuni.

Sasa wewe kama jirani au uliyekuwa jirani yake inatakiwa uonyeshe hisia za kuonyeshwa kuguswa sympathy kusikitika pamoja,kumfariji,kulia naye pamoja ndio UTU,au ubinadamu,au good morals na hasa kwa jamii zetu sisi watanzania tunaishi kijamaa bado tuna elements za kijamaa.
Hata kama hujahuzunishwa na yaliyompata jirani yako unaweza kuigiza kumsikitikia na kumpa pole au kumfariji hata kwa kuigiza.

Pia uki inunua bado kumbukumbu za jirani yako na pengine na yeye ataweza kufikiri,umetumia ule msemo wa KUFA KUFAANA,au umetake advantage au ulikuwa unaitamani au umefurahia matatizo yake.Sidhani kama yeye jirani yako atafurahia hilo.Kwa sababu hakupenda iuzwe au haiuzi kwa ridhaa yake au kupenda au kwa kupanga.Ila inauzwa na BANK kwa kushindwa kurejesha mkopo(MATATIZO/CHANGAMOTO AMEPATA AU MAJANGA).Ni tofauti na kama yeye mwenyewe angeamua kuuza kwa kupenda.

UKIACHA BUSARA
,KISHERIA SIO KOSA,WALA HAKUNA MADHARA YOYOTE UKINUNUA.
Lakini mpaka umeamua kuuliza huku JF ina maana uko dilemma au kuna nafsi inakwambia usinunue nafsi nyingine inakwambia nunua.Ila maamuzi au umeshachagua upande moyoni mwako wa kununua au kutonunua,hapa unatafuta pengine justification au support ya kufanya kile ambacho umeshakiamua moyoni mwako.Fanya kile ambacho moyo wako utakuwa na amani na furaha,kadiri ya imani yako na utu wako na mahusiano yako na jamii yako.
Ni kweli kabisa kwa watu wa tanzania ambao hatueleweki kama ni mabepari au majamaa.
Sena hukawii kuinunua halafu akaomba akae kidogo na ukigoma utaonekana una roho mbaya
 
Inunue, halafu unamrudishia huyo jirani yako hiyo nyumba yake kwa makubaliano ya kukurejeshea hela yako kidogo kidogo! Na huo ndiyo ujirani mwema.
Huu ushauri ni mzuri sana ,na kama utapata neema na imani ya kuutekeleza.Basi utakuwa umefanya jambo lenye baraka,utampendeza Mungu pia utampendeza jirani yako na jamii.Mungu atakubariki,hata jirani atakuombea mema na baraka na kukushukuru,pia atamshukuru Mungu kwa ajilii yako.
Na ndio namna ya kuishi kwa upendo ambao Mungu anatufundisha,na dini zote zinatufundisha upendo kama huu.
 
Huu ushauri ni mzuri sana ,na kama utapata neema na imani ya kuutekeleza.Basi utakuwa umefanya jambo lenye baraka,utampendeza Mungu pia utampendeza jirani yako na jamii.Mungu atakubariki,hata jirani atakuombea mema na baraka na kukushukuru,pia atamshukuru Mungu kwa ajilii yako.
Na ndio namna ya kuishi kwa upendo ambao Mungu anatufundisha,na dini zote zinatufundisha upendo kama huu.
Hii inaweza kuleta shida zingine.. Kama alishindwa kulipa kwa wakati huko alikokopa mpaka kufikia dhamana kupigwa mnada je kwa jirani ataweza?
 
Huu ushauri ni mzuri sana ,na kama utapata neema na imani ya kuutekeleza.Basi utakuwa umefanya jambo lenye baraka,utampendeza Mungu pia utampendeza jirani yako na jamii.Mungu atakubariki,hata jirani atakuombea mema na baraka na kukushukuru,pia atamshukuru Mungu kwa ajilii yako.
Na ndio namna ya kuishi kwa upendo ambao Mungu anatufundisha,na dini zote zinatufundisha upendo kama huu.
Akikiuka makubaliano si itakula kwangu kama ameshindwa na bank kwangu si itakuwa vile vile
 
Nadhani inunue alafu umsikie huyo jirani anakuja kujaje, akiwa mjuaji endelea na maisha yako, akiwa na busara, mwambie akulipe uisitiri familia yake.

UBAYA UBWEGE
 
Nakushauri kama wewe ni mwanamme kweli,inunue nā umuombe akutafutie pesa yako taratibu hata kwa miaka mi5 umrudishie nyumba yake.
Ukifanya jambo kama Hilo litakupa heshima Hutaamini.
 
Inunue, halafu unamrudishia huyo jirani yako hiyo nyumba yake kwa makubaliano ya kukurejeshea hela yako kidogo kidogo! Na huo ndiyo ujirani mwema.
Mtu ashindwe kurejesha hela kwa benki mpaka ifikie kumtimua kwake. Ndio mtu huyohuyo aje kukulipa deni kubwa la nyumba???

Hakuna investor mpuuzi wa kufanya hivyo.
 
Nilikuwa mnunuzi mzuri sana wa vitu vya minada.. LaKini baada ya kuanza kupata majanga nikaaza kuvifuatilia baadhi.. Kwakweli niliyokuja kukutana nayo yanatisha
Kuna vitu vimefanyiwa mazindiko na mhusika akashindwa masharti na hakutengua yale mazindiko.. Ukivinunua hivi vitu vinakuja na mazindiko yake
Kuna vitu vilifanyiwa ibada za mvuto na ulinzi halafu zikafeli.. Ukivinunua vinakuja na yale maroho yanayoshindana
Kuna vitu vimefanyiwa maapizi
Kuna vitu vimefanyiwa ushirikina.. Nk
Unaponunua kitu cha mnada sometimes ikibidi pata historia yake.. Ni muhimu sana usije kubeba ama kurithi madubwana yasiyokuhusu
 
Mtu ashindwe kurejesha hela kwa benki mpaka ifikie kumtimua kwake. Ndio mtu huyohuyo aje kukulipa deni kubwa la nyumba???

Hakuna investor mpuuzi wa kufanya hivyo.
Soma vizuri kichwa cha habari. Mtoa mada ameomba tu ushauri! Kwa hiyo ungejikita zaidi kwenye kutoa maoni, badala ya kutaka kutunishiana misuli.
 
Back
Top Bottom