Hakuna kitu cha bure.
Naungana na wachangiaji waliopita waliosema ZAWADI tunazopokea nyingine zimekuwa zimenenewa./zinenuiziwa manuizo mabaya au zimelogezewa zimebeba au zimeambatanishwa na roho za uharibufu za kuzimu.
Unaweza UKATOA kitu wewe uliyetoa kama umetoa kwenye madhabahu ya shetani na mawakala wa shetani /kuzimu /ikiwemo hawa mitume na manabii wa uongo,waganga wa kienyeji washirikina wachawi mizimu majini. n.k
.ile zawadi uliyotoa kuwapatia hao watu washirikina wanaweza kuinuizia ikakudhuru mwenyewe Ukapata athari hasi au ikatambua /ikabadilisha hatima ya maisha yako wewe mwenyewe.
wengine wanaweza wakaiba hata kitu chako chochote hata bila ridhaa yako mfano nguo/viatu ,chakula chochote cha kwako hata nywele,kucha ,kivuli,unyayo,mate ,mkojo n.k na wakavitumia kukudhuru katika ulimwengu wa kiroho
Chochote kinachotoka kwako iwe umetoakwa kupenda au umepeka kwa hiyari au kimeibwa kutoka kwako kinaweza kutumiwa katika ulimwengu wa giza kukudhuru.
Kadhalika kwenye KUPOKEA unaweza ukapokea zawadi au kitu chochote kutoka kwa ufalme wa giza na washirika wa ufalme wa giza kuzimu ,ambacho kimetoka kuzimu au kimenenewa maagano mabaya kimeambatanishwa na nguvu za giza ushirikina ,UKIPOKEA TU tayari unakuwa umefungwa umenasa kwenye hayo maagano na madhabahu za kuzimu.
Na unaweza ukadhurika
TAHADHARI
Tuwe makini katika kupokea na kutoa zawadi.Hata kula kula vyakula vya watu ovyo ofa za vyakula iwe sherehe au misiba au kufuturishwa.Au kupewa kugawiwa nyama zinaweza zikawa nyama za kadara zimwfanyiwa matambiko ,ibada za kiluzimu, au kugawia watu nguo,viatu,n.k
wengi wamepata kuharibikiwa na kuingizwa katika maagano na kufanyiwa ushirikina hata kufa kwa ajili ya kutoa na kupokea zawadi.
Na kuna watu wanapenda kuwaalika watu kuwagawia vyakula vya bure na zawadi mbalimbali wakisema wanasaidia au wanafanya wema hisani kumbe wana siri nyuma ya hizo zawadi wanazigawa bure.
DAWA
Ni kusikiliza roho mtakatifu moyoni mwako kama ukiwa huna amani rohoni,nafsi ikisita kupokea au kutoa usifanye hivyo.
Vitu vingine hata ukiviombea havitakasiki mana ni vitu vilivyotoka kuzimu tayari vinamilikiwa na maagano ya kuzimu dawa ni kuviondoa .Ila ipo neema ya Mungu ipitayi neema zote inayoeweza kutusaidia.
Kusali kuomba Mungu na kuombea vitu unavyopokea unavyonunua .Mungu atusaidie kujua ,Roho mtakatifubatisaidie.HAKUNA MTUME NA NABII WA KWELI..TUJIHADHARI NA MANABII WA UONGO.