Kuna uhusiano gani wa CC za gari na ulaji mafuta?

Kuna uhusiano gani wa CC za gari na ulaji mafuta?

Jerrymsigwa

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2012
Posts
14,084
Reaction score
8,384
Wakuu ninafuatilia mtandaoni kuhusu uhusiano wa hii topic naishia kuchanganyikiwa tu. Pia nimesearch Jf bahati mbaya sijaona, ukiwa na gari ya cc1990 na ingine ya cc2700 bado the same amount of gas utatumia?

TIA
 
Ukiona gari zinatofautina engine kiasi hicho, most likely hiyo ya cc 1900 itakuwa ni ya Petrol na hiyo ya cc2700 itakuwa ni ya Diesel. Diesel ni ngumu kuwaka na haitoi moto mkali kama wa Petrol, so engine inabidi iwe kubwa ili kuweza kupata moto mkubwa wa kuzungusha engine.

Pia gari ya Diesel inaweza kuwa na engine kubwa isiyo na nguvu nyingi lakini ikawa na towing capacity kubwa, yani uwezo wa kubeba mizigo au kuvuta tela. Ndio maana gari ya diesel yenye engine kubwa unaweza ukaondokea gia namba mbili wakati gari ya petrol inakuhitaji uondokee na gear namba moja.

Gari ya Petrol inakula mafuta mengi kwa kuwa mafuta yote yanayoenda huchomwa. Nasikia gari ya diesel huwa inarudisha mafuta ili yaunguzwe raundi nyingine, sina uhakika na hili. Ngoja wataalam zaidi waje.
 
Ukiona gari zinatofautina engine kiasi hicho, most likely hiyo ya cc 1900 itakuwa ni ya Petrol na hiyo ya cc2700 itakuwa ni ya Diesel. Diesel ni ngumu kuwaka na haitoi moto mkali kama wa Petrol, so engine inabidi iwe kubwa ili kuweza kupata moto mkubwa wa kuzungusha engine.

Pia gari ya Diesel inaweza kuwa na engine kubwa isiyo na nguvu nyingi lakini ikawa na towing capacity kubwa, yani uwezo wa kubeba mizigo au kuvuta tela. Ndio maana gari ya diesel yenye engine kubwa unaweza ukaondokea gia namba mbili wakati gari ya petrol inakuhitaji uondokee na gear namba moja.

Gari ya Petrol inakula mafuta mengi kwa kuwa mafuta yote yanayoenda huchomwa. Nasikia gari ya diesel huwa inarudisha mafuta ili yaunguzwe raundi nyingine, sina uhakika na hili. Ngoja wataalam zaidi waje.

Mkuu inawezekana mengine uliyoyasema ni sahihi lakini ili la kusema gari ikiwa na Cc kubwa ni ya diesel sio kweli. Kuna magari ya diesel yana cc 2,700 na wakati huo kuna magari ya petrol yana cc 4,700, mfano VX V8. Hapo sijui unasemaje.

Tiba
 
Wakuu ninafuatilia mtandaoni kuhusu uhusiano wa hii topic naishia kuchanganyikiwa tu. Pia nimesearch Jf bahati mbaya sijaona, ukiwa na gari ya cc1990 na ingine ya cc2700 bado the same amount of gas utatumia?

TIA
Mkuu hii hutegemea mambo mengi
Ingawaje mara nyingi gari yenye cc ndogo hula mafuta kidogo zaidi ya cc kubwa

Kama gari za model na design moja basi jibu litakuwa direct kuwa cc mdogo consume less fuel than cc kubwa

Lakini kama ni magari tofauti model hapo hutegemea mambo mengi
 
Mkuu hii hutegemea mambo mengi
Ingawaje mara nyingi gari yenye cc ndogo hula mafuta kidogo zaidi ya cc kubwa

Kama gari za model na design moja basi jibu litakuwa direct kuwa cc mdogo consume less fuel than cc kubwa

Lakini kama ni magari tofauti model hapo hutegemea mambo mengi

Mkuu ungefafanua technically kabisa ili tuelewe.
Hata mimi mwanzo nilikuwa sijui maana ya cc mpaka nilipokuja kusoma kwenye mtandao. Na baada ya kusoma sijaweza kurelate cc na ulaji wa mafta maana cc maana yake kumbe ni cubic centimetre na inapimwa kuanzia pale piston inapokuwa imecmama (dead) mpaka inapo rotate hadi mwisho.
Kwa mantiki hiyo ningependa mtu anielezee kuna uhusiano gani na utumiaji wa mafta
 
nimejaribu kupitia mitandao mbalimbali sasa hivi nimegundua yafuatayo.
Fuel effieciency. Hii haina uhusiano kabisa na cc za gari bali inahusiana na ni mfumo gani gari inatumia ku inject mafta kwenye engine.
Fuel economy- hii kweli ina husiana na cc, cc kubwa ina maana gari ina engine kubwa, gari ikiwa na engine kubwa itahitaji mafta zaidi kufanya engine ifanye kazi pia hivyo ita consume mafta zaidi.
Pia namba za cylinder zinahusiana na ulaji mafuta maaana cylinder zaidi zinamaanisha kuna mlipuko zaidi.
4 cylinder itakula mafta machache compared na 6 cylinder.
 
Wakuu ninafuatilia mtandaoni kuhusu uhusiano wa hii topic naishia kuchanganyikiwa tu. Pia nimesearch Jf bahati mbaya sijaona, ukiwa na gari ya cc1990 na ingine ya cc2700 bado the same amount of gas utatumia?

TIA

mkuu...tuchukulie gari za aina moja ila cc ndio tofauti tunaweza kuongelea vizuri ulaji wa mafuta....
kuna bmw 5 series, ipo ya cc2200[520i] na ipo ya cc2500[523i]
1. hizi cc ni cylinder capacity au displacement...yaani ya cc2500 itakuwa inaingiza hewa nyingi na mafuta mengi kwenye combustion chamber kuliko ya cc2000 hapa nazungumzia gari zisizo na turbo.
2.nguvu ya gari inatokana na mlipuko wa mafuta na hewa[oxygen]...mafuta+oxygen nyingi na nguvu ya gari inakuwa kubwa.

KWA HIO ILI KUPATA NGUVU KUBWA KWENYE ENGINE unahitaji mafuta+hewa nyingi kwahio unaongeza CC.

Kuna njia mbadala za kuongeza nguvu ya gari bila kuongeza cc na common ni TURBO CHARGER.
Unaweza kuwa na gari ya cc2000 bila TURBO NA ukawa na gari ya cc2000 YENYE TURBO...kwahio hapo cc ni sawa lakini YENYE TURBO inakuwa na nguvu sana kuliko isiyo na turbo...kwanini??? Kazi ya turbo ni kuingiza extra oxygen na fuel kwenye combustion chamber kwa maana hio gari ile ile ya cc2000 ukiifunga turbo charger itaingiza mafuta mengi na hewa nyingi kuliko ingine isiyo na charger.

?Kwahio kuongeza cc ni kuongeza nguvu kwenye gari ila unaweza kuongeza nguvu kwenye gari bila kuongeza cc kwa kuweka turbo...mfani ni subaru zina cc1600-2000 tu lakini zinakuwa na nguvu kuliko gari nyingi zenye cc2000 au zaidi.

Niongezee diesel na petrol kidogo...petrol inaungua haraka kuliko diesel kwahio gari ya diesel inakuwa nzito kidogo[za sasa hivi ni almost the same diesel/petrol]. kwa kujua hili mara nyingi utakuta gari ile ile ya petrol lets say jaguar x type 2000cc pacha wake wa diesel mara nyingi anakuwa na cc2200 ili kuiongezea nguvu kidogo iwe sawa na petrol
 
Gari kuwa na cc kubwa au ndogo hakuna uhusiano na aina ya mafuta inayotumia moja kwa moja bali design ya mzigo ambao engine itakuwa inabeba. CC maana yake ni Cubic Centimeter yaani ni ukubwa au volume ya cylinders ambamo ndimo mchanganyiko wa mafuta na hewa huchomwa. sasa kama gari ina cc kubwa itakuwa inatumia mafuta mengi kwa sababu ya ukubwa wa cylinder. sasa cc inapatikanaje?

Kwenye gari kuna kitu kinaitwa
bore na stroke. ambapo bore ni kipenyo cha cylinder na stroke ni umbali ambao piston inatumia kusafiri juu hadi chini ya cylinder yaani kwa kitaalam Top dead center hadi bottom dead center. Sasa ili kupata cc ya engine ya gari yako unachukua volume ya one cylinder unazidisha na idadi ya cylinder yaani area of bore x stroke x number of cylinder kama gari yako ina piston 4 au 6 then unazidisha ila uhakikishe units ziko kwenye centimeter hapo utapata cc.

Kuhusu gari ya Petrol na Diese ni kweli diesel ni economical kwani hutumika kidogo kuliko petrol ingawa mfumo wa kisasa wa petrol engines umeboreshwa kufanana na ule wa diesel yaani kutumia nozzel ku inject mafuta kwenye cylinder tofauti na carburettor hapo zamani. Hii ni topic ndefu nitaanzisha uzi kuelezea kwa kirefu tofauti ya Diesel na Petrol Engines.
 
Gari kuwa na cc kubwa au ndogo hakuna uhusiano na aina ya mafuta inayotumia moja kwa moja bali design ya mzigo ambao engine itakuwa inabeba. CC maana yake ni Cubic Centimeter yaani ni ukubwa au volume ya cylinders ambamo ndimo mchanganyiko wa mafuta na hewa huchomwa. sasa kama gari ina cc kubwa itakuwa inatumia mafuta mengi kwa sababu ya ukubwa wa cylinder. sasa cc inapatikanaje?

Kwenye gari kuna kitu kinaitwa
bore na stroke. ambapo bore ni kipenyo cha cylinder na stroke ni umbali ambao piston inatumia kusafiri juu hadi chini ya cylinder yaani kwa kitaalam Top dead center hadi bottom dead center. Sasa ili kupata cc ya engine ya gari yako unachukua volume ya one cylinder unazidisha na idadi ya cylinder yaani area of bore x stroke x number of cylinder kama gari yako ina piston 4 au 6 then unazidisha ila uhakikishe units ziko kwenye centimeter hapo utapata cc.

Kuhusu gari ya Petrol na Diese ni kweli diesel ni economical kwani hutumika kidogo kuliko petrol ingawa mfumo wa kisasa wa petrol engines umeboreshwa kufanana na ule wa diesel yaani kutumia nozzel ku inject mafuta kwenye cylinder tofauti na carburettor hapo zamani. Hii ni topic ndefu nitaanzisha uzi kuelezea kwa kirefu tofauti ya Diesel na Petrol Engines.
Maelezo yako ni mazuri sana,sasa hebu fafanua pale unapokuta gari kama Ipsum new model cc2400 engine vvti inakuaje inakwenda almost sawa na gari ya cc 1500 yaani 1liter inagonga mpaka 13km.
 
Maelezo yako ni mazuri sana,sasa hebu fafanua pale unapokuta gari kama Ipsum new model cc2400 engine vvti inakuaje inakwenda almost sawa na gari ya cc 1500 yaani 1liter inagonga mpaka 13km.

Hizo gari zenye engine za kisasa zote km VVTI, D4-D, GDI n.k zina mfumo mzuri wa ulaji wa mafuta ambao ni electronic contlolled na hata kama ni petrol inatumia nozel na Petrol,air mixture inafanyika kwa ku optimize air ratio zaid kwenye combustion chamber tofauti na zile za zamani ambapo ilikuwa kwa Petrol mchanganyiko huo unafanyika ndani ya cylinder theni unakuwa ignited na spark plug.

nitatoa tofauti moja kuu ya Diesel na Petrol engines nayo ni Ignition point. kwa waliosoma Chemistry watakuwa wanajua hii kitu. sasa Deisel fuel ina low iginition point ndio maana engines zake huwa hewa inaingia kwenye cylinder then inakuwa compressed halafu inakuwa ignited na Diesel fuel moja kwa moja wakati Petrol Engine Petrol and air has to be mixed at a certain proportion then compressed before being ignited by the sparking plug. Hii inafanya Diesel kutumika kidogo kuliko Petrol

Sasa maboresho yaliyofanyika ni pamoja na kufanya mchanganyo uwe bora zaidi yaani premix kwa kuwa elecronic controlled with nozzels and sensors inside the manifold.

ndio maana kwa mafundi wetu tulionao wengi hawajajiendeleza na teknolojia hii ya kisasa badoa wako na zile za zamani gari hizi zinakuwa tabu kwao kutengeneza.
 
mkuu...tuchukulie gari za aina moja ila cc ndio tofauti tunaweza kuongelea vizuri ulaji wa mafuta....
kuna bmw 5 series, ipo ya cc2200[520i] na ipo ya cc2500[523i]
1. hizi cc ni cylinder capacity au displacement...yaani ya cc2500 itakuwa inaingiza hewa nyingi na mafuta mengi kwenye combustion chamber kuliko ya cc2000 hapa nazungumzia gari zisizo na turbo.
2.nguvu ya gari inatokana na mlipuko wa mafuta na hewa[oxygen]...mafuta+oxygen nyingi na nguvu ya gari inakuwa kubwa.

KWA HIO ILI KUPATA NGUVU KUBWA KWENYE ENGINE unahitaji mafuta+hewa nyingi kwahio unaongeza CC.

Kuna njia mbadala za kuongeza nguvu ya gari bila kuongeza cc na common ni TURBO CHARGER.
Unaweza kuwa na gari ya cc2000 bila TURBO NA ukawa na gari ya cc2000 YENYE TURBO...kwahio hapo cc ni sawa lakini YENYE TURBO inakuwa na nguvu sana kuliko isiyo na turbo...kwanini??? Kazi ya turbo ni kuingiza extra oxygen na fuel kwenye combustion chamber kwa maana hio gari ile ile ya cc2000 ukiifunga turbo charger itaingiza mafuta mengi na hewa nyingi kuliko ingine isiyo na charger.

?Kwahio kuongeza cc ni kuongeza nguvu kwenye gari ila unaweza kuongeza nguvu kwenye gari bila kuongeza cc kwa kuweka turbo...mfani ni subaru zina cc1600-2000 tu lakini zinakuwa na nguvu kuliko gari nyingi zenye cc2000 au zaidi.

Niongezee diesel na petrol kidogo...petrol inaungua haraka kuliko diesel kwahio gari ya diesel inakuwa nzito kidogo[za sasa hivi ni almost the same diesel/petrol]. kwa kujua hili mara nyingi utakuta gari ile ile ya petrol lets say jaguar x type 2000cc pacha wake wa diesel mara nyingi anakuwa na cc2200 ili kuiongezea nguvu kidogo iwe sawa na petrol

Kwahyo kipi ni advisable ili kuliongeza nguvu ya gari?? Kufunga turbo au kuwa na cc kubwa??
 
Hizo gari zenye engine za kisasa zote km VVTI, D4-D, GDI n.k zina mfumo mzuri wa ulaji wa mafuta ambao ni electronic contlolled na hata kama ni petrol inatumia nozel na Petrol,air mixture inafanyika kwa ku optimize air ratio zaid kwenye combustion chamber tofauti na zile za zamani ambapo ilikuwa kwa Petrol mchanganyiko huo unafanyika ndani ya cylinder theni unakuwa ignited na spark plug.

nitatoa tofauti moja kuu ya Diesel na Petrol engines nayo ni Ignition point. kwa waliosoma Chemistry watakuwa wanajua hii kitu. sasa Deisel fuel ina low iginition point ndio maana engines zake huwa hewa inaingia kwenye cylinder then inakuwa compressed halafu inakuwa ignited na Diesel engine moja kwa moja wakati Petrol Engine Petrol and air has to be mixed at a certail proportion then compressed before being ignited by the sparking plug.

Sasa maboresho yaliyofanyika ni pamoja na kufanya mchanganyo uwe bora zaidi yaani premix kwa kuwa elecronic controlled with nozzels and sensors inside the manifold.

ndio maana kwa mafundi wetu tulionao wengi hawajajiendeleza na teknolojia hii ya kisasa badoa wako na zile za zamani gari hizi zinakuwa tabu kwao kutengeneza.

Mkuu uko deep sana asante kwa elimu hii
 
Ukiona gari zinatofautina engine kiasi hicho, most likely hiyo ya cc 1900 itakuwa ni ya Petrol na hiyo ya cc2700 itakuwa ni ya Diesel. Diesel ni ngumu kuwaka na haitoi moto mkali kama wa Petrol, so engine inabidi iwe kubwa ili kuweza kupata moto mkubwa wa kuzungusha engine.

Pia gari ya Diesel inaweza kuwa na engine kubwa isiyo na nguvu nyingi lakini ikawa na towing capacity kubwa, yani uwezo wa kubeba mizigo au kuvuta tela. Ndio maana gari ya diesel yenye engine kubwa unaweza ukaondokea gia namba mbili wakati gari ya petrol inakuhitaji uondokee na gear namba moja.

Gari ya Petrol inakula mafuta mengi kwa kuwa mafuta yote yanayoenda huchomwa. Nasikia gari ya diesel huwa inarudisha mafuta ili yaunguzwe raundi nyingine, sina uhakika na hili. Ngoja wataalam zaidi waje.

hujui unachokisema migari ya diesel ndo inaongoza kutoa moshi
 
Sasa ninataka kujua cc 1000 inakula mafuta 1lita kwa km ngapi?
cc 2000 pia.
Ahsante
 
Wakuu ninafuatilia mtandaoni kuhusu uhusiano wa hii topic naishia kuchanganyikiwa tu. Pia nimesearch Jf bahati mbaya sijaona, ukiwa na gari ya cc1990 na ingine ya cc2700 bado the same amount of gas utatumia?

TIA
Kwanza elewa maana ya maneno yanayotumika kwa vile yamebeba maudhui ya kiufundi. cc kwa maana ya cubic centimeter ambayo ni ukubwa wa cylinder kati ya pale piston inapokuwa mwisho chini B.D.C. (Bottom dead center) na T.D.C (Top dead center) ambamo ndilo eneo la kuchanganyia mafuta na hewa na kufanya mlipuko. hivyo katika mazingira ya kawaida, magari yanayotumia mafuta ya aina moja yenye ukubwa tofauti CC wa injini, tegemea ulaji wa mafuta uwe tofauti kufuatana na ukubwa, japo kuna mambo mengine yanayochangia vile vile kama vile Automatic na Manual drive, Electronic fuel injection na ile ya kawaida. Ukitaka kujua zaidi itabidi uingie darasani usome motor vehicle mechanics ili ujue zaidi.
 
Hizo gari zenye engine za kisasa zote km VVTI, D4-D, GDI n.k zina mfumo mzuri wa ulaji wa mafuta ambao ni electronic contlolled na hata kama ni petrol inatumia nozel na Petrol,air mixture inafanyika kwa ku optimize air ratio zaid kwenye combustion chamber tofauti na zile za zamani ambapo ilikuwa kwa Petrol mchanganyiko huo unafanyika ndani ya cylinder theni unakuwa ignited na spark plug.

nitatoa tofauti moja kuu ya Diesel na Petrol engines nayo ni Ignition point. kwa waliosoma Chemistry watakuwa wanajua hii kitu. sasa Deisel fuel ina low iginition point ndio maana engines zake huwa hewa inaingia kwenye cylinder then inakuwa compressed halafu inakuwa ignited na Diesel fuel moja kwa moja wakati Petrol Engine Petrol and air has to be mixed at a certain proportion then compressed before being ignited by the sparking plug. Hii inafanya Diesel kutumika kidogo kuliko Petrol

Sasa maboresho yaliyofanyika ni pamoja na kufanya mchanganyo uwe bora zaidi yaani premix kwa kuwa elecronic controlled with nozzels and sensors inside the manifold.

ndio maana kwa mafundi wetu tulionao wengi hawajajiendeleza na teknolojia hii ya kisasa badoa wako na zile za zamani gari hizi zinakuwa tabu kwao kutengeneza.

Mkuu, kuna uhusiano wowote wa sensors zilizoanza kuchoka na ulaji wa mafuta?
 
Back
Top Bottom