Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Gari ya diesel in return pipe ambayo hurudisha mafuta ya ziada ambayo hayakuingia kwenye combustion chamber lkn hili wataalam wanaweza wakaliweka vizuri zaidiUkiona gari zinatofautina engine kiasi hicho, most likely hiyo ya cc 1900 itakuwa ni ya Petrol na hiyo ya cc2700 itakuwa ni ya Diesel. Diesel ni ngumu kuwaka na haitoi moto mkali kama wa Petrol, so engine inabidi iwe kubwa ili kuweza kupata moto mkubwa wa kuzungusha engine.
Pia gari ya Diesel inaweza kuwa na engine kubwa isiyo na nguvu nyingi lakini ikawa na towing capacity kubwa, yani uwezo wa kubeba mizigo au kuvuta tela. Ndio maana gari ya diesel yenye engine kubwa unaweza ukaondokea gia namba mbili wakati gari ya petrol inakuhitaji uondokee na gear namba moja.
Gari ya Petrol inakula mafuta mengi kwa kuwa mafuta yote yanayoenda huchomwa. Nasikia gari ya diesel huwa inarudisha mafuta ili yaunguzwe raundi nyingine, sina uhakika na hili. Ngoja wataalam zaidi waje.
Labda gari ikiwa na cc kubwa kiwango cha mafuta kinachoingia kwenye cylinder ili kunguzwa ni kikubwa kuliko ya kile cha gari yeye cc ndogo. MF cc kubwa inachukua kijiko cha chakula cha mafuta kwa muunguzo mmoja kwa cylinder lkn cc ndogo inachukua nusu kijiko cha chai kwa muunguzo mmoja kwa cylinder, huo ni muono wangu wa kawaida tu.Mkuu ungefafanua technically kabisa ili tuelewe.
Hata mimi mwanzo nilikuwa sijui maana ya cc mpaka nilipokuja kusoma kwenye mtandao. Na baada ya kusoma sijaweza kurelate cc na ulaji wa mafta maana cc maana yake kumbe ni cubic centimetre na inapimwa kuanzia pale piston inapokuwa imecmama (dead) mpaka inapo rotate hadi mwisho.
Kwa mantiki hiyo ningependa mtu anielezee kuna uhusiano gani na utumiaji wa mafta
Nimesoma maelezo yako vizuri sana. Asante kwa ufafanuzi.Gari kuwa na cc kubwa au ndogo hakuna uhusiano na aina ya mafuta inayotumia moja kwa moja bali design ya mzigo ambao engine itakuwa inabeba. CC maana yake ni Cubic Centimeter yaani ni ukubwa au volume ya cylinders ambamo ndimo mchanganyiko wa mafuta na hewa huchomwa. sasa kama gari ina cc kubwa itakuwa inatumia mafuta mengi kwa sababu ya ukubwa wa cylinder. sasa cc inapatikanaje?
Kwenye gari kuna kitu kinaitwa bore na stroke. ambapo bore ni kipenyo cha cylinder na stroke ni umbali ambao piston inatumia kusafiri juu hadi chini ya cylinder yaani kwa kitaalam Top dead center hadi bottom dead center. Sasa ili kupata cc ya engine ya gari yako unachukua volume ya one cylinder unazidisha na idadi ya cylinder yaani area of bore x stroke x number of cylinder kama gari yako ina piston 4 au 6 then unazidisha ila uhakikishe units ziko kwenye centimeter hapo utapata cc.
Kuhusu gari ya Petrol na Diese ni kweli diesel ni economical kwani hutumika kidogo kuliko petrol ingawa mfumo wa kisasa wa petrol engines umeboreshwa kufanana na ule wa diesel yaani kutumia nozzel ku inject mafuta kwenye cylinder tofauti na carburettor hapo zamani. Hii ni topic ndefu nitaanzisha uzi kuelezea kwa kirefu tofauti ya Diesel na Petrol Engines.
Yeah na kuna brevis pia 2500/3000cc ni petrolMkuu inawezekana mengine uliyoyasema ni sahihi lakini ili la kusema gari ikiwa na Cc kubwa ni ya diesel sio kweli. Kuna magari ya diesel yana cc 2,700 na wakati huo kuna magari ya petrol yana cc 4,700, mfano VX V8. Hapo sijui unasemaje.
Tiba
Mkuu kama sensors za fuel au ignition system zina tatizo utajuaje? Je mafundi wa mtaani wanaweza jua hili?kwasababu gari yangu imeongeza matumizi ya mafuta na fundi wangu naona kama imeshamshinda.Kama ni sensors za Fuel system na au ignition system kuna uhusiano mkubwa sana mkuu.
Mkuu @prondo njoo utoe jibu hapaNimesoma maelezo yako vizuri sana. Asante kwa ufafanuzi.
Naomba nijuze.. ivi mafuta ya Petrol yanayouzwa kwenye vituo vya kuuzia mafuta zinatofautiana??..
Mfano: baadhi ya vituo unakuta petrol hii ni "unleaded"
Kwenye kituo kingine utakuta Petrol ni "super"
Wengine utakuta ni " Premium"
Tofauti na Diesel huwa naona ni diesel tu.
Je hizi ni brand name tu au huwa zinatofautiana ubora.
Kama kuna utofauti wa ubora. Ipi ipo recomended, kwa uzoefu wako.
Thank you in advance.
Jibu ni rahisiMaelezo yako ni mazuri sana,sasa hebu fafanua pale unapokuta gari kama Ipsum new model cc2400 engine vvti inakuaje inakwenda almost sawa na gari ya cc 1500 yaani 1liter inagonga mpaka 13km.
Ufafanuzi mzuri.Jibu ni rahisi
Kuna uwezekano mkubwa gari yenye Engine ndogo kula mafuta mengi ukilinganisha na yenye Engine kubwa na sababu ni hizi
1. Gari inakula mafuta mengi unapotembelea gia kubwa yaani Nr .1
2. Kwahiyo gari ndogo pahala unapotembelea gia Nr 1 au Nr 2 kwa gari yenye Engine kubwa unatembelea gia Nr 4 au tano.
3. Ngari yenye Engine ndogo inabidi wakati mwingi ukanyage mafuta mpaka mwisho wakati Engine kubwa ukikanyaga kidogo unapata mwendo unaouhitaji
4. Mambo mengine yanayochangia ulaji wa Mafuta Aina ya Matairi, Upepo katika matairi, Barabara (mzuri au mbovu)
Kasi ya Upepo, Kufungua kioo pia kunachagia ulaji wa Mafuta, Mkato wa gari (yaani gari yenye kioo cha Flat kama Defender itakula mafuta mengi kulikoni yenge round Glasses
Ziko Fakto nyingi
ni ukweli petrol ikichomwa inakuwa imechomwa ila diesel ikichomwa inarud tenaUkiona gari zinatofautina engine kiasi hicho, most likely hiyo ya cc 1900 itakuwa ni ya Petrol na hiyo ya cc2700 itakuwa ni ya Diesel. Diesel ni ngumu kuwaka na haitoi moto mkali kama wa Petrol, so engine inabidi iwe kubwa ili kuweza kupata moto mkubwa wa kuzungusha engine.
Pia gari ya Diesel inaweza kuwa na engine kubwa isiyo na nguvu nyingi lakini ikawa na towing capacity kubwa, yani uwezo wa kubeba mizigo au kuvuta tela. Ndio maana gari ya diesel yenye engine kubwa unaweza ukaondokea gia namba mbili wakati gari ya petrol inakuhitaji uondokee na gear namba moja.
Gari ya Petrol inakula mafuta mengi kwa kuwa mafuta yote yanayoenda huchomwa. Nasikia gari ya diesel huwa inarudisha mafuta ili yaunguzwe raundi nyingine, sina uhakika na hili. Ngoja wataalam zaidi waje.
Petrol na diesel yote ni mafuta ila wakati wa uchomwaji baadhi hurudishwa kwenye tank na kwani sio mafuta yote uchomwa kwa wakati mmoja mengine hubakia na kurudishwa kwenye tank, mfano mzuri ni toyota spacio ambapo gari hii utumia petrol, ukifungua mfuniko wa tank wakati iko sailensa utaona baadhi ya mafuta yanachuruzika kutoka kwa ndani kidogo ambapo kuna pipe yakurudisha mafuta na kuelekea kwenye tankni ukweli petrol ikichomwa inakuwa imechomwa ila diesel ikichomwa inarud tena
hapo kwenye red, inakuwaje?Jibu ni rahisi
Kuna uwezekano mkubwa gari yenye Engine ndogo kula mafuta mengi ukilinganisha na yenye Engine kubwa na sababu ni hizi
1. Gari inakula mafuta mengi unapotembelea gia kubwa yaani Nr .1
2. Kwahiyo gari ndogo pahala unapotembelea gia Nr 1 au Nr 2 kwa gari yenye Engine kubwa unatembelea gia Nr 4 au tano.
3. Ngari yenye Engine ndogo inabidi wakati mwingi ukanyage mafuta mpaka mwisho wakati Engine kubwa ukikanyaga kidogo unapata mwendo unaouhitaji
4. Mambo mengine yanayochangia ulaji wa Mafuta Aina ya Matairi, Upepo katika matairi, Barabara (mzuri au mbovu)
Kasi ya Upepo, Kufungua kioo pia kunachagia ulaji wa Mafuta, Mkato wa gari (yaani gari yenye kioo cha Flat kama Defender itakula mafuta mengi kulikoni yenge round Glasses
Ziko Fakto nyingi
Aina ya Matairi nilikusudia Profile ya Pira wenyewe (Umekakwa na Kashata kubwa kama mpira wa Offroad au ya kwaida tu)hapo kwenye red, inakuwaje?
Maelezo yako ni mazuri sana,sasa hebu fafanua pale unapokuta gari kama Ipsum new model cc2400 engine vvti inakuaje inakwenda almost sawa na gari ya cc 1500 yaani 1liter inagonga mpaka 13km.
VVTI ni ya zaman kidogo mpya.ni hizi D4 au D4D kwa upande wa toyota GDI kwa mitsubishi na TDI kwa audi na bmwHizo gari zenye engine za kisasa zote km VVTI, D4-D, GDI n.k zina mfumo mzuri wa ulaji wa mafuta ambao ni electronic contlolled na hata kama ni petrol inatumia nozel na Petrol,air mixture inafanyika kwa ku optimize air ratio zaid kwenye combustion chamber tofauti na zile za zamani ambapo ilikuwa kwa Petrol mchanganyiko huo unafanyika ndani ya cylinder theni unakuwa ignited na spark plug.
nitatoa tofauti moja kuu ya Diesel na Petrol engines nayo ni Ignition point. kwa waliosoma Chemistry watakuwa wanajua hii kitu. sasa Deisel fuel ina low iginition point ndio maana engines zake huwa hewa inaingia kwenye cylinder then inakuwa compressed halafu inakuwa ignited na Diesel fuel moja kwa moja wakati Petrol Engine Petrol and air has to be mixed at a certain proportion then compressed before being ignited by the sparking plug. Hii inafanya Diesel kutumika kidogo kuliko Petrol
Sasa maboresho yaliyofanyika ni pamoja na kufanya mchanganyo uwe bora zaidi yaani premix kwa kuwa elecronic controlled with nozzels and sensors inside the manifold.
ndio maana kwa mafundi wetu tulionao wengi hawajajiendeleza na teknolojia hii ya kisasa badoa wako na zile za zamani gari hizi zinakuwa tabu kwao kutengeneza.