Kuna utajiri mkubwa wa kusaka dola za Adsense online lakini sasa...

Kuna utajiri mkubwa wa kusaka dola za Adsense online lakini sasa...

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
1645899888611.png


Katika ulimwengu huu wa sasa teknolojia imekua kubwa, baadhi ya vijana wamejiajiri katika blogging, youtube, n.k.

kwa hapa kwetu wapo a aina mbili

Aina ya kwanza - kwa upande wa bloggers wengi bado wapo google adsense lakini wengi wao wanacheza wanapokea laki 2 jadi laki 8 kwa mwezi, hali hii imefanya wengi kuhamia youtube kwenye nafuu, kuna kipindi youtube ilimpa millard ayo mkwaja mrefu miaka ya 2013 hadi 2015 alikuwa anapiga views kijiji ila saizi ushindani ni mkubwa na pia mabando yamepanda bei ni changamoto kiasi, pia kuna adsense ya kwenye apps nayo imetulia maana ushindani ni mdogo ukilenga penye uhitaji unaogelea pesa.

Aina ya pili - hawa wanatengeneza blog hata haina mpangilio inakuwa na kitufe ambacho mtu akiminya pesa imeingia, wanashare link za blog zao kwa kutegesha picha zinazoshawishi kuminya kwenye makundi ya facebook ili mtu aingie kwenye blog zao aende kuminya sehemu ambayo inawaingizia pesa, mfano kwenye group la fb unakutana na picha ambayo iliyopachikwa kitufe cha video, kwa akili yako unadhani hio ni video, utaminya hapo utapelekwa kwenye blog ambayo ina picha ile ile uliyoina, unaminya hio picha ukidhani ni video kumbe imepachikwa link ya tangazo, hapo tayari ukiminya blogger kapiga pesa.. kindi hili wanapiga hadi milioni 20 kwa mwezi, adsense walipowastukia mchezo wao wakahamia propeller ads, huko nako wakazinguliwa wakahamia adsterra, wakazinguliwa hiko kwa sasa wapo gg agency, mtu analaza laki 6 kila siku utadhani mchezo.

miaka hiyo wakiwa google adsense ikifika tarehe 22 ndio ilikuwa siku ya malipo, unakuta dogo ana miaka 19 amaenda kuchukua milioni 4 na upuuzi kwenye lile dirisha la kupokea hela kwa western union, hapo walikuwa wanapiga milioni 4.x kwa maksudi maana ilikuwa ukizidisha hapo basi western union inakua ngumu kutoa hela, sasa hao bloggers wakaja kufanya uchunguzi wa kuruka hicho kiunzi ndio wakajua kuna njia ya bank transfer inayorusu kutoa pesa zaidi na pesa zinaingia moja kwa moja benki,

Hii watu walikuwa wanapiga milioni 20 kila mwezi, benki pendwa ilikuwa ni Equity Bank ambayo waliweza kuungansha hio njia ya bank transfer, watu wa bank walikuwa wanashangaa sana. Mpaka sasa watu wanaendelea kupiga dollar ila wamehamia gg agency huko naskia wanalipa kwa bitcoins then unaziuza na kuzibadili ziwe tshs kwa watu wanaonunua bitcoins sehmu kama Remitano, Coinbase, n.k.

Huku mtu akikusikia anaweza kuona ni rahisi ila asikwambie mtu huku mambo yanabadilka sana, njia ikianz kutumika leo kupiga dollar unakuta inakaa miezi sita tu baada ya hapo ishachuja, hizi njia wanaziita "triki", ili kupata hizo triki inabidi uwe na marafiki wa vikundi tofauti vya bloggers hawa maana nao huwa wana vikundi vyao na pia uwe na pesa ya kulipia kufundishwa hizo triki, triki zinauzwa mpaka milioni huko.

Pia kuna visasi na umafia wa hali ya juu sana, unakuta kuna wale waliokuwa wananyimwa triki, wamepambana wakapata triki zao wakaanza kupiga dollar, hizo triki huwa hawawapi waliowanyima enzi hizo, kazi inakuwa ni kuposti kwenye magroup yao ya whatsapp dollar wanazopiga ila hawatoi mbinu, hii kitu huwa inakasirisha sana wale waliowanyimaga triki, kuna bloggers walikuwa wanalaza dolla za kutosha miaka ya 2015 lakini baada ya triki zao kuchujaleo hii wanatia huruma uchumi umeyumba, so huku hkunaga uhakika wa kesho.

Binafsi nilikuwa natamani huko sehemu ya pili ila ilishindikana kwasababu zangu binafsi kulingana na kazi ilivyo.


HITIMISHO:

Kundi la kwanza kuna uhakika na usalama, mambo yapo wazi ila linahitaji juhudi na uvumilivu sana maana unaweza kuanza kupiga hela ya maana kidogo baada ya msoto wa miaka mitatu., baada ya hapo inaweza kuwa kazi rasmi ya kuitegemea kukuingizia kipato kwa miaka ijayo.

kundi la pili hilo halina uhakika maana mambo yanaenda kwa triki ambazo hazipo wazi na huwa zinafungiwa sana, yaani kufumba na kufumbua triki inaweza kupigwa pini. Uzuri wake ni kwamba ukiwa na hio ramani utapiga pesa nyingi tu, ila ndio hivyo tena, trick kwa tafsiri yake ni kutoka kiingereza ni ujanja, hizo janja janja huwa hazidumu, wapo watu waliokula maisha mithiri ya peponi miaka ya juzi tu hapo 2018 lakini kwa sasa wana maisha magumu ambayo yamegeuka kuwa furaha kwa wale waliokuwa wakiwanyima hizo triki, ni umafia na visasi, na hawa ambao miaka hii wameotea mbinu si ajabu miaka ya mbele yakawakuta.
 
Online kuna pesa sana hasa kwa kwetu Tanzania ambapo wengi bado hawana uelewa wa hayo mambo hivyo kufanya ushindani kuwa mdogo na was kawaida.

Anzisha huduma yoyote, ipeleke online kisha cheza na SEO (Search engine optimization) kibongo bongo ukiwa serious utauza sana.

Jiongeze weka na Adsense kwenye blog yako.


Ukicheki comment nyingi hapo juu inadhihirisha kabisa bongo watu bado wamelala kifikra hasa katika kutumia fursa za mtandao.


Wengi watashtuka too late.
 
Umeongea utafikiri Ni kitu rahisi mnoooo
Hakuna sehemu nimeandika ni rahisi, kuna watu wana struggle mwaka wa tatu huu hilo kundi ka pili, mtu anaambulia laki kwa mwezi na hapo kajikaza sana, unamwambia atafute shughuli nyingine yeye anakwambia kina fulani wanapiga dola ndefu nae atafikia huko, lakini ukweli ni kwamba anapewa triki ambazo zilishaoza, umri unaenda tu anakuwa kama wale watu wanaotafuta rupia za mjerumani.

kwa kundi la kwanza nako kunahitaji kujitoa si mchezo, nakumbuka kina millard ayo na issa michuzi walianza kipindi kile unalipia internet cafe ili utumie internet, matunda walianza kuyala baada ya miaka mitatu hivi.

Millard alipokosea ni alipoacha kupost habari za Diamond na wcb, kwa kufanya hivi aliacha pengo kubwa sana na kuna watu walilijaza na wakaanza kumpiga kanzu Millard,, kwa sasa naona akili zimemrudi kaanza kumpost Diamond na wcb 😂😂, hii kazi huwa haihitaji utimu.
 
Hakuna sehemu nimeandika ni rahisi, kuna watu wana struggle mwaka wa tatu huu hilo kundi ka pili, mtu anaambulia laki kwa mwezi na hapo kajikaza sana, unamwambia atafute shughuli nyingine yeye anakwambia kina fulani wanapiga dola ndefu nae atafikia huko, lakini ukweli ni kwamba anapewa triki ambazo zilishaoza, umri unaenda tu anakuwa kama wale watu wanaotafuta rupia za mjerumani.

kwa kundi la kwanza nako kunahitaji kujitoa si mchezo, nakumbuka kina millard ayo na issa michuzi walianza kipindi kile unalipia internet cafe ili utumie internet, matunda walianza kuyala baada ya miaka mitatu hivi. Millard alipoacja kupost habari za Diamond aliacha pengi kubwa sana kuna watu walilijaza wakaanza kumpiga kanzu Millard, kwa sasa akili zimemrudi kaanza kumpost Diamond 😂😂
Nilikuwa namjibu huyo anajiita Mr. Purpose.

Millard hategemei AdSense sasa hivi kwasababu ana access ya kupata Direct Ads kutoka kwenye makampuni.
 
Nilikuwa namjibu huyo anajiita Mr. Purpose.

Millard hategemei AdSense sasa hivi kwasababu ana access ya kupata Direct Ads kutoka kwenye makampuni.
ok.

Ila kwa upande wa millard ayo ka haso sana kiukweli na watu tumeona, ana kila haki ya kupata kikubwa ili awe inspiration kwa vijana.

Kaanza hizi blogging na youtube kitambo sana, enzi hizo ilikuwa unafanya kwa taaluma yako kuzidi pesa maana hata gharama za kuendesaha blog zilikuwa kubwa.

Mbegu aliyoipanda ilianza kumpa matunda baada ya miaka mitatu ama minne.

Kwa ushauri wangu saizi mtu akijikita kwenye michezo Simba na Yanga soko bado halijachuja.
 
Back
Top Bottom